Hapana!
Kwanza, nadhani ni vyema tuelewe maana ya neno
"maombi"
Maombi maana yake: Ni kutamka unachokihitaji kiwe au kitokee. Maneno haya yatamkwe mbele ya mwenye uwezo au nguvu ya kukupa hicho kitu katika eneo maalumu linaloitwa
madhabahu au kwa kiingereza
altar
Maombi huenda sambamba na sadaka au kafara au dhabihu kwa huyo mwenye nguvu ya ku - provide kile mwombaji anachotaka. Kumbuka, kufanikiwa kwako ni lazima kubebwe na "Imani" yaani uamini kuwa itakuwa kama utakavyo
Sadaka au kafara yako unaitoa mbele ya madhabahu (altar) ya huyo mwenye nguvu (yaweza kuwa mchawi/mganga au jini nk) kisha atakuambia "say your wish" yaani "tamko unachotaka kiwe". Ukimaliza hatua hii, kinachofuata na kuamini na kufanya matendo ya Imani kwa ajili ya kupata utakacho
NOTE:
1. Haiwezekani ukaruka na kuanza kutenda kabla hujabebwa na nguvu ya madhabahu ya Mungu unayemwabudu kwa kwanza kupitia hatua hizo hapo👆juu yaani: Toa kafara➖say your wish➖amini imekuwa➖tenda vitendo vya kuwezesha hicho unachochoamini kitokee na ukione kwa macho ya mwili na nyama!
2. Wachawi na waganga wana uwezo wa kuwapa watu vitu ikiwemo pesa, madaraka ya kimamlaka, utajiri, heshima na utukufu lakini huu wa kwao haudumu na huambatana na masharti magumu ya kutoa kafara kila siku, kila mwezi au kila baada ya kipindi fulani. Kumbuka pia, wachawi wanaweza kufunga watu wasivuke mstari fulani au wawe watumwa wa hali fulani daima mfano umasikini, magonjwa, huvuki kiwango fulani cha maisha nk nk
3. Ili kuishinda nguvu za madhabahu za kichawi, ni lazima upate madhabahu yenye nguvu zaidi kuzidi za majini, kichawi, kiganga na wasoma nyota na za wasihiri. Na ni lazima utoe sadaka kuu kuzidi sadaka iliyotolewa kwenye madhabahu hizi za kichawi. Na ni lazima na wewe utamke maneno (maombi) kwa kusema unataka kutokee nini badala yake kile usichokitaka. Na hiki ndicho alichomaanisha
Mshana Jr aliposema "tuzidishe maombi"
4. Habari njema ni kuwa, kwa sisi Wakristo na yeyote anayetaka kuwa upande wa Kristo, hatuhitaji kutoa kafara au dhabihu au sadaka yoyote Ili madhabahu ya Mungu wetu Yehova itusikie na kutujibu. Ni kwa sababu, Mungu mwenyewe kupitia kwa mwanae wa pekee Yesu Kristo alishajitoa sadaka kwa kufa na kumwaga damu yake msalabani,
akatukomboa na
kutugomboa maana tulikuwa tumeuzwa tukawa watumwa sababu ya dhambi ya adamu bustanini Eden. Ili kujikomboa malipo ya damu yalihitajika. Sisi tulikuwa hatuwezi kujikomboa wenyewe. Ilikuwa ni lazima tukombolewe na Mungu mwenyewe. Ndipo akaja mwenyewe kwa sura ya Yesu Kristo
Tumegombolewa kutoka ktk kila aina ya vifungo vya kishetani na kila aina ya utumwa ikiwemo magonjwa, umasikini, mauti za kichawi, kuonewa nk. Kinachohitajika kufanyika ni kila mtu kukiri na kuiamini kazi hii nzuri na takatifu ya msalaba na baada ya hapo tufanye matendo ya Imani ili tupate tunachohitaji
Kwa hiyo:
👉Sadaka/kafara/dhabihu ya ukombozi wetu ilishatolewa (kifo cha Yesu Kristo msalabani na kumwagika kwa damu yake). Ukikiri na kuiamini hii kazi, hakuna nguvu ya mchawi wala mganga wala majini yatakayokusogelea‼️
👉Kwa sababu wao humwaga damu chafu zenye hatia. Yeye (Yesu Kristo) alitukomboa kwa damu yake ya thamani kuu, takatifu isiyo na doa la dhambi yoyote. Shetani akiiona hiyo kupitia kwa mawakala wake wachawi, waganga hupigwa shoti na kamwe hawezi kukusogolea na kukudhuru!!