Kuhani nimesema hitimisho langu ni lile la kamati ya Bunge kwamba TANESCO wawezeshwe kununua mitambo. Sijasema TANESCO wanunue au wasinunue mitambo ya DOWANS. Hii sio kazi ya kamati. Mitambo gani wananunua na kutoka wapi ni kazi ya TANESCO wenyewe. Hili nimeliweka wazi kabisa katika michango yangu humu (unspinned, niliyoandika mwenyewe) ndani na pia katika barua ambayo nimeandika kwa Waziri wa Nishati na Madini. Kuhani, nipo very clear na judgement za watu humu nazichukua kama changamoto. As i said, humu JF sishindani, ninajifunza.
Msimamo wangu ni msimamo wa kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
This Day Feb 19, 2008
Dr Mwakyembe said Rostam was sent a summons to appear before the probe team, but dodged it by claiming he was outside the country when the committee was sitting in Dar es Salaam.
Rostam was apparently summoned for questioning on his links with the US-based Richmond Development Company LLC and UAE-based Dowans Holdings SA, after more than five witnesses had named him during earlier testimony.
Said Mwakyembe: He (Rostam) was also required by our committee to explain why the postal and e-mail addresses of his own company, Caspian Construction Company Ltd, were being used by Dowans Holdings SA. The committee was also given several names of employees of Caspian who also work for Dowans Holdings SA.
KANUNI na sio sheria.
Sasa hizo statement zako hapo mbili kwenye same reply, sijui niiamini ipi??
Yaani wewe kwenye issue ya dola $90million kulipwa dowans na kujaribu kwenda kwa manufacturer ambaye anaweza kutupa hiyo mitambo kwa about $50million tena mipya na warranty, una question safari ya wabunge wawili Ama??? Kwani safari za mwaka zinazolipiwa na serikali yetu si zaidi ya watu maelfu tena kwenye mambo yasiyo na maana kwenda kujitambulisha blah blah, sasa kwenye hili la maana unaanza kuquestion?? Aisee Mh. Yapi tena yaliyokusibu mbona unakuwa erratic kwenye hili suala??
Baada ya kuwashuku wabunge wenzako kuwa wanaspin sheria ili kujenga hoja zao, nawewe umefanya nini hapo chini (in red)? Hio "pale inapowezekana" hukuiongeza ili kutetea hoja zako za kuwabeba Dowans?...Kanuni inasema SHALL be Brand New, wewe unasema "pale inapowezekana". Yale yale.
Na again, wananchi wanamfuatisha mwalimu wako Prof. Shivji kwamba, DOUBT EVERYTHING!... We are just doing that.
Mh. Zitto,
Ni kweli ni kanuni na sio sheria. Nilisema kwenye post yangu uliyonukuu kwamba, kanuni ni sehemu ya hiyo sheria husika kwa kuwa zimetungwa kwa mujibu wa sheria mama, ndo maana zinatumika zote kwa pamoja katika taratibu za manunuzi. Utakubaliana nami kuwa kwenye taratibu za "tender" na matangazo hizo kanuni na sheria hutumika sambamba. Ndio maana kwenye matangazo huandikwa maneno haya hapa chini nanukuu;
"A consultant will be selected in accordance with the procedures set out in the Public Procurement Act No. 21 of 2004 and the Public Procurement (Goods, Works,Non-consultant services and disposal of public assets by tender) Regulations, 2005 Government Notice No. 97 of 15th April, 2005"
Kwa hiyo sheria na kanuni zinaenda pamoja na hazitenganishwi. Ukienda kinyume na kanuni ambayo imetungwa kwa mujibu wa sheria mama, unahesabika mkosaji. Katika kushughurikia mambo mbalimbali ya serikali, lugha hii hutumika sana kwamba je, " Sheria, Kanuni na Taratibu" zimefuatwa?
Mh. Zitto, tuendelee na mjadala.
Mbunge Kijana, mtaalamu anamaanisha kuwa 'kanuni' hiyo ni sehemu ya 'sheria' ndio maana kanuni za aina hiyo zinatungwa - na kusomwa - chini ya sheria husika. Mkuu usijaribu kutumia fursa hii kushusha hadhi kazi ya Kamati Teule ya Bunge ya Kuchunguza Utoaji wa Zabuni kwa Richmond (na pacha wake Dowans) na kusafisha wasifu wa aliyekuwa Waziri Mkubwa na aliyetajwa kuwa Swahiba wake. Kaka weka nguvu zako kwenye kuibana Serikali Bungeni ili itekeleze maazimio (maagizo?) ya Kamati/Bunge hasa lile azimio la kutatua hili tatizo la umeme wa dharura! Mheshimiwa usipoziba ufa wa Richmond utajenga ukuta wa Dowans!
nimespin
Sasa hizo statement zako hapo mbili kwenye same reply, sijui niiamini ipi??
Yaani wewe kwenye issue ya dola $90million kulipwa dowans na kujaribu kwenda kwa manufacturer ambaye anaweza kutupa hiyo mitambo kwa about $50million tena mipya na warranty, una question safari ya wabunge wawili Ama??? Kwani safari za mwaka zinazolipiwa na serikali yetu si zaidi ya watu maelfu tena kwenye mambo yasiyo na maana kwenda kujitambulisha blah blah, sasa kwenye hili la maana unaanza kuquestion?? Aisee Mh. Yapi tena yaliyokusibu mbona unakuwa erratic kwenye hili suala??
nakubaliana nawe. ndio mjadala unakuwa mzuri. kwa hiyo kanuni za manunuzi zinakataza mitambo iliyotumika.
katika barua yangu kwa Waziri nimesema tanesco wanunue mitambo ya umeme kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.
bodi ya shirika la umma inataka kununua mitambo, inaamua kutuma wabunge. unaona ni sawa kabisa........ nakushangaa. Rashidi aliwakatalia. Wamekasirika kukosa katrip.
Sheria ya manunuzi ya mwaka 2004 husomwa pamoja na kanuni zake, hii ina maana GN. No. 97 (THE PUBLIC PROCUREMENT (GOODS, WORKS,NON-CONSULTANT SERVICES AND DISPOSAL OF PUBLIC ASSETS BY TENDER) REGULATIONS, 2005; ni sehemu ya sheria hiyo kwa kuwa zimetengenezwa chini ya sheria husika na kutangazwa katika gazeti la serikali.
Kwenye kanuni hiyo hapo juu sehemu ya IV kifungu cha 58 (1)-(6), nina vinukuu hapa chini:
...........
(5) The preferred motor vehicles or other motorised equipment as determined under sub-regulation (4) of this Regulation, shall be procured either directly from the manufacturer of the said motor vehicles or through competitive quotations from reputable authorised local and international
suppliers or dealers of the specified vehicles.
......................Neno "Shall' linapotumika kwenye sheria, linaweka msisitizo kuwa ni lazima, na sio vinginevyo.
..
Mh. Zitto hizo petty fights zenu kwenye kamati, mimi hazinihusu. Lakini kwenye possibility ya kusave over $50 million siwezi kuanza kuquestion investigation itakayocost at most $15,000.
Ni hayo tu Mheshimiwa sababu kila siku serikali inasafirisha watu kwenda nje hata kwenye kuhudhuria seminar tu au mambo mengine ambayo hayana hata benefits kwetu.
nakubaliana nawe. ndio mjadala unakuwa mzuri. kwa hiyo kanuni za manunuzi zinakataza mitambo iliyotumika.
katika barua yangu kwa Waziri nimesema tanesco wanunue mitambo ya umeme kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.
Tuko pamoja kabisa, na kama serikali itafuata sheria, kanuni na taratibu zake ambayo ni yenyewe imeziweka, basi, mitambo ya Dowans haitanunuliwa, labda kama kuna "loopholes" kwenye sheria yenyewe au kanuni zenyewe.
This is what is supposed to be. Vinginevyo, kama tuko kwenye hali mbaya sana, then, tutafanya kile wanachofanya Marekani, kuokoa uchumi wa nchi yao. Sasa justification hiyo ipo kwa sasa?
Huo ni mtizamo wangu tu.
Tuendelee kujadili na kuelimishana.
Article 97 ya Katiba ya JMT, kifungu cha (5), Kinalipa bunge uhuru wa kumpa mtu(waziri in this case) au idara ya serikali mamlaka ya kutengeneza kanuni "having the force of law".
Kwahio suala la kuitwa sheria au kanuni halina mashiko kwenye utekelezaji wake, as zote zinaenda sambamba kama mkuu Ngereja alivyoonyesha hapo juu.
Mheshimiwa kateleza,... kama hajateleza basi anayumbishwa na kimbunga cha Dowans...
Aisee Companero na Ngereja, Ahsanteni mno maana sisi wengine watu wa Idara walituambia na kutuhakikishia kuwa PPRA 2004 hairuhusu hayo mambo ya Dowans, na ndio maana tulitaka Mh.Zitto atuonyeshe wapi PPRA inasema inaruhusu. Lakini nyie mmetupa kitu na box kabisa kwa hiyo kumbe wasiwasi wetu unalindwa na sheria za Jamhuri, kwa hiyo kidogo nitalala salama maana najua kutakuwa na price ya kupay kama mitambo ya Dowans ikinunuliwa.
All in all, at least imetusaidiia kujua lazima tutafute watu wengine bungeni kukamilisha agenda za wananchi maana Mh. Zitto naona kidogo hajui zile no no za politics, Yaani mfano Republicans right or wrong lazima wasupport Tax cuts, ukitaka kuleta mambo ya sijui nina msimamo unajiuzulu tu na kwenda huko msimamo wako unakowakilishwa.