Dokta mimi siumwi huko

Dokta mimi siumwi huko

Sasa ndugu Daudi1 si ungesubiri tu hadi saa moja jioni watu wasome wenyewe story inaendelea vipi
 
Last edited by a moderator:
Dokta Mimi Siumwi Huko - 11




ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

Kwa kutumia tundu la komeo la mlangoni, Sulee alichungulia ndani.
“Duh! Yaani kweli…?” Sulee alitamka maneno hayo baada ya kuona kwa ndani.
BURUZANA NAYO SASA…

Akarudi na kukaa tena kwenye benchi kama zamani, lakini akawa hatulii sehemu moja…
Kila mara alikuwa akiinuka kukaa, mara asogee mbele na nyuma, hakika wivu ulikuwa ukimpeleka vibaya…

“Haiwezekani, huyu Dokta Kisarawe anaweza kutuchanganya na rafiki yangu kweli? Hapana haiwezekani…,” Sulee akawa anawaza moyoni.
Baada ya muda mfupi, kilisikika kimya kutoka chumbani kwa Dokta Kisarawe. Baadaye akatoka Monica lakini uso wake ulikuwa haueleweki.

Kwa mbali alionekana mchovu kwa shughuli fulani lakini pia wakati mwingine alionesha uso wa uchangamfu na kuzidi kumchanganya zaidi Sulee.
“Vipi…,” Sulee alimuuliza Monica wakati wakiongoza njia ya kurudi nyumbani.
“Safi tu…”
“Umeonana na dokta…?”
“Sijaonana naye…,” Monica alimjibu Sulee huku akimkazia macho.
“Hujamuona…!?,” Sulee akauliza kwa sauti ya mshangao mkubwa.
“Sulee bwana, sasa wewe unajua kabisa niliingia ndani kwa dokta tena wewe ndiye uliyenipeleka, sasa unaponiuliza kama nimemuona dokta ulitaka nikujibuje? Basi sijamuona…,” Monica alijibu huku akimtazama Sulee kwa jicho la ‘Uwe unafikiri kabla ya kuuliza swali’.

Sulee akakaa kimya na kumuangalia Monica kama anayesema ‘Leo umeniweza’.
Wakaendelea na safari yao, lakini Sulee hakuwa amejiridhisha na majibu ya Monica hivyo akaendelea kumdadisi zaidi kujua kilichoendelea kati yake na Dokta Kisarawe.
“Oke, kasemaje…?”
“Amenipima na kunipa dawa hizi, lakini ameniambia nirudi baada ya siku mbili…,” Monica alimjibu Sulee na kumuonesha dawa ambazo alikuwa amepewa na Dokta Kisarawe.

Moyoni Sulee alijisikia wivu zaidi kwani hata yeye mara ya kwanza kuonana na Dokta Kisarawe alipimwa na kisha kupewa dawa na kuambiwa arudi baada ya siku mbili.
Hisia za Dokta Kisarawe kufanya kama alivyomfanyia yeye zikazidi kumgubika moyoni.

“Siku ya kurudi utaniambia ili twende wote, sawa…?”
“Sawa…,” Monica alijibu kwa mkato na sauti ya chini mno.
“Mbona kama umeishiwa na raha Monica…?”
“Hamna, mbona niko kawaida tu Sulee…”
“Au umeambiwa nini na Dokta Kisarawe…?”
“Hakuna kitu Sulee, niko sawa…”

Waliendelea na mazungumzo ya hapa na pale, lakini Monica alionesha wazi kuwa hakuwa sawa kabisa, jambo ambalo lilizidi kumuweka njia panda Sulee.
Baadaye waliagana na kila mmoja kwenda nyumbani kwake kwani tayari ilishakuwa usiku wa saa tatu kama na robo hivi…

Monica akiwa njiani, alianza kuwaza mambo mengi sana, lakini kubwa ni kwa nini Sulee aendelee kung’ang’ania kwenda naye mara ya pili wakati alishamuelekeza.
“Aah wapi, naenda peke yangu, si ameshanionesha…?” Monica akaendelea kuwaza na kufikia uamuzi wa kutokwenda na Sulee mara ya pili.

***

Baada ya siku mbili, Monica aliamua kwenda kwa Dokta Sulee peke yake bila kumtaarifu Sulee…
Baada ya kutimu saa moja na nusu karibia saa mbili, Sulee akazidi kushangaa kwa nini Monica hakumpitia kama walivyokubaliana.
“Huyu mbona hajafika hadi sasa hivi, au kaghairi…?” Sulee alizidi kuwaza baada ya kuona muda unazidi kusonga mbele bila kumuona rafiki yake Monica.
Akachukua simu na kujaribu kumpigia ili amuulize kama alikuwa ameghairi kwenda kwa dokta.

Simu ya Monica iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa licha ya Sulee kurudia tena zaidi ya mara tano. Akazidi kuchanganyikiwa.
Akampigia Dokta Kisarawe, naye akawa hapokei. Akaamua kumpigia mume wake na Monica ili kujiridhisha. Mume wake Monica alimwambia Sulee kuwa rafiki yake huyo alikuwa ameenda kwa dokta.

Sulee akatulia. Baada ya kupita saa nzima, simu ya Sulee iliita na alipoitazama, alikuwa ni mumewe Monica akimtaarifu kuwa Monica amepokea na kumueleza kuwa anajiandaa kurudi. Sulee hakujibu kitu zaidi ya kulala.

Kesho yake, aliamua kwenda kimyakimya nyumbani kwa Monica. Baada ya kuzungumza, walikubaliana kwenda pamoja siku hiyo huku Sulee akimlaumu kwa kumuacha jana yake.
“Nilichelewa nikaona nitakusumbua shoga yangu,” alijibu Monica lakini akikimbiza macho yake chini kwa aibu f’lani hivi.

Ilipotimu jioni, waliongozana pamoja hadi kwa Dokta Kisarawe, walikuta wagonjwa wengine wamepanga foleni.
Mlango ukafunguliwa na Dokta Kisarawe akatoka, alipowaona haraka akamuita Monica na kuwaacha wagonjwa wengine, akafunga mlango. Sulee kuona vile, akasogea hadi mlangoni na kuanza kuchungulia tena.

Kwa mbali akaanza kusikia tena vitu vikisogezwa. Mara kikatokea kimya cha ajabu.
Baadaye kidogo, Sulee alisikia sauti ya kulalamika ya Monica akisema
Dokta mimi siumwi huko jamaniiii, mmh!.

Usikose kufuatilia wiki ijayo.


 
Dokta Mimi Siumwi Huko - 11




ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:
Kwa kutumia tundu la komeo la mlangoni, Sulee alichungulia ndani.
"Duh! Yaani kweli…?" Sulee alitamka maneno hayo baada ya kuona kwa ndani.
BURUZANA NAYO SASA…
Akarudi na kukaa tena kwenye benchi kama zamani, lakini akawa hatulii sehemu moja…
Kila mara alikuwa akiinuka kukaa, mara asogee mbele na nyuma, hakika wivu ulikuwa ukimpeleka vibaya…
"Haiwezekani, huyu Dokta Kisarawe anaweza kutuchanganya na rafiki yangu kweli? Hapana haiwezekani…," Sulee akawa anawaza moyoni.
Baada ya muda mfupi, kilisikika kimya kutoka chumbani kwa Dokta Kisarawe. Baadaye akatoka Monica lakini uso wake ulikuwa haueleweki.
Kwa mbali alionekana mchovu kwa shughuli fulani lakini pia wakati mwingine alionesha uso wa uchangamfu na kuzidi kumchanganya zaidi Sulee.
"Vipi…," Sulee alimuuliza Monica wakati wakiongoza njia ya kurudi nyumbani.
"Safi tu…"
"Umeonana na dokta…?"
"Sijaonana naye…," Monica alimjibu Sulee huku akimkazia macho.
"Hujamuona…!?," Sulee akauliza kwa sauti ya mshangao mkubwa.
"Sulee bwana, sasa wewe unajua kabisa niliingia ndani kwa dokta tena wewe ndiye uliyenipeleka, sasa unaponiuliza kama nimemuona dokta ulitaka nikujibuje? Basi sijamuona…," Monica alijibu huku akimtazama Sulee kwa jicho la ‘Uwe unafikiri kabla ya kuuliza swali'.
Sulee akakaa kimya na kumuangalia Monica kama anayesema ‘Leo umeniweza'.
Wakaendelea na safari yao, lakini Sulee hakuwa amejiridhisha na majibu ya Monica hivyo akaendelea kumdadisi zaidi kujua kilichoendelea kati yake na Dokta Kisarawe.
"Oke, kasemaje…?"
"Amenipima na kunipa dawa hizi, lakini ameniambia nirudi baada ya siku mbili…," Monica alimjibu Sulee na kumuonesha dawa ambazo alikuwa amepewa na Dokta Kisarawe.
Moyoni Sulee alijisikia wivu zaidi kwani hata yeye mara ya kwanza kuonana na Dokta Kisarawe alipimwa na kisha kupewa dawa na kuambiwa arudi baada ya siku mbili.
Hisia za Dokta Kisarawe kufanya kama alivyomfanyia yeye zikazidi kumgubika moyoni.
"Siku ya kurudi utaniambia ili twende wote, sawa…?"
"Sawa…," Monica alijibu kwa mkato na sauti ya chini mno.
"Mbona kama umeishiwa na raha Monica…?"
"Hamna, mbona niko kawaida tu Sulee…"
"Au umeambiwa nini na Dokta Kisarawe…?"
"Hakuna kitu Sulee, niko sawa…"
Waliendelea na mazungumzo ya hapa na pale, lakini Monica alionesha wazi kuwa hakuwa sawa kabisa, jambo ambalo lilizidi kumuweka njia panda Sulee.
Baadaye waliagana na kila mmoja kwenda nyumbani kwake kwani tayari ilishakuwa usiku wa saa tatu kama na robo hivi…
Monica akiwa njiani, alianza kuwaza mambo mengi sana, lakini kubwa ni kwa nini Sulee aendelee kung'ang'ania kwenda naye mara ya pili wakati alishamuelekeza.
"Aah wapi, naenda peke yangu, si ameshanionesha…?" Monica akaendelea kuwaza na kufikia uamuzi wa kutokwenda na Sulee mara ya pili.
***
Baada ya siku mbili, Monica aliamua kwenda kwa Dokta Sulee peke yake bila kumtaarifu Sulee…
Baada ya kutimu saa moja na nusu karibia saa mbili, Sulee akazidi kushangaa kwa nini Monica hakumpitia kama walivyokubaliana.
"Huyu mbona hajafika hadi sasa hivi, au kaghairi…?" Sulee alizidi kuwaza baada ya kuona muda unazidi kusonga mbele bila kumuona rafiki yake Monica.
Akachukua simu na kujaribu kumpigia ili amuulize kama alikuwa ameghairi kwenda kwa dokta.
Simu ya Monica iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa licha ya Sulee kurudia tena zaidi ya mara tano. Akazidi kuchanganyikiwa.
Akampigia Dokta Kisarawe, naye akawa hapokei. Akaamua kumpigia mume wake na Monica ili kujiridhisha. Mume wake Monica alimwambia Sulee kuwa rafiki yake huyo alikuwa ameenda kwa dokta.
Sulee akatulia. Baada ya kupita saa nzima, simu ya Sulee iliita na alipoitazama, alikuwa ni mumewe Monica akimtaarifu kuwa Monica amepokea na kumueleza kuwa anajiandaa kurudi. Sulee hakujibu kitu zaidi ya kulala.
Kesho yake, aliamua kwenda kimyakimya nyumbani kwa Monica. Baada ya kuzungumza, walikubaliana kwenda pamoja siku hiyo huku Sulee akimlaumu kwa kumuacha jana yake.
"Nilichelewa nikaona nitakusumbua shoga yangu," alijibu Monica lakini akikimbiza macho yake chini kwa aibu f'lani hivi.
Ilipotimu jioni, waliongozana pamoja hadi kwa Dokta Kisarawe, walikuta wagonjwa wengine wamepanga foleni.
Mlango ukafunguliwa na Dokta Kisarawe akatoka, alipowaona haraka akamuita Monica na kuwaacha wagonjwa wengine, akafunga mlango. Sulee kuona vile, akasogea hadi mlangoni na kuanza kuchungulia tena.
Kwa mbali akaanza kusikia tena vitu vikisogezwa. Mara kikatokea kimya cha ajabu.
Baadaye kidogo, Sulee alisikia sauti ya kulalamika ya Monica akisema
Dokta mimi siumwi huko jamaniiii, mmh!.
Usikose kufuatilia wiki ijayo.


Ungeanzisha ya kwako ingekuwa vema zaidi unaniharibia mtirirko
 
[h=1]Dokta Mimi Siumwi Huko - 12[/h]


ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

Baadaye kidogo, Sulee alisikia sauti ya kulalamika ya Monica akisema Dokta mimi siumwi huko, mmh!
RUKARUKA NAYO SASA…

Moyo ukazidi kumwenda kasi Sulee, alijua kilichokuwa kikiendelea kati ya Monica na Dokta Kisarawe.

"Yaani kweli Kisarawe anaweza kunifanyia hivi…?.," Sulee alijikuta akisema kwa sauti na kuwafanya baadhi ya wagonjwa waliokuwa wamekaa kwenye benchi wamwangalie kwa jicho la kumshangaa kutokana na sauti yake.

"Haiwezekani, nasema haiwezekani hapa ni lazima nifanye kitu…," akazidi kuwaza huku akiwafikiria njia ya kuzuia kilichokuwa kikiendelea kati ya Monica na Dokta Kisarawe.
Kitendo cha Dokta Kisarawe kumuita Monica aliyefika mwishoni na kuwatangulia baadhi ya wagonjwa kilileta kero kwa baadhi ya wagonjwa na kuanza kumjadili kwa tabia yake hiyo.
"Mh, ina maana huyu dokta hajaona kama kuna wagonjwa wengine hapa tuliowahi…?" alihoji kwa sauti ya juu mama mmoja aliyekuwa amekaa kwenye benchi la wagonjwa.
"Shangaa, halafu kila akiingia na mwanamke ni lazima afunge mlango," alishadadia mwanamke aliyekuwa ameketi jirani kabisa na Sulee.

Mjadala juu ya tabia ya Dokta Kisarawe ulizidi kupamba moto baina ya wale wanawake waliochukizwa hasa kwa kitendo chake cha kumuita Monica licha ya kuwakuta baadhi yao wakiendelea kusubiri zamu yao ifike.
"Hapo kutakuwa na kitu, siyo bure nyie niaminini mimi," alisema mwanamke mwingine aliyeonekana kuwa na umri mkubwa kuliko wote.
"Mama yangu vile, haiwezekani watu tumewahi kufika halafu mwingine anafika na kuitwa, hapo kuna jambo, nyie fuatilieni sana," alisema dada mmoja aliyeonekana kuwa na haraka kutokana na kukosa pozi maalum, ilikuwa mara asimame, mara akae, kifupi alikosa utulivu.
Sulee alizidi kuwaza mambo mengi sana, kwanza moyoni alianza kujilaumu ni kwa nini alimuonesha Monica kwa Dokta Kisarawe. Alijua kamwe hawezi kuukwepa mtego wa dokta huyo kwani licha ya yeye mwenyewe kuwa mgumu hadi wanaume wengi mtaani kwao kushindwa kumpata, lakini kwa Dokta Kisarawe alishindwa kupindua, hivyo aliamini hata Monica hawezi kukwepa.
Fujo za Dokta Kisarawe zilizidi kumchanganya Monica kule chumbani, kwani alipokuwa akimpima mikono yake ilikosa staha hivyo akawa anayagusa maeneo hatarishi ya mwanamke huyo mrembo.
Mwanzoni alionekana kuwa mtulivu huku akimuuliza Monica maswali ya kutaka kujua kama tatizo liko kwake au kwa mumewe.

"Kweli kabisa na urembo wote huu, bado hujapata mtoto Monica…?" Dokta Kisarawe alianza kuuliza maswali yake ya mtego.
"Nimeshapata…," Monica alijibu kwa sauti kavu tena isiyokuwa na masihara hata kidogo.
"Umeshapata…?" Dokta Kisarawe aliuliza kwa mshangao aliposikia kuwa Monica alikuwa ameshapata mtoto.

"Ee, unajua dokta nakushangaa sana, sasa kama ningekuwa nimeshapata muda ningekuwa niko hapa…?"
"Mh, hapa nimepatikana, lakini atalainika tu, mimi ndiye Dokta Kisarawe bwana…," Dokta Kisarawe aliwaza moyoni baada ya kugundua kuwa Monica alikuwa mwanamke mtata kuliko alivyokuwa akifikiria.

Oke, sasa hebu kaa hapo…," Dokta Kisarawe alisema na kumuonesha Monica kiti kilichokuwa karibu yake.
Monica alikaa kwa utulivu na kumwangalia dokta kwa macho ya ‘nakusikiliza'.

"Ni wanawake wengi sana walikuja na tatizo kama la kwako, lakini kupitia mikoni hii waliondoka hapa wakiwa na furaha…," alisema Dokta Kisarawe na kumfanya Monica atabasamu japo kwa mbali.
"Kweli kabisa dokta…?" aliuliza Monica.
"Mama yangu vile…"

"Unafanyaje…?"
"Mimi siyo daktari kwa matokeo ya mtihani, bali ni mtaalam wa taaluma…," Dk. Kisarawe alijibu.
Dokta alisogeza kiti karibu kabisa na alipokuwa amekaa Monica, alianza kumshika tumboni na maeneo mengine.

Mwanzoni Monica alionekana kutulia lakini kadiri mikono ya Dokta Kisarawe ilivyokuwa ikikosa staha, ndivyo alizidi kuhisi kitu cha ajabu kikimtokea.
Dokta alimsimamisha Monica, akawa anamshika kifuani na kumwambia kuwa alikuwa anaangalia kama mishipa ilikuwa ikipeleka vyema damu.

Kwa kuwa Monica hakujua chochote kutokana na taaluma ya kidaktari kumpita kushoto, ilibidi atulie na kumuacha Dokta Kisarawe aendelee na utaratibu wake.
"Aaah, sasa Dokta mbona unanishika huko tena…," Monica aliuliza baada ya mikono ya dokta kushika yale matunda mawili yaliyokuwa yamesimama wima kifuani kwa Monica, wakati akisema hayo alikuwa akijigeuza na kusababisha kiti alichokalia kizidi kutoa mlio wa kuashiria kitu kisicho cha kawaida.
Je, nini kiliendelea hapo? Usikose wiki ijayo.


 
Dokta Mimi Siumwi Huko - 13




ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:
"Aaah, sasa dokta mbona unanishika huko tena...?" Monica aliuliza baada ya mikono ya dokta kushika yale matunda mawili yaliyokuwa yamesimama wima kifuani kwa Monica, wakati akisema hayo alikuwa akijigeuza na kusababisha kiti alichokalia kizidi kutoa mlio wa kuashiria kitu kisicho cha kawaida.
PAPARIKA NAYO SASA...

Licha ya kulalamika kwa kitendo cha Dokta Kisarawe kumgusa maeneo hatari, Monica hakuwa na upinzani mkubwa kwa mashambulizi ya daktari huyo mzoefu kwa kuwakwangua wanawake wasiokuwa na msimamo na ndoa zao, hakika Monica alikuwa amepatikana.

"Oooh, ophhhhuuu...," Monica alianza kulalamika kwa sauti ya kubana tofauti na alivyokuwa akilalama kwa sauti ya juu, sasa alianza kuhema kwa nguvu huku akigeuza macho yake makubwa na meupe.

Dokta Kisarawe akazidisha mashambulizi kwa kushika na kupapsa kila eneo alilohisi ni hatari kwa mwanamke huyo mrembo kuliko wote ambao dokta huyo aliwahi kuvunja nao amri ya sita.
"Kwa nini jamani dokta...?," Monica aliuliza huku akimtazama Dokta Kisarawe kwa macho ya ‘sasa umenibakiza nini? Si umalizie tu...'
"Aah, kwani nini tena jamani Monica...?"
"Sasa mbona unanishika huko bila lidhaa ya....nguuu....," Monica alihoji lakini hakuimalizia sentensi yake kwani tayari Dokta Kisarawe alikuwa amelishika tunda lake la upande wa kushoto na kulibinya huku akilinyonya mithili ya maembe nyonyo yale ya Tanga...

"Sasa si usubiriiiiii....," Monica akazidi kulalamika na kuongeza manjonjo ya kujikunja hali iliyomfanya Dokta Kisarawe alizidisha utundu mwilini kwa mwanamke huyo ambaye hakuwahi kuchubuliwa kwa mkwaruzo wa aina yoyote.

"Ok, sasa kama unataka mchezo si useme jamani dokta kuliko kuendelea kupeana mateso makali namna hii...," alilalamika Monica huku akizidi kuhisi hali ambayo hata kama ungekuwa wewe ni lazima uhitaji huduma tena ile ya haja.
"Kwani wewe hujui hadi niseme jamani...," alihoji dokta, lakini safari hii Monica hakujibu chochote zaidi ya kuanza kutoa sauti ya kugugumia kutokana na utamu wa sukari guru aliyokua akionjeshwa na Dokta Kisarawe.
"Aaah, hapo sasa jamani dokta, umejuaje jamaniiiii..., Monica alilalama baada ya Dokta Kisarawe kushika maeneo ya nyonga na kufanya kama anayekamua jipu kwa staili ya kubinya kwa mapozi yasiyosimulika.

Baada ya mashambulizi ya dokta kumzidishia raha ya ajabu, Monica akaona isiwe taabu kwani tayari akilini mwake alikuwa ameshahisi kuwa hakukuwa na jambo jingine ambalo Dokta Kisarawe alihitaji zaidi ya mchezo wa baba na mama.

Akaanza kujibu mashambulizi kwa kujibu mapigo ya utundu wa ajabu. Kwanza alimuangalia Dokta Kisarawe kwa macho ya karibu tena bila kupapasa, akamkazia na kusogeza kabisa kinywa chake karibu na cha Dokta Kisarawe, hapo akatoa ulimi wake mpana uliojaa mate ya uchu.
Hakuishia hapo, akausogeza kabisa karibu na midomo ya Dokta Kisarawe na bila kujali harufu ya sigara iliyokuwa ikitoka kinywani kwa mwake, Monica alitumbukiza ulimi wake mdomoni na kuanza kuuviringisha kila kona.

Utalaamu alioutumia kuchezesha ulimi wake kwa mbwembwe zaidi mdomoni, hali hiyo ilimtia wazimu Dokta Kisarawe na kuanza kugugumia kama dume la njiwa lililotoka malishoni.
Dokta Kisarawe akazidi kutoa sauti ambayo haikueleweka.

Monica naye akiwa na hali mbaya ya mhemko kutokana na kuchezewa kwa muda mrefu na mikono ya Dokta Kisarawe ambayo alikuwa akiipitisha maungoni kwake kwa ufundi na umaridadi wa kiwango cha juu.

Bila kutarajia, wailjikuta wakiwa wameegemea kitanda cha kulaza wagonjwa huku kila mmoja akiwa anahema kama aliyetoka kukimbia mbio ndefu za marathoni.
"Baby...," Monica aliita huku akiushika mkono wa kushoto wa Dokta Kisarawe na kuupitisha katika tunda lake la kulia na kuanza kumwelekeza jinsi ya kulipikicha kwa ustadi mzuri, kitendo cha dokta huyo kuanza kupita juu ya eneo jeusi lililokuwa likizunguka kikonyo cha tunda hilo.
"Basi, basiiiii, basiiiiii jamaniiii...," Monica uzalendo ulimshinda na kuanza kujinyonyoa manyoa bila ya kutakiwa kufanya hivyo, alipomaliza kujipembua, huku akilalamika kwa sauti ya kudai huduma, haraka alimvuta Dokta Kisarawe na kumlalalia kifuani mwake, akajiweka sawa tayari kwa mechi kali ya watani wa jadi.

Je, nini kitafuata? Usikose kufuatilia wiki ijayo.



 
[h=1]Dokta Mimi Siumwi Huko - 14[/h]


ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

"Basi, basiiii, basiiiii jamaniiii," Monica uzalendo ulimshinda na kuanza kujinyonyoa manyoa bila kutakiwa kufanya hivyo, alipomaliza kujipembua, huku akilalamika kwa sauti ya kudai huduma, haraka alimvuta Dokta Kisarawe kifuani mwake, akajiweka sawa tayari kwa mechi ya watani wa jadi.
HANG OVER NAYO SASA…


Kila mmoja wao alikuwa na hali ya uhitaji wa huduma.
Refaa na wasaidizi wake wakaingia uwanjani na kuruhusu mechi kuanza…
Kila upande ulianza kwa kasi kubwa na mashambulizi ya kushitukiza kwenye lango la upinzani, hali iliyowafanya washangiliaji wa pande zote kulipuka kwa mayowe kila mara.


Si Dokta Kisarawe aliyekuwa akifungua kinywa kusema chochote zaidi ya miguno na mihemko ya raha kusikika.
"Mmh! Jamani doktaaa…" Monica akajikuta akichombeza baada ya kuzidiwa na manjonjo ya Dokta Kisarawe…

"Nini tena jamani Monica, aaah, basi bwana mama…" Dokta Kisarawe naye akawa anagugumia kwa raha baada ya mikono laini ya Monica kupapasa maeneo hatari ya mwanaume huyo.

Monica alikuwa akitembeza vidole vyake kwenye bustani ya kifuani ya Dokta Kisarawe, akawa anavitanua vidole na kuvikutanisha kama mkasi ukatavyo nguo, wakati mwingine vidole hivyo vikawa vinagusa hadi vinundu viwili vya kifuani hapo hali iliyomfanya daktari huyo wa tiba za akina mama aanze kuangua kilio cha raha ya ajabu.


Monica hakuishia hapo, sasa mikono ikawa inatambaa kwa kasi katika sehemu mbalimbali za mwili wa Dokta Kisarawe.
"Jamani mama, si tumesema tuanze…"
"Nakusubiri baba…"

"Oooh, nasikia hali ya tofauti sana mama…," Dokta Kisarawe aliendelea kulalama huku mechi ikiendelea kuchezwa.
Kuna wakati Monica alimzuia Dokta Kisarawe kuendesha gari lake, na kumtaka atulie ili yeye kunyonga la kwake bila bughudha.

"Tuliaaa, tuliaaa jamaniii…," Monica alisema huku akimshikilia kwa nguvu Dokta Kisarawe.
Monica akawa anajizungusha peke yake huku macho yakiwa yamefumbwa, muda mfupi baadaye akaanza kutoa miguno mfululizo huku ulimi akiutoa nje.


Akawa anakunja mapaja na kunyoosha miguu kama kuku aliyekuwa akijinasua kutoka kwa mchinjaji.
"Aaa, aaaah, aaaahaaa…," Monica alitoa kelele hiyo na kutulia baada ya kufika mwisho wa safari yake.
Kuona hivyo, Dokta Kisarawe naye akakazana na muda si mrefu naye akatangaza kufika mwisho wa safari yake ndefu na ya kuchosha.

"Ooooh, oooffffuuu…" alihitimisha huku akijinasua maungoni mwa Monica.
Baada ya mechi hiyo, haraka sana Monica alinyanyuka na kukaa juu ya kitanda hicho cha kulaza wagonjwa na kujiinamia huku akitoa kwikwi za kilio hali iliyomshitua sana Dokta Kisarawe.
"Haa, mbona unalia tena jamani?" Dokta Kisarawe alihoji huku akimalizia kuvaa suruali.

"Kwa nini mimi jamaniiii?" Monica akazidi kutoa kilio cha malalamiko na kujifuta machozi mengi yaliyokuwa yakitiririka kwa kasi ya ajabu mashavuni mwake.
"Kha, sasa mbona unalia na kuhoji kwa nini wewe, maana yake nini sasa…," Dokta Kisarawe akawa anauliza na kumsogelea mahali pale, akamgusa begani.


Monica akauondoa mkono wa Dokta Kisarawe kwa kasi hali iliyomjulisha daktari huyo kuwa hali si shwari kwa mrembo huyo.
"Kwa nini nimemsaliti mume wangu mimi?" Monica akawa anasema kwa sauti ya juu na kumshitua Dokta Kisarawe aliyekuwa akihofia watu waliokuwa nje kusikia.

"Sasa Monica, unaposema hivyo kwa sauti ya juu kiasi hicho maana yake nini jamani, au unataka watu wafanye mambo humu ndani?"
"Kwa nini umenishawishi na kumsaliti mume wangu jamani dokta?" Monica akazidi kuhoji huku akitafuta nguo zake na kuanza kuvaa huku akijisonya.

"Sikiliza Monica, wote tumejikuta katika hali hiyo, hakuna wa kumlaumu hapa, sasa nakushangaa sana kama utaanza kunilaumu mimi wakati kama ni raha tumezipata wote…"
"Raha gani, raha gani dokta nakuuliza, au unataka nikujazie watu chumbani kwako?" alilalama Monica.
"Sasa kwa nini ufikie huko kote, halafu unaposema nilikushawishi nashindwa kuelewa, hadi naanza kukushawishi ulikuwa wapi?"

"Wewe ndiyo chanzo cha usaliti, kwani mimi nilikuambia naumwa huko, ulipoanza kushika sehemu ambazo hazihusiani na ugonjwa wangu nilikuambia kabisa kuwa dokta mi' siumwi huko, lakini hukusikia, lengo lako lilikuwa nini...?"
Je, kilifuatia nini? Usikose kufuatilia chombezo hili wiki ijayo.


 
Dokta Mimi Siumwi Huko-16




ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

"Wewe ndiyo chanzo cha usaliti, kwani mimi nilikuambia naumwa huko, ulipoanza kushika sehemu ambazo hasihusiani na ugonjwa wangu nilikuambia kabisa kuwa dokta mimi siumwi huko, lakini hukusikia, lengo lako lilikuwa nini?

LEKA DUTIGITE SASA…


"Unajua Monica hatupaswi kulaumiana sana kwa hili…?" alisema Dokta Kisarawe huku akionesha uso wa huzuni japo moyoni alikuwa akifurahia na kujipongeza kwa kitendo cha kufanikisha kula tunda la mtoto mzuri kama Monica.

"Unasemaje wewe, hivi una akili kweli…?" Monica aliendelea kung'aka chumbani humo.
Kutokana na maneno matamu na kuonesha heshima aliyokuwa akiyatoa Dokta Kisarawe, kwa kiasi fulani yalichangia kumlainisha Monica na kuanza kushuka taratibu.

"Sawa lakini siyo vizuri bwana…"

"Sawa jamani, naomba tuchukulie kama bahati mbaya mama," alisema Dokta Kisarawe.
Kitendo cha daktari huyo kutumia jina la mama wakati wa kumuita Monica, kilimfurahisha sana mrembo huyo kwani tangu aolewe hakuwahi kuitwa kwa jina hilo na mumewe.

"Poa, nimekuelewa, nimekuelewa baba…" Monica naye alijibu kwa sauti ya chini lakini alijikuta akimalizia kwa neno la baba hali iliyomshangaza na kumchanganya sana Dokta Kisarawe.

Kwa pamoja walivaa nguo zao huku kila mmoja akikumbuka utundu na utaalamu wa mwenzake.

"Ila twende mbele turudi nyuma, huyu dokta ni kiboko kwa mambo ya chumbani, sasa kama amenifanyia utundu wote huu kwenye eneo lisilokuwa na uhuru kama hili, vipi kama tukikutana ndani ya chumba tukiwa na muda wa kutosha, itakuwaje…?" Monica aliwaza huku akimalizia kuvaa nguo yake ya ndani kabla ya kumalizia kwa zingine.
"Dah! Hata Mungu aliposema nitakufanyia msaidizi, aisee alikuwa akimaanisha huyu, mama yangu vile nakuambia...,"Dokta Kisarawe alijisemea kimoyomoyo huku akifunga mkanda wa suruali yake pana kiunoni.
"Sasa kwa hiyo kuhusu tiba dokta…?" Monica alimuuliza Dokta Kisarawe huku akimuangalia kwa macho ya ‘Ila unayaweza sana.'

"Aaah, kuhusu tiba inabidi uje baada ya siku mbili lakini kwa sasa nitakupa vidonge f'lani, sawa…?" alijibu dokta huku akimuangalia Monica kwa jicho la ‘hata hii si ni sehemu ya tiba?'
Baada ya muda waliagana na Dokta Kisarawe akampa Monica vidonge f'lani vya rangi nyekundu na kumpa maelekezo ya namna ya kuvitumia.


"Basi sawa, lakini dokta nitakushukuru mno kama nitapona na hatimaye kupata mtoto, ujue nina hamu sana ya kuitwa mama jamani…," Monica alisema huku akimtolea macho Dokta Kisarawe hali iliyobadili kabisa hali ya mzunguko wa damu wa daktari huyo mwenye uchu wa warembo wazuri kama alivyokuwa Monica.

"Usijali Minie, mimi ndiyo Dokta Kisarawe bwana, si umeona mfano kwa rafiki yako Sulee, naye alikuja hapa akiwa haamini kama wewe lakini kwa sasa ni mama kijacho..."

"Mmh! Sawa kama kweli basi mimi naenda bwana…"
"Sawa, tutaonana…"
Monica alifungua mlango na kuwakuta wateja wengine wakingojea huduma ya Dokta Kisarawe.
Walimtupia Monica macho ya chuki kwani kitendo cha kuitwa yeye kwanza na kuwaacha waliokuwa wametangulia kiliwakera na kuwaudhi vibaya mno.


"Muone kwanza, watu wengine wanajirahisi kwa madaktari wakidhani ndiyo njia pekee ya kutibu magonjwa yao sugu…," yalikuwa mazungumzo ya akina mama wawili waliokuwa wamekaa kwenye benchi la kusubiri zamu huku wakimuangalia Monica kwa jicho baya.


Monica alimkuta rafiki yake Sulee amenuna bila kujua chanzo na sababu ya yeye kufanya hivyo. Moyoni akawaza huenda kilichomuudhi Sulee ni kitendo cha yeye kuchelewa chumbani kwa dokta.
Hali ilikuwa tofauti kabisa kwa upande wa Sulee, wivu wa mapenzi ya Dokta Kisarawe ulikuwa umemkaba hadi shingoni na sasa alikaribia kuzimia kwa hasira.


Kitendo cha kusikia meza na viti vikitoa sauti ya kusukumwa kila mara kilichangia kwa asilimia nyingi sana kwa Sulee kuamini kuwa ni lazima kwa vyovyote vile Monica atakuwa ametembea na Dokta Kisarawe jambo ambalo lilimuumiza kuliko ncha ya wembe kupita kwenye kidonda kibichi.

"Vipi rafiki yangu mbona unaonekana umenuna sana, pole kwa kuchelewa mwaya, "Monica alijibalaguza huku akimshika begani Sulee bila kujua hali mbaya ya wivu iliyokuwa ikimtesa mke huyo wa mtu.
"Ina maana kweli Monica unaweza kunifanyia hivyo…?" aliuliza Sulee kwa sauti ya kukwaruza.

"Nimefanya nini tena Sulee, si nimekuomba msamaha kwa kuchelewa jamani…?"
"Si umetembea na Dokta Kisarawe wewe…," alijibu Sulee kwa sauti ya juu na yenye hasira.


Je, nini kitatokea kuhusu penzi la Dokta Kisarawe na wawili hao? Usikose kufuatilia wiki ijayo.



 
Ni matumaini yangu kuwa umenielewa
 
[h=1]Dokta Mimi Siumwi Huko-17[/h]


ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:
"Si umetembea na Dokta Kisarawe wewe…" alijibu Sulee kwa sauti ya juu na yenye hasira.
JIMALIZE NAYO SASA…

"Mimi Sulee, una akili kweli au? Kwa nini unifikirie hivyo jamani?"
"Akili ninazo tena nyingi sana Monica. Sasa ile kukurukakara ya viti kutoa mlio ilikuwa nini? Ndiyo matibabu yenyewe?"

"Sasa je? Madokta we Sulee unawajua, wakimpima mwanamke mara wamshike makalio, mara watamani kumbusu, kama hukutumia akili yako unaweza kujikuta umemalizwa."
"Mh! Mi siamini Monica."
"Kwa nini huamini? Kwanza naomba nikuulize Sulee, umekuwa ukiniwekea wingu kuonana na dokta, kwani ni nani yako?"

Sulee alishtuka kwa swali hilo hasa alipokumbuka kwamba, mumewe na mume wa Monica ni marafiki na wao pia ni marafiki. Mambo yanaweza kufika mbali…
"Mi nimeuliwa tu, si nani wangu wala nini!"
"Sasa ni kwa nini umenitolea mimacho kwamba nimetembea na dokta kisa ulisikia viti vikilialia ndani?"
"Maana yangu usije ukamsaliti shemeji."

"Mmmh! Au wewe siku ulipotembea naye mliliza viti? Sema ukweli Sulee."
Ilibidi Sulee acheke ili kupoza mambo, akabalaguza kwa kuanzisha hoja nyingine kabisa nje ya hiyo.
Lakini Monica alishapata ujumbe, aliamini kuna kitu kati ya Sulee na Dokta Kisarawe…
"Amekupa dawa lakini?" aliuliza Sulee.

"Ndiyo, amesema nitumie hizo kisha niwasiliane naye.
Walifika kwanza nyumbani kwa Sulee, baadaye Monica akaenda nyumbani kwake.
Alifikia kwenye kiti akiwa amechoka sana kwa purukushani za Dokta Kisarawe…

"Lakini kama asingetumia nguvu walahi vile asingenipata, ana bahati sana, kidogo nimpigie kelele…
"Lakini lo! Dokta anayajua mambo yule, sijui ni dokta wa mapenzi au wa mwili. Kama ofisini kwake tena chapchapu ni vile. Je, tungekuwa chumbani?" Monica alijikuta akiwaza mengi sana kuhusu dokta na mazingira yote yaliyotokea. Ilikuwa mara yake ya kwanza kumsaliti mumewe na akahisi kuna tofauti kubwa kati ya mumewe na Dokta Kisarawe.

"Kwanza mume wangu hana pawa sana kama dokta. Halafu mume wangu utadhani hahemi, dokta anatoa mhemo mpaka unajua mwanaume yuko kazini," alisema moyoni Monica.
***
Dokta Kisarawe alikaa kwenye kiti akimuwaza Monica…
"Huyu mwanamke ni mzuri sana kuliko wengine. Da! Bonge la mwanamke. Sijawahi kukutana na mwanamke mzuri kama huyu, ngozi nzuri, laini, hana kipele wala manundunundu kama wengine," aliwaza moyoni daktari huyo ambaye inawezekana mpaka kwa Monica ni mwanamke wa mia mbili tangu aanze kutoa tiba.
***
Usiku wakiwa kitandani, mume wa Monica ndiye aliyeanza mazungumzo…
"Mke wangu, kwa dokta kuliendaje leo?"
Monica moyo ulimlipuka, alihisi aliulizwa swali lile kwa maana kwamba mumewe amesikia alitembea naye palepale kazini.

"Kwani vipi mume wangu?" Monica aliuliza kwa sauti ya chini.
"Ulikwenda hukwenda?"
"Nilikwenda dear."
"Si ndiyo nakuuliza kulikuwaje?"

"Ooo, alinipa dawa akasema nitumie nikimaliza nirudi kumwambia."
"Basi, tusubirie. Asubuhi unioneshe hizo dawa."
"Sawa."
***
Nyumbani kwa Sulee, mumewe alikuwa akilishikashika tumbo la Sulee akijifanya ndiyo anaulea ujauzito huo kwa mapenzi ya dhati…
"Natamani uzae hata leo mke wangu."
Sulee alicheka huku moyoni akisema…
"Ungejua mtoto si wako, wala usingejipongeza, mwenzako mwenye nguvu za kusababisha mtoto ndiyo amehusika."
***
Asubuhi, mume wa Monica akiwa ameshajiandaa kutoka kwenda kazini alikumbuka kitu, akamwita mkewe…
"Abee."
"Nipe zile dawa."
Monica alikwenda chumbani, akatoka na kipakti…
"Tena dokta alisema nikitaka kuzinywa lazima niwe nimekunywa chai ya kutosha," alisema huku akimpa dawa hizo mumewe…

"Khaa! Mbona ni dawa mpya za mafua mke wangu, vipi kwani?"
"Dawa mpya za mafua?"
"Ndiyo. We hukumbuki siku zile mama alipokuja akawa anasumbuliwa na mafua nilinunua dawa hizi?"
"Mh! kweli? Kwani zile si zipo, ngoja nikazilete."

Monica alikwenda kwenye bakuli kubwa la plastiki, akachakurachakura na kuona kipakti cha dawa hizo.
"Kweli mume wangu, si hizi hapa!"
"Si ndiyo sasa."
"Mh! Ina maana Dokta Kisarawe kaniingiza mkenge siyo?"
"Haya, kumbe dokta mwenyewe anaitwa Kisarawe! Kisarawe si walaya ya mkoa wa Pwani, tangu lini likawa jina la mtu! Makubwa haya."
Monica alifedheheka, akaanza kuhisi Sulee amemwingiza mkenge kwa kumpeleka kwa daktari feki na si yule aliyemsaidia yeye…

"Lakini kama ni feki, mbona pale nje palikuwa na wanawake wengine wengi tu tena wasiofahamiana na Sulee. Au..?" alishindwa kumalizia.
Baada ya dakika tano mumewe kuondoka, Monicha alishika simu, akampigia simu Dokta Kisarawe…
"Dokta za leo, mimi Monica…"

"Ooo, Monica mpenzi, umeamkaje? Vipi, umenimisi my dear?"
"Sikiliza Dokta Kisarawe…"

Je, unajua nini kiliendelea? Usikose wiki ijayo bwana.


 
Ni matumaini yangu kuwa umenielewa

Ni vizuri kujadili, lakini ni haki-miliki za watu hizi, hazipaswi kuchukuliwa bila kuappreciate mwenye nazo, ni sheria na haki kurefer aliyeitunga na kuitengeneza hii hadithi. Please jifunze hili ni muhimu sana.
 
Ni vizuri kujadili, lakini ni haki-miliki za watu hizi, hazipaswi kuchukuliwa bila kuappreciate mwenye nazo, ni sheria na haki kurefer aliyeitunga na kuitengeneza hii hadithi. Please jifunze hili ni muhimu sana.
Nadhani nimetaja nilikoitoa mwanzo kabisa sehemu ya kwanza ila kwakuwa dhamira yako imetimia basi
 
Back
Top Bottom