Dowans lazima walipwe

Halipwi mtu hapa nanyi mnaojidai mmesoma sijui mmepitia bla bla acheni kutudanganya hapa asiyejua kusoma nani? Dowans ilipwe ilipwe my %$&&&$$****^%%^%halipwi mtu na tuone kama watatufanya kitu hawataki wahame nchi wasituletee ujinga na upumbavu wao hapa. Na ninyi mnaojitia tumepitia tumesoma kwa makini rudini shule mkasome kwa makini mjijenge kimaisha kwa kutoa maamuzi ya busara kwa manufaa yenu na familia zenu sio kuja hapa tumesoma tumesoma asiyesoma nani tuondoleeni majinamizi yenu yes i said majinamizi.
 
Pamoja na mengi aliyofanya huko nyuma ameendelea kuwa mbunge. Atalipwa na kuendelea na nyadhifa zake. Itachukua muda kwa sisi Watz kujitambua!

Haaaaaaaaa! Kumbe kelele zote hizi lakini bado tunamchangia kodi zetu kumlipa mshahara na posho Rosta kama mbunge!!??????-'Eee watanzania tusio na akili baba yetu tutukuze! Utupe leo fahamu zetu na utu......
 
Dah!!! DOWANS imewafanya watanzania wasahau kama kuna adha ya mgao wa umeme. This country is just ****ed up
 
tanzania ya kweli tutaipata kwa kumwaga damu hakuna lingine.....maisha ni uhai wako....sasa angalia uhai wako unavyokuwa wa kugandamizwa heri kufa kwa kutetea haki yako kuliko kufa kwa aibu ya kunyanyasa nchi kwenu na watanzania wenzako.
 
kulipwa walipwe, lakini wasitukandamize wananchi kwenye huduma za kijamii kutupandishia gharama.
waliyataka wao.
 
Son of soil,

Nakuomba kwanza hii tabia ya kutuandikia kwa maandishi makubwa inakuwa ngumu kufatilia unachokisema yet alone kukufahamu nini unachoongea.

Pili usitulazimishe tukubaliane na mtazamo wako wakati hoja yako ni dhaifu kama ifuatavyo:-
a. Kwanza wahusika wakuu wa mkataba ni REDVCO au Richmond na Tanesco. Hivyo Richmond alitakiwa apate consent ya Tanesco na sio waziri. Hilo ni kosa kubwa na mimi ningeliletewa hiyo kesi wangelipumulia mashine kama sio kutokwa na majasho.

Tatu. Unadai waziri wake amewapa go ahead na tanesco wakakubali umeme kumbuka Tanesco kabla ya hapo walikataa kukubali huo mkataba wa Richmond. Akina Karamagi na wenzie wakawalazimisha waukubali. Pia baadae ilipokuja Dowans pia walilazimisha ndio Tanesco wakakubali. Lakini jiulize je Richmond ilihamisha mkataba wake na Tanesco lini? (Ilikuwa kabla hawajawaandikia Tanesco kuhamishia ownership Dowans). Hivyo basi bwana mkubwa hilo ni kosa kuu huwezi kufanya mambo kienyeji kwa jina lengine misrepresentation of facts ambazo ni conditions of the contract na hapo ndio unakuta Richmond wamevunja mkataba wao in the first place.

Sasa kama wao wametuletea umeme tukatumia imekula kwao kwani mkataba ambao ni void mwanzoni kila kitu kinachoendelea pale ni void na hivyo basi Tanesco hawana wajibu wa kuwalipa mpaka watueleze kwanini walihamisha mkataba kwa Dowans.

Nashukuru kwa ushauri wa kutumia maandishi madogo,ni kweli hata mimi nikiwa natumia simu napataga shida kusoma na kupata idesas,ila niliomua kufanya hivyo kuonyesha msimamo na msisitizo,

Umezungumza ukweli na vizuri sana ila naomba uelewe na uelewe vizuri hapa kani ni muhimu TAREHE 23 DECEMBER 2006 tanesco na Dowans waliingia mkataba halali

Pamoja na madudu yote ya huko nyuma mkataba huu ulihalalishwa tarehe tajwa hapo juu ,kwa hiyo ni makosa kusema Tanesco walikuwa hawana mkataba halali na Dowans;

Tujikumbushe baadhi ya vipengele vya Ripoti ya Mwakyembe hapa


"" Kamati teule haikufanikiwa kupata majibu ya Citibank ila iliambiwa kulikuwa na shinikizo toka Wizarani “kuwa viongozi wa Wizara kama kawaida yao waliishinikiza TANESCO kukubaliana na ombi la Richmond Development Company LLC la kuhamisha mkataba.” Ni kutokana na hilo tarehe 21 Disemba, 2006 TANESCO ikaiandikia kampuni ya Richmond kukubali uhaulishaji wa mkataba huo kwenda kwa Dowans kwa barua yenye SEC. 388/12/206 ambapo pamoja na mambo mengine ilitaka “ipate hati ya uthibitisho kutoka Dowans Holdings, S.A ya kuridhia uwajibikaji kamilifu katika kutekeleza Mkataba wa tarehe 23 Juni, 2006, kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC.”

Hivyo tarehe 23 Disemba 2006 Mkataba ukaingiwa kati ya TANESCO na Dowans S.A ambao ulikuwa ni kuhamishia mkataba kati ya TANESCO na Richmond kwenda kwa Dowans Holdings S.A. )


 
Unazidi kuonyesha ulivyolelewa kifisadi na ulivyokosa adabu kwa wasomaji wa JF kwa kuendelea kuwapasua masikio kwa maandishi ya jazba na yasiyokuwa na mshiko. Loo ! unafisadi hadi nafasi ndani ya JF ! Pole sana lakini hoja yako ya kuwatetea wezi na matapeli na kudai lazima walipwe kamwe haingeweza kutolewa na mtu anayejiita mzalendo, leave alone mwenye akili timamu.



Tazama unavyojichanganya, unaposema sisi tukae chini tupange namna ya kuwa..blah blah, je una maana gani ? Hao sisi ni akina nani na wao ni akina nani ? Hivi hujui kuwa wawajibishaji ndio hao hao wezi wetu na ndio hao hao Dowans na wameamua kujilipa kwa mlango wa nyuma. Unadai wewe ni mzalendo lakini mzalendo wa nchi gani ? Nina hakika sio Tanzania - wacha kujitafuna mwenyewe kama punguani,waaacha !

Una matatizo ya akili ndugu yangu nenda ukachek kwa wataalamu watakusaidia,kama unashindwa hata kuelewa LENGO na UZALENDO wangu kwa nchi yangu ya Tanzania basi una matatizo

Hii ni kwa faida yetu wote tusijipe moyo DOWANS watalipwa,ila sisi wananchi,wazalendo,tukishirikiana na viongozi wetu waadilifu tuwakamate wale wote walioihujumu nchi yetu kwenye hili

Malipo ya Dowans NI LAZIMA ila ADHABU kwa wale waliotufikisha hapa ni maamuzi yetu,tukiamua kukaa kimya na kuendelea kuandika na kubishana hapa JF hayaaa,tukiamua kufungua kesi kuwashika ,kuwafilisi na kuwafukuza nchini haya,tukiamua kuwachagua tena kama wananchi wa IGUNGA na MONDULI hayaaaa,kazi kwetu
 
Halipwi mtu hapa nanyi mnaojidai mmesoma sijui mmepitia bla bla acheni kutudanganya hapa asiyejua kusoma nani? Dowans ilipwe ilipwe my %$&&&$$****^%%^%halipwi mtu na tuone kama watatufanya kitu hawataki wahame nchi wasituletee ujinga na upumbavu wao hapa. Na ninyi mnaojitia tumepitia tumesoma kwa makini rudini shule mkasome kwa makini mjijenge kimaisha kwa kutoa maamuzi ya busara kwa manufaa yenu na familia zenu sio kuja hapa tumesoma tumesoma asiyesoma nani tuondoleeni majinamizi yenu yes i said majinamizi.

Mawazo ya kijinga yanatokana na fikra za kijinga kwa mtu wa kijinga

Unapayuka na kutukana ilhali wewe binafsi hujitambui wala hujijui,ungelijua maswala haya wala usingelizungumza utumbo huo,ungekaa chini usome magazeti usikilize radio,usome katiba,sheria za PPA ,mkataba wa Tanesco na Richmond na ule wa Tanesco na Dowans kisha usome Sheria za ICC na hukumu ya ICC halafu usome kesi iliyofunguliwa na kima Mvungi High Court kupinga kusajiliwa kwa tuzo ya ICC,ukishamaliza kusoma hayo yote ndio ungekuja hapa ukiwa mtu mzima mwenye akili timamu na unayejua jambo unalotaka kuchangia lakini hii kukaa saloon na umeshakunywa Heinken mbili ndio unatumia simu yako uliyohongwa na Fisadi kuandika kwa kuchefua watu makini na wanazuoni wenye uwezo mpana ,sio sawa na sio sahihi

Kaa chini chukua ushauri wangu wakati mwingine utaandika jambo la maana ,asubuhi njema
 
basi walipani tu yaishe; fedha zipo, viongozi wapo na uamuzi ndio huo. Hamhitaji kibali kwa watanzania.
 
Jamani hii sinema ya dowans inaishaa lini? Vipaumbele taifa hili hatunaa au ni taifa la matukio tuuu?
 
son of soil, Dowans= Duwanzi,watanzania wa leo sio waduwanzi namna hiyo.:angry:
 
son of soil, dowans= duwanzi,watanzania wa leo sio waduwanzi namna hiyo.:angry:

jipe moyo ila hawa mafisadi watalipwa hamna ubishi,tutakuwa hapa hapa tukifundishana ,na hata maamuzi ya high court tutayajadili humu humu na tutayaafiki tuu dowans watalipwa jukumu letu ni kuamua kuwachukulia hatua mafisadi au la hatuna mkono wa kuzuia malipo ya dowans hatuwezi
 
ni watanzania wachache sana ambao mpaka sasa hawaijui serikali yao
Kwa serikali hii ya JK na marafiki zake ,hawa jamaa hawana huruma na nchi hata kidogo wako tayari kutafuna rasilimali zetu mpaka ziishe na ni kweli kabisa DOWANS watalipwa lakini sio kwamba wanalipwa hao wakosta rika ni kina JK,RA,EL NK na wengine

La muhimu ni sisi wtanzania kupinga malipo haya mpaka mwisho hata kama watalipwa lakini ujumbe uwafikie Jumuia za kimataifa na kote duniani HATUKO TAYARI KAWALIPA DOWANS,
 
Wasiwasi wangu ni kwamba hata wale watu nilio kuwa nawaamini wamegeuka kabisa.Jamani what is this for Gods' sake.Money,money,money,money,zilimuua Yesu,sasa zinaua wengi.Generali Ulimwengu shame on you!
 
Wasiwasi wangu ni kwamba hata wale watu nilio kuwa nawaamini wamegeuka kabisa.Jamani what is this for Gods' sake.Money,money,money,money,zilimuua Yesu,sasa zinaua wengi.Generali Ulimwengu shame on you!

Mkuu, bado hata mimi najiuliza, jee huyu mtu mwenye ID GEN ULIMWENGU anayemtolea thanks za nguvu huyu sos , ni yule Jenerali tunayemfahamu?

Nadhani sie, ni mpuuzi mmoja amekuja na huyu sos kupeana support na si vinginevyo.
Hata jina lenyewe, tunayemfahamu huwa anajitambulisha kama JENERALI na wala sio GENERAL
 
mkuu, bado hata mimi najiuliza, jee huyu mtu mwenye id gen ulimwengu anayemtolea thanks za nguvu huyu sos , ni yule jenerali tunayemfahamu?

Nadhani sie, ni mpuuzi mmoja amekuja na huyu sos kupeana support na si vinginevyo.
Hata jina lenyewe, tunayemfahamu huwa anajitambulisha kama jenerali na wala sio general

mbona mnaangalia minors na kuacha major inapotea,mtoto wa udongo anasema lazima dowans walipwe na wasipolipwa nchi itapata shida sasa tuache porojo tujenge point ni kwa nini wasilipwe

mimi sijasimamia upande wowote ila hukumu ya icc inakomalia sana kipengele cha tanesco kupokea na kuuza umeme wa dowans kwa miezii kadhaa bila kulalamika na baadae wanavunja mkataba,hii inaweza kuwa point

tunaweza kupinga sana halafu mwisho wa siku wote tukakimbia humu jf na kukaa kimya kwa aibu,
tujaribu kuchambua mambo kwa upana wake tuone kama huyu sos ana la kutuambia au la;
 
Na kama hana jipya basi tumuache aende zake sio kutukanana na kuangalia mambo yasiyo ya msingi,huyu mtu anaweza kuwa ametumwa lakini kaja pazuri tuwape majibu wakamueleze aliewatuma
 
i hate you we si mzalendo na c mtanzania bora ungetoa sababu nyingine na si hii
baada ya kuupitia vizuri mkataba wa tanesco na richmond wa june 2006,na baadae nikaupitia mkataba wa dowans na tanesco wa december 2006,pamoja na madudu yote ambayo richmond waliyafanya dhidi ya tanesco bado kulikuwa na concert ya waziri na serikali hata kama tunasema richmond walihamisha mkataba kwenda dowans bila kuwaeleza tanesco si kweli kwani waziri karamagi alikubaliana na richmond.

jambo la pili na muhimu ni kwamba nimepitia hukumu ya icc kwa mapana yaek na kipengle kimoja ambacho waamuzi wa icc wanakishikia bango ni kuwa dowans waliperfom na tanesco walipokea umeme wa dowans

hili ni la muhimu na watanzania wanatakiwa kujua hata kama mkataba wa tanesco na dowans ulikuwa sio halali bado unawishwa kuwa halali kwa sababu ya tanesco kupokea umeme wa dowans kama tanesco wasinglipokea umeme wa dowans basi mkataba ungekuwa batili ,lakini as long as the dowans perfomed and tanesco received those whether one or hundred megawats ,maana yake ni kuwa kulikuwa na mkataba halali na tanesco kuuvunja ilikuwa ni batili

cha kufanya

kwa ushauri wangu,serikali iwalipe dowans hizo billion lakini sasa irudi kwa kina karamagi na wengine wote waliohusika kuirubuni tanesco wakamatwe,wafilisiwe na wawekwe ndani huu uwe mfano.

angalizo

kama tanesco na serikali yetu ikikataa kuwalipa dowans,balozi zetu nje ya nchi zitakuwa atached na mwisho wa siku tutawalipa kwa riba kubwa sana,


watanzania,

msiogope kuwalipa dowans bilion 94,hao dowans wameshalipwa zaidi ya bilioni 172 mpaka sasa kwa ajili ya mitambo waliyoinunua kwa shilingi bilioni 60,nchi hii ina hela nyingi sana kazi yetu tunatakiwa kuwadhibiti wale wanaotumia fedha zetu vibaya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom