DOWANS wameingilia mlango wa nyuma. Wameingia mkataba na SONGAS. Umeme wao wanawauzia SONGAS. Kisha SONGAS inaiuzia TANESCO. Tafakari.
Al Adawi amesema amekuja kuongea na tanesco, wala hana shida na ngeleja. Na amesema yuko tayari kupunguza gharama badala ya bilioni 94 tulizotakiwa kumipa basi atatuunguzia kidogo waau tupate kiasi cha kuwalipa waathirika wa makombora gongo la mboto.
sasa kama jana tu ametangaza kuongea na tanesco na leo mtambo umewashwa, hiyo ni kusema aliitisha waandishi wa habari huku akiwa amemaliza mazungumzo na tanesco, vinginevyo watakuwa wamezungumza fasta kama kawaida yao inapokuja suala la dharura ni wepesi wa kufanya negotiation na kufikia maamuzi.
Nadhani huajielewa dahana ya soko huria. IMF ilisema serikali ijotoe katika kufanya biashara na iruhusu private sectort kufanya shughuli. IMF haimaanishi kuachia wezi wapore au mikataba ya hovyo, wanachosema ni serikali isimamie shughuli na isijishirikishe kama mfanyabiashara.
Marekani waliachia soko huru bila serikali kuingilia matokeo yake ni economical crisis tunayoiona. Obama ameingilia kati na sasa pale Wall street kuna rules and regulations.
Margreth Sacher alipobinafsisha kila kitu UK, ilifika mahali wananchi wake wakamwambia no! kaa pembeni, hawezi kubinafsisha Posta na Reli. Elewa kuwa soko huria si soko holela na serikali lazima iwajibike kuhakikisha wananchi wake wanatendewa haki na wenye pesa.
Hakuna tatizo la shirika binafsi kuuzi umeme TANESCO, tatizo ni kuwa akina RA hawafanyi biashara ni matapeli wanaotaka kulipwa kwa hila mabilioni ya fedha. Bado serikali ingeliweza kuwa ''BAIL OUT'' TANESCO wanunue mtambo kama wa Dowans, lakini kwa hila BoT wame bail out Richmond/Dowans kwa sababu tu kuna watu wachache wanafaidika na mgao wa RA. hapa ndipo hasira za wananchi zilipo, si privatisation! Kutokana na madudu ya RA/EL leo tunapandishiwa bei ya umeme ili tumlipe RA. Jiulize, hivi kama TANESCO haina pesa za kujiendesha, inapata wapi pesa billion 100 kumlipa Dowans! huu si upuuzi wa kutufanya matutusa.
Sasa, tunasikia umeme umewashwa, maana yake ni kuwa Dowans inatambuliwa na kama inatambuliwa Richmond inapata uhalali, na ni kwa uhalali huo Lowasa anakuwa safi, Zigo linakwenda kwa Mwakyembe na Sitta wazalendo wenye uchungu na nchi hii.
Kwa taarifa tu, hujuma za umeme zimeingia Mabwawani, Songas n.k ili kujenga mazingira ya Dowans kuzalisha umeme. Tulijua kuna jambo pale January alipoteuliwa kuwa mwenyekiti wa nishati, akaanza na safari mtera, akaja na wazo la mkataba w miezi 6, Ngeleja akasema kunnuua Dowans si tatizo na kama watauza umeme hakuan shida, jenerali kaingia kinyemela Dar, jenerata zinawashwa siku inayofuata!
Tukimruhusu RA aendelee hivi tujue kuwa tunamuandaa Jenerli Farah Aideed, naye alikuwa na power kama ya RA.
Bora tukae gizani kuliko kumhalalisha fisadi huyu. Tusimfundishe panya kula sufi ipo siku atatafuna vidole.
sad!
Tukiendelea kuruhusu mediocre performance toka kwa hizi Serikali za CCM miaka nenda miaka rudi nchi yetu itabaki nyuma sana kimaendeleo huku hao wanaojiita Viongozi wakijiendelea kujilimbikizia mali wao, familia zao na marafiki wao wa karibu. Rwanda waliuana kwa mamilioni mwaka 1994 lakini sasa hivi nchi hiyo katika maendeleo inafanya vizuri sana ukilinganisha na sisi "wenye amani" ya miaka nenda miaka rudi. I am not demanding too much ninachotaka kuwe na kuwajibika pale hawa wanaojiita Viongozi wanaposhindwa kutimiza wajibu wao kama Viongozi wa nchi au wizara mbali mbali. Tumeona kwa mfano mabomu ya Mbagala miaka miwili iliyopita hakuna aliyewajibika kwa kujiuzulu au kufukuzwa kazi, miaka miwili baadaye mabomu ya gongo la mboto wamekuwa na kiburi cha kuweza hata kutamka kwamba "sijiuzulu" si ajabu miaka miwili mingine mabomu hayo yatalipuka tena katika moja ya sehemu hizo au inaweza kuwa Lugalo.
Rais anasimama na kuwadanganya Watanzania kwamba hawajui wamiliki wa Dowans wakati ni uongo wa hali ya juu. Hivi wewe kama Rais wa nchi baada ya sakata lote hili la Dowans hata kama huwajui wamiliki wa Dowans huwezi kuwauliza wasaidizi wako toka wizara ya nishati wakupe briefing kuhusu Dowans na hatimaye uwajue wamiliki wa Dowans? Iweje Ngeleja awajue wamiliki wa Dowans wakati Kikwete anadai hawajui? Kama wewe unaruhusu uzembe na ufisadi wa hali ya juu unaofanywa na hii Serikali iliyopo madarakani kila la heri lakini wengine hatukubaliani na hali hiyo na hivyo tuna haki ya kujadili hapa bila wewe kutaka kuonyesha kwamba...we're demanding too much from them.
Mramba alisema hata watanzania tule majani ilikuwa lazima ndege ya raisi inunuliwe, mimi nimefikiwa uamuzi wa kukaa gizani kusubiri mvua ya Mungu ijaze mabwawa ya Mtera na Kidatu kuliko umeme wa RA, JK na serikali yake wametusaliti na kututupa kamwe si Mungu, na njia pekee ya kutuokoa watanzania kwa sasa nikupitia matatizo.
AM WAITING KWA HAMU KUBWA SIKU TUTAKAYOINGIA BARABARANI KUWATOA HAWA WATAWALA BOMU....:rain:
...thanks for the infomation!!! i'm eager for more and more infoz!Wakuu hivi ninavyoandika ni kuwa mtambo mmoja wa Dowans aina ya LM6000 PD 40MW uliopo site A nyuma ya ghorofa la Tanesco umewashwa na hadi sasa unazalisha 37MW.
Nitawaletea habari zaidi lakini nina uhakika kuwa hawataweza kutembeza mitambo yao yote kutokana na sababu ambazo nitazieleza hapo baadae. Kiufundi mtambo huo kwa sasa ume-substitute mtambo wa Songas ambao kwa sasa upo down kutokana na kupata ajali ya moto hapo jana.
Habari kamili baadae.
Wakuu hivi ninavyoandika ni kuwa mtambo mmoja wa Dowans aina ya LM6000 PD 40MW uliopo site A nyuma ya ghorofa la Tanesco umewashwa na hadi sasa unazalisha 37MW.
Nitawaletea habari zaidi lakini nina uhakika kuwa hawataweza kutembeza mitambo yao yote kutokana na sababu ambazo nitazieleza hapo baadae. Kiufundi mtambo huo kwa sasa ume-substitute mtambo wa Songas ambao kwa sasa upo down kutokana na kupata ajali ya moto hapo jana.
Habari kamili baadae.
</p>Hiii nchi kweli kiraka...
Mkuu jana nilikupinga sana, samahani.... nimeuliza the same question, KUUNGUA SONGAS NA KUWASHWA DOWANS KUNATUAMBIA NINI??
INAKUAJE MTU MWENYE KESI NA SISI AND ALL SORTS OF TROUBLES AKUBALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SISI?? HOW COME MITAMBO ILIUZWA KWA KAMPUNI YA KIGENI IBAKI UBUNGO? ILIKUA INALINDWA KWA GHARAMA YA NANI?