Makala Jr
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 3,395
- 1,110
Hii ni kauli aliyoitoa alipokuwa anaongea na waandishi wa habari leo. Dr.Edward Hoseah amesema ushiriki wa jamii ya Watanzania katika vita dhidi ya rushwa umekuwa mdogo..."watu wanalalamika tu ooh yule mtoa rushwa,yule fisadi,maneno matupu hayatusaidii "......Hivyo ndivyo alivyosema Mkurugenzi wa taasisi ya kuzuia na Kupambana na rushwa (TAKUKURU) nchini Tanzania......source:star tv...........MY TAKE................Kama taasisi kama TAKUKURU yenye wataalamu wanaolipwa kwa ajili ya kuzuia na kupambana na rushwa hawawezi kuifanya kazi hiyo basi wanalipwa kwa kazi gani? Watu wasioweza kutafuta ushahidi EPA,RICHMOND,MEREMETA,KAGODA na rushwa katika uwekezaji wa ardhi badala yake wanataka wananchi wanaodhurika kwa rushwa na kulalamika wawapelekee ushahidi? Kweli TAKUKURU ni toothless dog kwani ni vizuri wananchi kuripoti kuhusu rushwa lakini siyo kutoa ushahidi kwani hawana utaalamu wa kutosha.Kwa mwendo huu,kuna matumaini ya kutokomeza rushwa Tanzania?