DOWANS waanza kulipwa rasmi na serikali

DOWANS waanza kulipwa rasmi na serikali

Kwa serikali hii lolote linawezekana,sauti ya mwisho hapa nchini ni sauti ya Rais pekee,kama yeye hajasema kuwa hyo pesa hailipwe bs ujue hakuna la maana hapo,kuna mda nafikiria kama mkuu wetu nae anaongozwa na kupewa amri na watu fulani

Inawezekana mpaka leo hujamfahamu raisi wako!!!!? Hili ndio tatizo hasa la waTZ na ndio sababu wanashindwa kuchukua maamuzi thabiti kama ya wenzetu Sierra Leon, Tunisia, Misri, Libya e.t.c ..........

Mmmmmh .........!!! Bado nafikiri tatizo ni nini hasa kama ambavyo masanja nafikiri kama ...
 
kumbe hata mwizi ni haki yake kuiba sio?

TUNALIPA DOWANS kutokana na KIBURI, JEURI, FITNA NA SIASA ZA CHUKI ZA SITTA na kundi lake la CCJ.

Ile Report ya Richmond ilipikwa na ikatangazwa kiufundi sana pale Bungeni.
SISI walalahoi tulimsifia sana MWAKYEMBE. Leo tunalipa Billion 96 na tunalalama nini????? Tulishabikia sana. Tuliwaona Mashujaa wale wabunge waliotaka mkataba uvunjwe. Jamani MKATABA ni MKATABA siyo lele mama. Ndiyo imetufikisha hapa. MASIFA KIBAO leo tunainamisha vichwa vyetu. Sisi vijana tusipotahadhali tunatumika vibaya kwa kibwege ----- tu.
 
Wengine tuliyasema haya toka 2009-2010. Wangelilipwa kipindi kile tungelilipa Billion 95 tukapata mitambo ikawa yetu. Sasa mitambo tunakodi na deni tunalipa kweli wajinga ndio waliwaoao
 
Zitto alionya kuvunja mkataba wanasheria uchwara wakajifanya kubisha, sasa kwenye court ya kimataifa ya biashara na ya ndani tumekula mweleka na gharama ya fidia ni kubwa kuliko bei waliyokuwa wanataka kutuuzia,

sasa fidia tunalipa na Rostam kaingia ubia na Wamarekani ili kuwaziba wanasiasa midomo, kwenye Symbion hii ilobadilishwa jina toka Dowans hatumsikii Slaa,mbowe,sitta wala Mwakyembe wakati mitambo ni ileile iloitwa chakavu, wamefyata kisa Marekani ina hisa so wakipinga itakula kwao.

Sasa Rostam anakula Fidia,anakodisha Mitambo kama kawa na kelele zimestop kwa nini wahindi wasitudharau?
Mbona unamtaja Rostum peke yake? Kikwete je?
 
Hatmaye serikali imeanza kuilipa DOWANS baada ya kesi iliyokuwa mahakamani kuamuliwa DOWANS ilipwe.

Sasa ndo naanza kufahamu sababu za wao kuja na senema ya kina Lwakatare na Ludovick.
Ili ndilo lengo lao, tujikite kwenye sakata hilo wakati wao wanajichotea mahela ya Watanzania kwa kisingizio cha kuilipa Dowans, kampuni hewa!
HEBU SIKILIZA HII NGOMA YA NSELA WA KIMAKONDE JINSI ALIVYOWACHANA MAFISADI.
 

Attachments

wATWAMBIE TU KUWA DOWANS WAB
NAMUUZIA TANESCO UMEME WA KIASI GANI NA KWA SH NGAPI, WANSLIPA PANGO SH NGAPI, JE WAPO KWENYE ULE MRADI WA GESI YA MTWARA, HIYO PESA YATOKA WAPI? NA ACCOUNT IMEFUNGULIWA LINI YA MALIPO, JE MKATABA NAO MSISHO LINI.
 
katika bajeti ya mwaka huu,kila idara katika kila taasisi ya serikali imekatwa asilimia 5 ya bajeti yake kuchangia ..trust me

Ndiyo maana watumishi wengi katika baadhi ya tasisi za serikali walikuwa wakilalamika kucheleweshewa mishahara yao bila sababu zisizoeleweka kwa miezi ya karibuni!
 
kasharunga

Mbunge Sitta kwanza ni mwan Sheria na Mwakyembe naye kasomea Sheria. pili mkataba wowote unakuwa na kifungu cha kuweza kuvunja mkataba kwa sababu ya upande moja kutokuwa wakweli au kwa kuvunja vipengele vya mkataba, sasa hili jambo kwenda mrama sio Sitta au Mwakyembe wenye kuliweza, na hata kampuni iliyokuwa inaitetea Tanesco nayo imeshindwa, ujue hapo kuna kitu kilicho zaidi ya sheria, wenyewe wamependa hizo hela ziende huko, kwani hatukuweka kinga za kuzuia hili jambo lisitoke kama lilivyo tokea. ni sawa sawa na mkataba wa trl na wale rites na kuna mingine mingi tu. ni suala la kuwa hakuna utashi wa kisiasa wa kuzuia wizi
 
Last edited by a moderator:
Kwa sasa watanzania wengi wametunisha macho na misuli yote katika sakata la Lwakatare. Pembeni mafisadi wanagawana kinyemela raslimali za taifa kwa mgongo wa Dowans! CCM ndio wanataka iwe hivyo!!! Rais alikwishatamka kuwa wala hata mmiliki wa Dowans hamfahamu?? Na sasa ameamua kumlipa!!! Kwa watu wenye mang'amuzi mazito, hivi ni nani angestahili kujadiliwa, kushinikizwa na hata kushitakiwa kwa uhaini kwa sasa? Ni Lwakatare au ni Kikwete??????!!!!!!!!!!!!!!!!! Watanzania bado tuna safari ndefu!!
 
Hivi yule Mzee Ndesamburo wa Moshi Chadema alipokuwa analizungumzia suala hili bungeni alikuwa anajua uzito wake? alisema anawafahamu hawa Dowans ni vijana wahuni wanaokaa pale kwenye hotel yake ya Keys, swali wahuni wanaweza ku file kesi katika mahakama ya kimataifa ya biashara? Huyu mzee Ndesamburo aliangalia nje ya kikombe na sio ndani ya kikombe, wako wakubwa ktk nchi hii kwenye scandal hili.
 
Kama kuna mtu alifikiri kuwa dowans hawatalipwa then alikuwa hajafuatilia sakata zima. Uhusiano wa RA, EL na JK uko wazi. RA alichofanya ni kujiondoa katika mstari wa mbele wa kundelea kuonekana machoni mwa watu kila mara. Amerudi nyuma, kama ni vitani tungesema amerudi kuwa think tank, yaani kule mipango yote inakopangwa. Tulipigwa changa la macho eti kajiuzuru ubunge sasa basi!
Kama mtu mmoja alivyochangia humu, fedha za uchaguzi 2015 zimeshapatikana!
 
Kwa sasa watanzania wengi wametunisha macho na misuli yote katika sakata la Lwakatare. Pembeni mafisadi wanagawana kinyemela raslimali za taifa kwa mgongo wa Dowans! CCM ndio wanataka iwe hivyo!!! Rais alikwishatamka kuwa wala hata mmiliki wa Dowans hamfahamu?? Na sasa ameamua kumlipa!!! Kwa watu wenye mang'amuzi mazito, hivi ni nani angestahili kujadiliwa, kushinikizwa na hata kushitakiwa kwa uhaini kwa sasa? Ni Lwakatare au ni Kikwete??????!!!!!!!!!!!!!!!!! Watanzania bado tuna safari ndefu!!

lwakatare, Wapi kwenye Sheria na Kanuni za manunuzi zinasema Rais lazima amjue mnunuzi? Hata kama Rais anamjua au hamjui haibadilishi kitu kwenye hukumu zilizotoka kwenye mahakama zote mbili, hii ni Dunia ya Kutumia akili mkileta ushabiki na hoja za kipropaganda lazima Taifa liingie hasara, Tunailipa fidia kwa sababu ya kulazimisha kuvunja mkataba, Wale walosema wapo sahihi kisheria mbona wamefyata?
 
Kwanini waliosini mikataba hii tusiwapige mawe mpk kufa,washasini mafeki mengi jamani na imetosha sasa......tutawajali mpk iweje!les react against their selfishness;Tuk Fhem!
 
Hakuna malipo yoyote yasiyoidhinishwa na bunge. Kama wameanza kulipwa nani kaidhinisha malipo hayo?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
kumbe hata mwizi ni haki yake kuiba sio?
Unajua nini maana ya wizi? Au una kurupuka tu? Munaingia mikataba halali kisha munaivunja kwa manufaa ya kisiasa munategemea nini hapo? Mbaya zaidi munashauriwa mununue kwa gharama nafuu 46bn munaleta siasa kwenye jambo linalo hitaji taaluma "mitambo mibovu" sasa mtu anadaichake utamwita mwizi?
Wacha sheria ikate kama inavyo julikana
 
Unajua CCM bado wana ndoto za kuendelea kuongoza Tz hata after 2015!
No wonder wanasaka ela za kuhonga khanga kofia tshirt na simu za kichina plus vocha inchi nzima
 
Politics of this country, one minute you think Membe is JK's hand picked successor the next minute you see everything working in Lowassa's favor! Basically paying Dowans is paying Lowassa and his accomplice.... Rostam. With so much money Lowassa will dictate public opinion through media propaganda, churches etc! The sky will be his only limit
 
Tatizo la Tanzania Siasa inaongoza nchi badala ya nchi kuongoza siasa. Chuki na fitina pamoja na akili mgando ni janga kwa Taifa hili.

Tumecheka na nyani tunaambulia mabua.Mh Zito pamoja na wadau wengine walishauri serikali inunue mtambo huo ilikunusuru nchi isiingie gizani pamoja ya kwamba sheria za manunuzi haziruhusu. Kamati ya Mwakyembe na Sitta alipinga vikali na kudanganya Umma kwamba haufai.

Katika mapendekezo yao walishauri serikali ivunje mkataba na mtambo huo uondolewe nchini AS SOON AS possible.

Kama kweli watendaji hao waliona hivyo kwa nini waliruhusu mtambo huo ubaki nchini?Inachoonekana siasa chafu za kupakana matope na unafiki ndo vinavyotutia umaskini wa kupindukia. Nchi inashindwa kutoa mikopo kwa wanavyuo au kulipa karo kwa walobahatika kupata wakati fedha zinachotwa kiunyanganyi. Haya mambo ya kudadia fani za watu hasa sheria tunaangamiza nchi.

Pamoja na hayo kwanini President asiingilie kati au autaifishe au hao Dowans/Symbion/Richmond tuwaombe watuonee huruma watusamee deni hilo. Kama ni hivyo unafuu wa kupata umeme ni hadithi ndo maana Mramba/Tanesco alisema ukweli kuwa hata Tanesco isilipe mishahara na huduma za uendeshaji zisitishwe Shirika haliwezi kusimama lenyewe lazma bill kwa mteja ziongezeke. Viongozi wetu hawataki kusema ukweli ingawaje ukweli unauma.

Mwache Rostam ale nchi twayataka wenyewe, hili deni linauma sana. Katika Program za RURAL ELECTIFICATION -UMEME VIJIJINI symbion anapendelewa sana wakandarasi wengi wananyimwa fursa hii.

Hapo penye red ndo ilikuwa kipengee kimojawapo kwenye mkataba, kuhakikisha kwamba wakiwekeza kwenye huo mtambo wa Dowans wapewe hizo projects za vijijini
 
Back
Top Bottom