Dowans! Dowans! Wakati nchi inaangamia.......

BIN BOR

JF-Expert Member
Nov 23, 2010
1,013
407
Tatizo la fidia sio kwa Dowans peke yake. Ni pesa kiasi gani ililipwa kama compensation kwa South Africa kwa kuvunja mkataba wa ATCL, au Rites wa India nao si wako katika mstari? Ni pesa kiasi gani ilipotea kwa kuvunja mkataba wa TTCL? Na kuna madudu mengi tu, ambayo hatuyajui au tunayajua kama ya mikataba ya madini, vitalu vya uwindaji na hili la kutengeneza noti mpya zenye kasoro kibao. Kwa sasa siasa inatupeleka kupiga mayowe Dowans! Dowans! Lakini ukweli ni kwamba nchi inaangamia kwa madudu mazito kuliko Dowans.
  • Rais apunguziwe madaraka ili katika mambo haya asiwe yeye refa, kipa na mshika kibendera, kama katiba mpya itachelewa hili lifanyike kama kiraka maana tushavizoea
  • Mikataba yote sasa ijadiliwe kwa uwazi bungeni, maana kuna faida za usiri lakini tukiwaachia usiri tunaibiwa
  • Itumike sheria ya uhujumu uchumi kuwafikisha kortini na kuwafilisi waliotufilisi
  • Ile habari ya kinga ya rais kutoshtakiwa haina tija kwa Tz ya leo

Bado naendelea kutafakari, lakini tunapopiga kelele za Dowans wenzetu wanazidi kutufilisi kupitia madudu mengine mengi tu.
 
  • Rais apunguziwe madaraka ili katika mambo haya asiwe yeye refa, kipa na mshika kibendera, kama katiba mpya itachelewa hili lifanyike kama kiraka maana tushavizoea
  • Mikataba yote sasa ijadiliwe kwa uwazi bungeni, maana kuna faida za usiri lakini tukiwaachia usiri tunaibiwa
  • Itumike sheria ya uhujumu uchumi kuwafikisha kortini na kuwafilisi waliotufilisi
  • Ile habari ya kinga ya rais kutoshtakiwa haina tija kwa Tz ya leo
Bado naendelea kutafakari, lakini tunapopiga kelele za Dowans wenzetu wanazidi kutufilisi kupitia madudu mengine mengi tu.
Mkuu nakubaliana na wewe kabisa hicho kiraka tunakihitaji kwanza, na haraka sana sababu sasa tuko uchi, na hatuwezi kuendelea hivyo wakati tunangoja nguo mpya
 
Tatizo la fidia sio kwa Dowans peke yake. Ni pesa kiasi gani ililipwa kama compensation kwa South Africa kwa kuvunja mkataba wa ATCL, au Rites wa India nao si wako katika mstari? Ni pesa kiasi gani ilipotea kwa kuvunja mkataba wa TTCL? Na kuna madudu mengi tu, ambayo hatuyajui au tunayajua kama ya mikataba ya madini, vitalu vya uwindaji na hili la kutengeneza noti mpya zenye kasoro kibao. Kwa sasa siasa inatupeleka kupiga mayowe Dowans! Dowans! Lakini ukweli ni kwamba nchi inaangamia kwa madudu mazito kuliko Dowans.
  • Rais apunguziwe madaraka ili katika mambo haya asiwe yeye refa, kipa na mshika kibendera, kama katiba mpya itachelewa hili lifanyike kama kiraka maana tushavizoea

  • Mikataba yote sasa ijadiliwe kwa uwazi bungeni, maana kuna faida za usiri lakini tukiwaachia usiri tunaibiwa

  • Itumike sheria ya uhujumu uchumi kuwafikisha kortini na kuwafilisi waliotufilisi

  • Ile habari ya kinga ya rais kutoshtakiwa haina tija kwa Tz ya leo

Bado naendelea kutafakari, lakini tunapopiga kelele za Dowans wenzetu wanazidi kutufilisi kupitia madudu mengine mengi tu.

MKuu nakubaliana na wewe na ni kweli kuwa Dowans ni dalili tu na mizizi ya matatizo ni uwezo mkubwa wa rais kikatiba. Ni muhimu sana apunguziwe maamuzi mazito. Katiba hii ilitungwa ikiwa na ideal president in mind kama Nyerere, lakini hawakuona mbele kuwa si kila kiongozi ana moyo na utashi kama wa Nyerere. Maana kuna mengi mzee wetu alikosea lakini hatuwezi kukataa kuwa alikuwa na utashi wa kuona makosa yake na ya kuyarekebisha na hata kuji-limit kwa kujiuzulu (anglieni Mubarak anavyong'ang'ania madaraka huko Misri)

Kwa hiyo marekebisho haya ni muhimu!
 
Mkuu, kwa hilo nakubaliana na wewe. Hila nataka niongeze kwamba apatikane mbunge aliulize swali hilo bungeni, akitaka kujua siyo tu fidia iliyolipwa, bali pia gharama nyinginezo zilizoambana na malipo hayo. Aidha takwimu hizo zihusishe pia fidia ambayo imekuwa ikilipwa kwa kampuni za ujenzi wa barabara kutokana na kuvunja mikataba bila ya kufuata utaratibu.
 
Tatizo la fidia sio kwa Dowans peke yake. Ni pesa kiasi gani ililipwa kama compensation kwa South Africa kwa kuvunja mkataba wa ATCL, au Rites wa India nao si wako katika mstari? Ni pesa kiasi gani ilipotea kwa kuvunja mkataba wa TTCL? Na kuna madudu mengi tu, ambayo hatuyajui au tunayajua kama ya mikataba ya madini, vitalu vya uwindaji na hili la kutengeneza noti mpya zenye kasoro kibao. Kwa sasa siasa inatupeleka kupiga mayowe Dowans! Dowans! Lakini ukweli ni kwamba nchi inaangamia kwa madudu mazito kuliko Dowans.
  • Rais apunguziwe madaraka ili katika mambo haya asiwe yeye refa, kipa na mshika kibendera, kama katiba mpya itachelewa hili lifanyike kama kiraka maana tushavizoea
  • Mikataba yote sasa ijadiliwe kwa uwazi bungeni, maana kuna faida za usiri lakini tukiwaachia usiri tunaibiwa
  • Itumike sheria ya uhujumu uchumi kuwafikisha kortini na kuwafilisi waliotufilisi
  • Ile habari ya kinga ya rais kutoshtakiwa haina tija kwa Tz ya leo

Bado naendelea kutafakari, lakini tunapopiga kelele za Dowans wenzetu wanazidi kutufilisi kupitia madudu mengine mengi tu.

Mkubwa chanzo cha matatizo yetu mengi ni hicho!!! Kwa kupitia uchochoro huo Mkwere anatupiga mabao ya kisigino huku akijua hatuwezi kumfanya chochote!!
 
Dowans in kama blanketi iliyomfunika mgonjwa mwenye maradhi mengi. Tukimfunua tutayatibu na hayo mengine tutakayoyaona.
 
Back
Top Bottom