Kumbe Waafrika tuna Mungu wetu, tofauti na huyo wa wenzetu.
Naona hata wanaobisha kuwa hakuna Mungu mada hii wameikubali.
Sasa si wangesema tu kuwa wanamtambua huyu Mungu wa Waafrika.
Kinachosumbua huyu Mungu wa waafrika kajificha sana, habari zake hazipatikani ki urahisi, mpaka uwe msomi sana ndo ujue habari zake.
Sasa sisi watu wa chini tutapataje kujua habari zake, sisi ambao kiingereza hatukijui wala kisomo cha chuo.
Mwenye kuweza kusaidia ili tumwelewe huyu Mungu wa Waafrika tafadhali atusaidie.
Yaani kupata Bible yake, ili nasisi tuisome tupate maarifa kama ya wenzetu.
Tunahitaji sana kumtambua huyu Mungu wetu Waafrika.
Msaada tafadhali.