Nimesoma makala kadhaa kuhusu Siasa za Marekani (US), ushoga, dini, vita baridi (US vs Russia), International funding organs n.k. nimefikia makubaliano na wanaoamini Donald Trump anaweza kuwa kiongozi bora kuliko Hillary Clinton. Muda ni mfupi uliobaki kuhamasisha wamarekani wamchague Trump lakini ukweli utabaki kama atapata ama atakosa urais. Kwa machache: huyu jamaa hategemei kuchangiwa pesa ili awe rais (funding organs duniani kote zinamchukia kwavile itakuwa rahisi kwake kuwatoroka kama Magufuli), ana misimamo inayotoka moyoni akiamini wahamiaji haramu marekani na hasa wenye misimamo mikali ya kidini wanaingiza marekani katika sintofahamu....hayo hayawezi kusemwa na Obama wala Clinton. Islamic State ni tatizo kuliko rais wa Syria anayetetewa na Putin....ndiyo maana Trump anamuunga mkono Putin. Mtu mkweli mara nyingi hutoa matamshi bila kuyamumunya....sometimes yanawaudhi wengine. Walioapa kulinda maslahi yao hawapendi awe rais na hata akiwa rais hawatapenda amalize muhula wake....haya yanajionyesha kwa Magufuli, kila siku anashambuliwa. Vyombo vya habari vinamuunga mkono Clinton na hiyo inamfanya aonekane bora wakati ukweli hataweza kuwa rais bora kwa marekani na hata ustawi wa dunia. Uamuzi ni wa wamarekani,,,,....kama tulivyoamua Tanzania kumpa Magufuli nao pia wanaweza kumpa Trump japo madhara yatakuwapo.