Asante sana, uko sahihi. Ndiyo maana nilisema kwamba maombi pekee hayatoshi; sikumaanisha kwamba maombi hayana umuhimu. Hakuna taifa, jamii (au hata mtu binafsi) iliyowahi kupiga hatua kwa kutegemea maombi pekee.
Mungu ametupa uwezo wa kufikiri na kutatua changamoto. Kwa mambo yaliyo ndani ya uwezo wetu, hatupaswi kumwachia Mungu pekee kufanya badala yetu, kwa kuwa kufanya hivyo kunaashiria uzembe na kukwepa wajibu.
Maisha ni muunganiko wa vipengele vya kiroho, kimwili na kiakili. Changamoto za kiroho hupambana na nguvu za kiroho; za kimwili hushughulikiwa kimwili; na zilizo katika uwezo wetu wa kiakili lazima tukabiliane nazo kwa kutumia maarifa na busara tulizopewa. Big up to TEC, na wengine wenye kusimamia haki na utu bia kuangalia mtu usoni.