Daudi1
JF-Expert Member
- Dec 14, 2013
- 14,563
- 22,839
- Thread starter
- #81
DOKTA SIUMWI HUKO-25
ILIPOISHIA
"Mtasha mbona umekuwa mstari wa mbele sana kunizuia mimi nisafanye uhalifu, inakuwaje wewe unashindwa kujizuia?" mume wa Monica alisema akimwita mwenzake huyo kwa jina lake la utani.
Mara, mwenye gari alitokea…
SASA ONDOKA NAYO…
Alishtuka kuona gari lake limeharibika sehemu ya mlango huku timbwili likiendelea…
"Jamani vipi tena?" aliuliza kwa mshangao mkubwa.
Majibu aliyoyapata yalimfanya ajutie lakini akaahidiwa kulipwa fedha ili kwenda kutengeneza gari hilo japokuwa alikubali lakini kwa shingo upande.
Baada ya utulivu kurejea lakini huku wanaume wote wakiwa na hasira ya wivu, waliamua kwenda polisi ambapo Dokta Kisarawe aliwekwa ndani ili kupisha uchunguzi wa madai ya wanaume hao kwamba ametembea na wake zao na kuwapa ujauzito.
Baada ya kuandikisha maelezo, walirudi nyumbani. Wote walifikia nyumbani kwa Mtasha, mume wa Sulee ambapo kikao kilikaa na misimamo ilitolewa…
"Mimi bwana kwa upande wangu nasema wazi kwamba sina haja ya kuwa na mke kama huyu," alisema mume wa Monica huku akimwangalia mkewe kwa macho yaliyojaa uchungu…
"Hata mimi, Sulee nakuandikia talaka zako tatu sasa hivi," alikuja juu Mtasha na kutaka kumpiga tena mke wake kwa hasira…
"Sasa Mtasha si umeshasema unamwandikia talaka si ufanye hivyo, achana na kumpiga bwana," alisema mume wa Monica.
Wanawake hao wawili waliangua kilio huku kila mmoja akimlaumu mwenzake kwamba alimsababishia lakini lawama za Monica kwa Sulee zilikuwa za kweli kwani yeye alipelekwa na shoga yake huyo ambaye alikuwa akiijua tabia chafu ya Dokta Kisarawe…
"Bila wewe Sulee mimi yasingenikuta haya. Ulijua Dokta Kisarawe ni mwingi wa habari ni kwa nini hukuniambia maana hata wewe ulishapitiwa…
"Halafu nilimwambia dokta. Alikuwa akipenda kunishikashika sehemu zisizohusika na matatatizo yangu, nikamwambia dokta mimi siumwi huko yeye hakusikia," alilalama sana Monica…
"Monica ni shetani, hata mimi nilimwambia dokta mimi siumwi huko wakati akipeleka mikono yake kwenye matiti yangu lakini hakutaka kunisikia. Tusameheni jamani."
"Hakuna msamaha hapa… Ala!" wanaume wote walijikuta wakijibu kwa pamoja bila kutaarifiana…
"Kwanza ni muhimu kwenda kupima afya zetu maana kama mna mimba ina maana mlikuwa hamtumii kinga," alisema mume wa Monica…
"Huko kuchepuka kwenu ndiyo faida yake mnaiona sasa," alisema mume wa Sulee huku akikohoa. Hapo alikuwa akisaka karatasi ya kuandikia talaka mara moja.
***
Siku ya pili, Mtasha, yaani mume wa Sulee na mume wa Monica walikwenda kupima virusi vya Ukimwi. Walikutana na wake zao huko wakiwa na shangazi wa Sulee ambaye aliomba kuzungumza na Mtasha kabla ya kuingia kwa dokta. Kwa heshima Mtasha alikubali na akatoka pembeni…
"Baba najua unaniheshimu sana…"
"Kweli shangazi…"
"Mwenzio kanijia na talaka analia. Lakini aliponisimulia kisa hata mimi nilikuunga mkono mwanangu…"
"Nashukuru sana kusikia hivyo shangazi…"
"Enhee, lakini sasa nina ombi moja tu kwako…"
"Lipi hilo shangazi?"
"Msamehe Sulee."
Mtasha palepale alijishika kichwa na kujikuna huku akitumbua macho, akakumbuka mema aliyowahi kuyafanya shangazi huyo kwake maana ana uwezo si wa kitoto.
Kuna mwaka Mtasha alipata kesi mbaya sana, uchumi wake ukayumba sana akajikuta hana hata pesa ya kula. Shangazi huyo wa mkewe akawa ndiye mfadhili wake kwani alikuwa akimpa pesa ya kula na pia alimsimamia kwenye kesi hiyo kwa kumuwekea wakili na akashinda.
Baada ya kushinda alimpatia mtaji akaendelea na miradi yake iliyosimama…
Wakati wa maongezi hayo, shangazi mtu hakumkumbusha kitu chochote Mtasha. Alimwacha ajipime mwenyewe tu…
"Da! Shangazi kusema ukweli umenipa wakati mgumu sana," alisema mume wa Sulee…
"Kwa nini mwanangu? Kusameheana kumewekwa na Mungu na ukimsamehe mwenzako hata Mungu atapenda na kukubariki."
"Ni kweli, lakini shangazi unalionaje hili la ujauzito?"
"Hilo unaweza kuliacha mikononi mwangu nikashughulika nalo."
"Utafanyaje shangazi? Maana mimi kusema kweli siwezi kuishi na mke mwenye ujauzito wa mwanaume mwingine."
"Ndiyo maana nimesema niachie mimi kuhusu hilo."
"Shangazi maamuzi yako ni mema na nakuheshimu wewe sana, je vipi kuhusu kupima Virusi vya Ukimwi?"
Muda wote huo, mume wa Monica alipokuwa amekaa alikuwa akimtumbulia macho mume wa Sulee kama anayemwambia asithubutu kukubali hata siku moja maneno ya shangazi wa Sulee…
"Ndiyo maana tupo hapa! Wewe unadhani Sulee ana virusi?" alisema shangazi mtu huyo…
"Siwezi kusema anavyo au hana, ila kupima ni muhimu shangazi."
"Kwa hiyo kama atakuwa salama utakuwa umepokea ombi langu siyo?
ILIPOISHIA
"Mtasha mbona umekuwa mstari wa mbele sana kunizuia mimi nisafanye uhalifu, inakuwaje wewe unashindwa kujizuia?" mume wa Monica alisema akimwita mwenzake huyo kwa jina lake la utani.
Mara, mwenye gari alitokea…
SASA ONDOKA NAYO…
Alishtuka kuona gari lake limeharibika sehemu ya mlango huku timbwili likiendelea…
"Jamani vipi tena?" aliuliza kwa mshangao mkubwa.
Majibu aliyoyapata yalimfanya ajutie lakini akaahidiwa kulipwa fedha ili kwenda kutengeneza gari hilo japokuwa alikubali lakini kwa shingo upande.
Baada ya utulivu kurejea lakini huku wanaume wote wakiwa na hasira ya wivu, waliamua kwenda polisi ambapo Dokta Kisarawe aliwekwa ndani ili kupisha uchunguzi wa madai ya wanaume hao kwamba ametembea na wake zao na kuwapa ujauzito.
Baada ya kuandikisha maelezo, walirudi nyumbani. Wote walifikia nyumbani kwa Mtasha, mume wa Sulee ambapo kikao kilikaa na misimamo ilitolewa…
"Mimi bwana kwa upande wangu nasema wazi kwamba sina haja ya kuwa na mke kama huyu," alisema mume wa Monica huku akimwangalia mkewe kwa macho yaliyojaa uchungu…
"Hata mimi, Sulee nakuandikia talaka zako tatu sasa hivi," alikuja juu Mtasha na kutaka kumpiga tena mke wake kwa hasira…
"Sasa Mtasha si umeshasema unamwandikia talaka si ufanye hivyo, achana na kumpiga bwana," alisema mume wa Monica.
Wanawake hao wawili waliangua kilio huku kila mmoja akimlaumu mwenzake kwamba alimsababishia lakini lawama za Monica kwa Sulee zilikuwa za kweli kwani yeye alipelekwa na shoga yake huyo ambaye alikuwa akiijua tabia chafu ya Dokta Kisarawe…
"Bila wewe Sulee mimi yasingenikuta haya. Ulijua Dokta Kisarawe ni mwingi wa habari ni kwa nini hukuniambia maana hata wewe ulishapitiwa…
"Halafu nilimwambia dokta. Alikuwa akipenda kunishikashika sehemu zisizohusika na matatatizo yangu, nikamwambia dokta mimi siumwi huko yeye hakusikia," alilalama sana Monica…
"Monica ni shetani, hata mimi nilimwambia dokta mimi siumwi huko wakati akipeleka mikono yake kwenye matiti yangu lakini hakutaka kunisikia. Tusameheni jamani."
"Hakuna msamaha hapa… Ala!" wanaume wote walijikuta wakijibu kwa pamoja bila kutaarifiana…
"Kwanza ni muhimu kwenda kupima afya zetu maana kama mna mimba ina maana mlikuwa hamtumii kinga," alisema mume wa Monica…
"Huko kuchepuka kwenu ndiyo faida yake mnaiona sasa," alisema mume wa Sulee huku akikohoa. Hapo alikuwa akisaka karatasi ya kuandikia talaka mara moja.
***
Siku ya pili, Mtasha, yaani mume wa Sulee na mume wa Monica walikwenda kupima virusi vya Ukimwi. Walikutana na wake zao huko wakiwa na shangazi wa Sulee ambaye aliomba kuzungumza na Mtasha kabla ya kuingia kwa dokta. Kwa heshima Mtasha alikubali na akatoka pembeni…
"Baba najua unaniheshimu sana…"
"Kweli shangazi…"
"Mwenzio kanijia na talaka analia. Lakini aliponisimulia kisa hata mimi nilikuunga mkono mwanangu…"
"Nashukuru sana kusikia hivyo shangazi…"
"Enhee, lakini sasa nina ombi moja tu kwako…"
"Lipi hilo shangazi?"
"Msamehe Sulee."
Mtasha palepale alijishika kichwa na kujikuna huku akitumbua macho, akakumbuka mema aliyowahi kuyafanya shangazi huyo kwake maana ana uwezo si wa kitoto.
Kuna mwaka Mtasha alipata kesi mbaya sana, uchumi wake ukayumba sana akajikuta hana hata pesa ya kula. Shangazi huyo wa mkewe akawa ndiye mfadhili wake kwani alikuwa akimpa pesa ya kula na pia alimsimamia kwenye kesi hiyo kwa kumuwekea wakili na akashinda.
Baada ya kushinda alimpatia mtaji akaendelea na miradi yake iliyosimama…
Wakati wa maongezi hayo, shangazi mtu hakumkumbusha kitu chochote Mtasha. Alimwacha ajipime mwenyewe tu…
"Da! Shangazi kusema ukweli umenipa wakati mgumu sana," alisema mume wa Sulee…
"Kwa nini mwanangu? Kusameheana kumewekwa na Mungu na ukimsamehe mwenzako hata Mungu atapenda na kukubariki."
"Ni kweli, lakini shangazi unalionaje hili la ujauzito?"
"Hilo unaweza kuliacha mikononi mwangu nikashughulika nalo."
"Utafanyaje shangazi? Maana mimi kusema kweli siwezi kuishi na mke mwenye ujauzito wa mwanaume mwingine."
"Ndiyo maana nimesema niachie mimi kuhusu hilo."
"Shangazi maamuzi yako ni mema na nakuheshimu wewe sana, je vipi kuhusu kupima Virusi vya Ukimwi?"
Muda wote huo, mume wa Monica alipokuwa amekaa alikuwa akimtumbulia macho mume wa Sulee kama anayemwambia asithubutu kukubali hata siku moja maneno ya shangazi wa Sulee…
"Ndiyo maana tupo hapa! Wewe unadhani Sulee ana virusi?" alisema shangazi mtu huyo…
"Siwezi kusema anavyo au hana, ila kupima ni muhimu shangazi."
"Kwa hiyo kama atakuwa salama utakuwa umepokea ombi langu siyo?