Dowans lazima walipwe


Kwanza unatakiwa ujifunze adabu na kwa kuanzia ujifunze internet etiquette, you are shouting na sisi si viziwi. Pili ujifunze heshima na ujue kuwa nchi kamwe haiwezi kuyumbishwa na wezi na matapeli. Tatu ujifunze uzalendo kwa nchi yako na taifa lako na uache kabisa kupotosha mambo kwa kuleta utetezi wa kijinga. Lazima ujue kuwa nguvu ya Umma ni paramount - shuhudia inavyofanya kazi hivi sasa dhidi ya ving'ang'anizi kama Mubarak wa Egypt. Wakumbuke Mao Tse Tung wa China, Nicolae Ceausescu wa Romania, Mohamad Reza Pehlavi wa Iran, Ferdinand Marcos wa Phillipines na karibuni Bel Bela wa Tunisia, walivyong'oka kwa nguvu za Umma !

Son of soil unatamka bila aibu kuwa liwapo na liwe Dowans lazima walipwe, hivi hapa unaongea kama nani na hii jeuri na dharau kwa Watanzania unaitoa wapi ? Je wewe ndiye Kikwete mwenyewe ama mbia wake ? Sasa ngoja na mimi nikutamkie wazi kuwa Dowans ikilipwa basi wewe, Kikwete na hilo genge lenu la wezi muanze kutafuta hifadhi nje ya Tanzania yetu. Nina hakika kuwa tukikataa kuburuzwa na hawa wezi, nchi nyingi zitatuunga mkono kwa msimamo wetu na tutajijengea heshima kubwa tofauti na unavyodai. Mahakama gani itabariki vitendo vya kitapeli na wizi na kuvihalalisha kwa sababu ya kuwa huduma ilipatikana, huu ni ujuha wa sheria.

Dowans ni Kikwete first and foremost ndipo wanafuatia hao wabia wake kina Rostam, Lowassa, Karamagi and the rest of the gang of thieves. Mtakuja wengi humu na mtatetea hadi mtokwe povu lakini mkae mkijua kuwa mmeisha kilukoroga na sasa mkae tayari kulinywa pamoja na machungu yake. Kikwete atazunguka dunia nzima, atasuluhisha hadi waChechnya lakini mwisho wa safari ajue tunamsubiri atupe maelezo kwa nini mchana anafuja hela zetu kwa kuwalipa matapeli halafu usiku anatembeza bakuli kama Matonya akiomba msaada. Imefikia mahali mtu unasita kutaja taifa lako, no enough is enough Kikwete must go - ni ama yeye au sisi wazalendo !
 



Son of soil unatamka bila aibu kuwa liwapo na liwe Dowans lazima walipwe, hivi hapa unaongea kama nani na hii jeuri na dharau kwa Watanzania unaitoa wapi ? J

mkuu ...huyu jamaa nilishagundua sio mtanzania
 


NI UKICHAA,WENDAWAZIMU NA UJINGA MKUBWA KUZUNGUMZA KAMA KICHAA
HAIWEZEKANI WEWE UWE NA AKILI TIMAMU ETI UNANIAMBIA MIMI NISHIKE ADABU NA UNANIFUNDISHA UZALENDO?MIMI NAUJUA UZALENDO NA DHAMANI YA NCHI HII KABLA HATA HUJAZALIWA SO SHUT UP AND LISTEN

NARUDIA TENA WATANZANIA MTAKE MSITAKE,MPENDE MSIPENDE.HATA KAMA WATANZANIA WATAKULA MAJANI NA UDONGO,DOWANS LAZIMA WALIPWE

NA HII SIO SIASA HII NI KWA FAIDA YA TANZANIA HUU NI MSIMAMO WA KIZUONI MIMI SIO MJINGA NA NINAYAANGALIA HAYA MASWALA KWA MAPANA ZAIDI SIO KUSIKILIZA KELEL ZA WANANCHI WASIOJUA HATA KATIBA YAO NA KULETA HAPA

NARUDIA TENA SHERIA ZA MIKATABA YA KIMATAIFA ZIKO WAZI NA ZINAELEWEKA U CAN GOOGLE AND SEE ANY OF THEM,DOWANS WALIPEWA MKATABA NA RICHMOND KINYUME CHA SHERIA NAKUBALI KABISA MADUDU MAKUBWA YALIFANYIKA LAKINI

NA HILI WEWE NA WENYE MTAZAMO WAKO WAELEWE LAKINI

TANESCO WALIPOKEA UMEME WA KAMPUNI BATILI,NA WAKAUFURAHIA,NA WAKAUUZA KWETU MIMI NA WEWE ,NA TANESCO WAKAPATA HELA KUTOKANA NA UMEME WA DOWANS(PERFOMACE) SASA KITENDO HIKI KISHERIA KINAMAANISHA MKATABA WA TANESCO NA DOWANS ULIKUWA HALALI NA HALALI KABISA .


HALAFU REX ATTORNEY MAFISADI WAKUU WA SHERIA WAKAWASHAURI WAVUNJE MKATABA NA DOWANS ILHALI DOWANS WAMESHAZALISHA UMEME NA TUMEULA

KWA HILI TANESCO WALIKUBALI BIASHARA YAKE NA DOWANS BILA UBISHI WALA BILA KULAZIMISHWA NA BAADAE WAKAAMUA KUVUNJA NDOA YAO MAKUSUDI ILIO TUWALIPE KINA ROSTAM AZIZ NA KINA KARAMAGI

SASA LEO HUWEZI SEMA HATULIPI MSIWAPE MOYO WATAANZANIA WAAMBIENI UKWELI KUWA DOWANS LAZIMA WALIPWE ILA SISI TUKAE SASA NA KUPANGA MIPANGO YA KUWAFILISI NA KUWAFUKUZA NCHINI WALE WALIOIDANGANYA TANESCO WALE WALIOIBA NA KUHUJUMU NCHI YETU

DOWANS WATALIPWA NA SISI SOTE TUTASHUHUDIA TUTAKUWA HAPA HAPA NA SIO SIKU NYINGI.

watalipwa na ni haki yao hilo ni funzo tumepewa.
 
Hatutawalipa na tuone mwisho wetu.

Mbona CUBA hadi leo bado wanaishi?

Tusiwalipe na mwisho wa siku, tuvunje MUUNGANO na wao wabaki wakiidai TANZANIA ambayo haitakuwepo.

Kama wao wanaujua huu, sisi tunaujuwa huu.

Duun hiyo kiboko but tamu sana
 

Son of soil,

Nakuomba kwanza hii tabia ya kutuandikia kwa maandishi makubwa inakuwa ngumu kufatilia unachokisema yet alone kukufahamu nini unachoongea.

Pili usitulazimishe tukubaliane na mtazamo wako wakati hoja yako ni dhaifu kama ifuatavyo:-
a. Kwanza wahusika wakuu wa mkataba ni REDVCO au Richmond na Tanesco. Hivyo Richmond alitakiwa apate consent ya Tanesco na sio waziri. Hilo ni kosa kubwa na mimi ningeliletewa hiyo kesi wangelipumulia mashine kama sio kutokwa na majasho.

Tatu. Unadai waziri wake amewapa go ahead na tanesco wakakubali umeme kumbuka Tanesco kabla ya hapo walikataa kukubali huo mkataba wa Richmond. Akina Karamagi na wenzie wakawalazimisha waukubali. Pia baadae ilipokuja Dowans pia walilazimisha ndio Tanesco wakakubali. Lakini jiulize je Richmond ilihamisha mkataba wake na Tanesco lini? (Ilikuwa kabla hawajawaandikia Tanesco kuhamishia ownership Dowans). Hivyo basi bwana mkubwa hilo ni kosa kuu huwezi kufanya mambo kienyeji kwa jina lengine misrepresentation of facts ambazo ni conditions of the contract na hapo ndio unakuta Richmond wamevunja mkataba wao in the first place.

Sasa kama wao wametuletea umeme tukatumia imekula kwao kwani mkataba ambao ni void mwanzoni kila kitu kinachoendelea pale ni void na hivyo basi Tanesco hawana wajibu wa kuwalipa mpaka watueleze kwanini walihamisha mkataba kwa Dowans.
 

Unazidi kuonyesha ulivyolelewa kifisadi na ulivyokosa adabu kwa wasomaji wa JF kwa kuendelea kuwapasua masikio kwa maandishi ya jazba na yasiyokuwa na mshiko. Loo ! unafisadi hadi nafasi ndani ya JF ! Pole sana lakini hoja yako ya kuwatetea wezi na matapeli na kudai lazima walipwe kamwe haingeweza kutolewa na mtu anayejiita mzalendo, leave alone mwenye akili timamu.


Tazama unavyojichanganya, unaposema sisi tukae chini tupange namna ya kuwa..blah blah, je una maana gani ? Hao sisi ni akina nani na wao ni akina nani ? Hivi hujui kuwa wawajibishaji ndio hao hao wezi wetu na ndio hao hao Dowans na wameamua kujilipa kwa mlango wa nyuma. Unadai wewe ni mzalendo lakini mzalendo wa nchi gani ? Nina hakika sio Tanzania - wacha kujitafuna mwenyewe kama punguani,waaacha !
 

You are Great thinker, Well said.
Hao akina PUMBA hapo juu wamepigwa JITI na RA wanasema ovyo.
 
tunaanzia hapa dowans kuwadhibiti hawa mabwege mafisadi. Kwa sababu wamewahi kulipwa mahela mengi zai di bilioni 172, kama wanataka wachukue mali zilizoko ubalozi ethiopia.

Very well said. Huwezi kusema walipwe alafu watu watawajibishwa baadaye. Hivi Tanzania tukoje hatu-learn kabisa jamani. Whether analysis ya mtoa hoja ni valid or not. kwani kuna-mtanzania gani ameshafaidi hayo mabalozi mnayoyasema. Ukiangalia hata ile kesi ya ufisadi wa ubalozi wa Italy, imeishia wapi? si afadhali zingetaifishwa tu. Angalia ubalozi wa DC ulivyonunuliwa kwa pesa nyingi eti kitega uchumi who is benefiting I wonder? Eti Tanzania tuna hela kama tunahela kwanini hospitali hazina dawa wala vitanda? Kwanini shule hazina madawati etc. Nawasi wasi na huyu aliyeandika hii mada. Hatuwezi kuanza na kuwalipa tunang'ang'ana mpaka kieleweke. Sheria ikitubana sana tunaanza na watu kuwajibika kwanza ndio tulipe. Accountability first tunaanza na Kikwete mwenyewe.
 

Hapo penye nyekundu pamenifurahisha saana. Can not say more chukua tano. Thank you very Much huu ndio ukweli halisi!!!
 
hakuna kulipaaaaaaaaaaaa, stop, la sivyo ya EGYPT soon yatatokea, trust me, hii ni kampuni hewa, halafu ww mtoa mada, weare are u from?
how can u legalize a fake & corrupt company, not existing to be paid? who gave you mandate to favor Dowans payment? ICC is a fisadi's associate, na it can't override our High court, period, wakilipa ya Egypt, Tunisia, Yemen, Russia utayaona, look at different perspective
huu ni moto, CCM itakufa wakilipa.
 

Mbwa ww, umetumwa, huku umekosea njia, F**K u
 
wanatafuta pa KUTOKEA SASA...................kwi kwi kwi.......damn mmebanwa kila angle...........katafute sababu zingine.........huwezi ku-rule out.........kwenda kinyume na mkataba in the first place........PERIOD!
 
Mkuu kumbuka kuwa hao wanaotakiwa kuwajibika bado ni wadau ktk Dowans na nadhani wana percent fulani ya mgao. Iwapo watalipwa na kutakiwa kuwajibishwa watatumia udhaifu wa sheria zetu na kuachiwa na mwisho wa siku tunarudi palepale ground 0.
 
Kuandika kwa herufi kubwa ni kupayuka."Unampayukia nani"
Ni kama vile wewe ndiye Dowans sasa unataka kufa na mtu??

Acha zako wewe>tapika hiyo Amplifire ongea kwa herufi ndogo.

 
Mwanzoni ulisema hivi:


Halafu kwa vile hoja yako ilikuwa inasimama au kuanguka katika maneno hayo mawili ukarudi (baada ya kufikiria sana bila ya shaka) na kusema:


NARUDIA TENA SHERIA ZA MIKATABA YA KIMATAIFA ZIKO WAZI NA ZINAELEWEKA U CAN GOOGLE AND SEE ANY OF THEM,DOWANS WALIPEWA MKATABA NA RICHMOND KINYUME CHA SHERIA NAKUBALI KABISA MADUDU MAKUBWA YALIFANYIKA LAKINI


Vyote kutoka mtu mmoja na kuhusu jambo lile lile.
 
Nahisi Son of Soil ni msemaji wa Rostam Hapa JF.

Wakati nasoma Hoja yake Son of Soil nilipata hisia mimate yake inanirukia usoni, huku juso lake bapa na nene kwa kula chipsi mayai likinkodorea huku imishipa na mige shingoni mwake ikiwa imemtoka kwa hasira. Mimacho yake nayo ilikuwa balbu kaa amplifire imemkwama kooni.Huku kidole chake kikinipa onyo la backoff.
 
Du Mtanzania wewe ni kweli unatokea Manzese Midizini au ni Rosta mwenyewe, kisha unatanguliza matusi, unalazimisha hata wasiotumia umeme zaidi ya 80% walipe mwisho unamtaja Karamagi ashtakiwewengine huwataji una lako.
Nakukumbusha awamu ya 3 ya utawala wa CCM mweka hazina wao alichota hela BOT na hadi leo DOWANS, hiyo mitambo tulinunua watanzania kwa mkopo wa CRDB na ilipofika Ubungo haikuwasha umeme kwenye grid ya Taifa kwa miezi 3 wakiendelea kulipa 159bn mpaka hapo hujui lisemwalo inaonyesha una-copy na paste

15: Kwamba wakati Richmond ilisajili jina la RDEVCO LLC Machi 2008 hii ilikuwa ni baada ya matukio mawili, kwanza baada ya kuwa imekwisha kuingia mkataba na Tanesco Juni 23, 2006 kwa bosi wa Tanesco kutishwa ili asaini, lakini pia baada ya Dowans kuwa amekwisha kuchukua mkataba huo; Lakini pia jina hilo halikusajiliwa kwenye mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura uliofikiwa Juni 23, 2006.
16: Kwamba Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) ilithibitisha pasi na shaka yoyote kwamba mchakato wa ufungaji wa mkataba wa Richmond na Tanesco ulikiuka sheria ya manunuzi ya umma;
TAFADHALI USILAZIMISHE HOJA ZAKO DOWANS HAWALIPWI MPAKA MJITAJE, NA HATUTAWAPA ILA NCHI NZIMA SASA TUTAANDAMANA BILA KUFUATA DINI, ITIKADI YA CHAMA
 
Du Mtanzania mwenzangu umeme bill tumelipa na hatudaiwai na mtu yoyote, Dowans walichotushtaki ni ku-uvunja Mkataba wao walitaka waendelee mpaka leo kutukamua wazalishe wasizalishe walipwe
Hata km wewe mtu anang'ang'ania kulala kwako ukimgundua ni mchawi na kumtoa atakudai fidia?
Acha tuandamane mpaka mtakapomtaja Dowans ni nani analia huko Misri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…