BIN BOR
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 1,013
- 407
Tatizo la fidia sio kwa Dowans peke yake. Ni pesa kiasi gani ililipwa kama compensation kwa South Africa kwa kuvunja mkataba wa ATCL, au Rites wa India nao si wako katika mstari? Ni pesa kiasi gani ilipotea kwa kuvunja mkataba wa TTCL? Na kuna madudu mengi tu, ambayo hatuyajui au tunayajua kama ya mikataba ya madini, vitalu vya uwindaji na hili la kutengeneza noti mpya zenye kasoro kibao. Kwa sasa siasa inatupeleka kupiga mayowe Dowans! Dowans! Lakini ukweli ni kwamba nchi inaangamia kwa madudu mazito kuliko Dowans.
Bado naendelea kutafakari, lakini tunapopiga kelele za Dowans wenzetu wanazidi kutufilisi kupitia madudu mengine mengi tu.
- Rais apunguziwe madaraka ili katika mambo haya asiwe yeye refa, kipa na mshika kibendera, kama katiba mpya itachelewa hili lifanyike kama kiraka maana tushavizoea
- Mikataba yote sasa ijadiliwe kwa uwazi bungeni, maana kuna faida za usiri lakini tukiwaachia usiri tunaibiwa
- Itumike sheria ya uhujumu uchumi kuwafikisha kortini na kuwafilisi waliotufilisi
- Ile habari ya kinga ya rais kutoshtakiwa haina tija kwa Tz ya leo
Bado naendelea kutafakari, lakini tunapopiga kelele za Dowans wenzetu wanazidi kutufilisi kupitia madudu mengine mengi tu.