Dodoma yazingirwa, BAVICHA wawindwa

Dodoma yazingirwa, BAVICHA wawindwa

Eti wanajiandaa na taharuki!?!? Ama kweli.... Haya tusubirie tuone
 
Hii nchi!! Kweli n nchi uchwara, jeshi uchwara
 
hahahahahah
bavicha wanataka kuwasaidia polisi. hahhahahahha
 
Tarehe kama ya Leo Mwaka 2015 Mh Edward Lowasa alikatwa na CCM.
# HappyMkatoDay
[emoji1] [emoji23] [emoji28][emoji3] [emoji2] [emoji38]
 
hahahahahah
bavicha wanataka kuwasaidia polisi. hahhahahahha
Na polisi wameandamana kupinga kusaidiwa hahaha. So funny. In short CCM acheni kutumikisha jeshi letu kwa manufaa ya chama ona sasa hadi wanachanganyikiwa
 
View attachment 365536

MJI wa Dodoma umezingirwa na Jeshi la Polisi. Gari la maji ya kuwasha na yaliyobeba polisi muda huu ndiyo yanayoonekana kwa wingi kwenye maeneo mbalimbali tofauti na ilivyo kawaida,anaandika Dany Tibason.

Polisi wanaonekana kuwa tayari Kwan lolote, wamejaa kwenye magari yao huku wakizunguka maeneo mbalimbali ya Mji wa Dodoma sambamba na gari la maji ya kuwasha ili kukabiliana na kile kinachojulikana kuwa ni vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA (BAVICHA).

BAVICHA wamedhamiria kuzuia mkutano huo uliolenga kukabidhiwa uenyekiti wa CCM kwa Dk. John Magufuli kutoka kwa mwenyekiti wa sasa, Dk. Jakaya Kikwete.

Awali, Jeshi la Polisi lilipiga marufuku mikutano yote ya hadhara na ya ndani ya vyama vya siasa, hali ambayo imeathiri mikutano ya CHADEMA hivyo BAVICHA kudhamiria mkutano wa CCM kutofanyika. Marufuku ya mikutano ya kisiasa ilianza kutolewa na Rais Magufuli.

Kutokana na dhamira hiyo, UVCCM walionya mkutano wao kutoingiliwa na yoyote, hata hivyo Jeshi la Polisi limeshindwa kuzuia mkutano huo huku wakibadili kauli kwamba, mikutano ya ndani haikuzuiliwa.

BAVICHA wamedhamiria kukutana Dodoma ‘kuisaidia’ polisi kuvuruga mkutano huo, hata hivyo polisi inatetea mkutano huo.

Mjini Dodoma leo, wananchi wamelazimika kusimamisha shughuli zao na kushangaa magari zaidi ya 20 yakiwemo ya kuwasha, magari ya askari wa mbwa na askari wengi wakiwa na sare zao, silaha za moto pamoja na mabomu ya machozi.

Kwa mujibu wa Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma amedai, ni mazoezi ya kawaida ambayo wameamua kuyafanya muda wa mchana badala usiku kama walivyozoea.

Mambosasa amesema, wamelazimika kufanya mazoezi kwa kutumia vifaa vya kipolisi ili wananchi waweze kutambua kuwa, Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma lipo imara zaidi.

Amesema, mazoezi hayo ni sehemu tu ya mazoezi huku akitamba kuwa, Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma lipo imara “na asiwepo mtu yoyote ambaye atajaribu kuingilia kazi za polisi.”

“Wale wote ambao watajipendekeza kwa madai ya kutaka kulisaidia Jeshi la Polisi, watakipata cha mtema kuni,” amesema na kuongeza;

“Hakika nataka kuwaeleza wananchi, asiwepo mtu wa kujaribu kwani tutawakamata na ijulikane wazi kuwa, kuingia rumande ni rahisi lakini kutoka itakuwa ngumu.”

Patrick Ole Sosopi, Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa amesema, kitendo cha Jeshi la Polisi kuzunguka mji mzima kwa kuonesha vifaa vyao vya kivita ni dalili za uoga.

“Kitika kitendo ambacho kimefanya na Jeshi la Polisi ni dalili uoga na inaonesha ni jinsi gani BAVICHA walivyo na nguvu kiasi cha kulitikisa jeshi hadi kufikia hatua ya kufanya vitisho,” amesema Sosopi.
magari ya zimamoto ni mangapi hapo sodoma
 
View attachment 365536

MJI wa Dodoma umezingirwa na Jeshi la Polisi. Gari la maji ya kuwasha na yaliyobeba polisi muda huu ndiyo yanayoonekana kwa wingi kwenye maeneo mbalimbali tofauti na ilivyo kawaida,anaandika Dany Tibason.

Polisi wanaonekana kuwa tayari kwa lolote, wamejaa kwenye magari yao huku wakizunguka maeneo mbalimbali ya Mji wa Dodoma sambamba na gari la maji ya kuwasha ili kukabiliana na kile kinachojulikana kuwa ni vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA (BAVICHA).

BAVICHA wamedhamiria kuzuia mkutano huo uliolenga kukabidhiwa uenyekiti wa CCM kwa Dk. John Magufuli kutoka kwa mwenyekiti wa sasa, Dk. Jakaya Kikwete.

Awali, Jeshi la Polisi lilipiga marufuku mikutano yote ya hadhara na ya ndani ya vyama vya siasa, hali ambayo imeathiri mikutano ya CHADEMA hivyo BAVICHA kudhamiria mkutano wa CCM kutofanyika. Marufuku ya mikutano ya kisiasa ilianza kutolewa na Rais Magufuli.

Kutokana na dhamira hiyo, UVCCM walionya mkutano wao kutoingiliwa na yoyote, hata hivyo Jeshi la Polisi limeshindwa kuzuia mkutano huo huku wakibadili kauli kwamba, mikutano ya ndani haikuzuiliwa.

BAVICHA wamedhamiria kukutana Dodoma ‘kuisaidia’ polisi kuvuruga mkutano huo, hata hivyo polisi inatetea mkutano huo.

Mjini Dodoma leo, wananchi wamelazimika kusimamisha shughuli zao na kushangaa magari zaidi ya 20 yakiwemo ya kuwasha, magari ya askari wa mbwa na askari wengi wakiwa na sare zao, silaha za moto pamoja na mabomu ya machozi.

Kwa mujibu wa Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma amedai, ni mazoezi ya kawaida ambayo wameamua kuyafanya muda wa mchana badala usiku kama walivyozoea.

Mambosasa amesema, wamelazimika kufanya mazoezi kwa kutumia vifaa vya kipolisi ili wananchi waweze kutambua kuwa, Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma lipo imara zaidi.

Amesema, mazoezi hayo ni sehemu tu ya mazoezi huku akitamba kuwa, Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma lipo imara “na asiwepo mtu yoyote ambaye atajaribu kuingilia kazi za polisi.”

“Wale wote ambao watajipendekeza kwa madai ya kutaka kulisaidia Jeshi la Polisi, watakipata cha mtema kuni,” amesema na kuongeza;

“Hakika nataka kuwaeleza wananchi, asiwepo mtu wa kujaribu kwani tutawakamata na ijulikane wazi kuwa, kuingia rumande ni rahisi lakini kutoka itakuwa ngumu.”

Patrick Ole Sosopi, Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa amesema, kitendo cha Jeshi la Polisi kuzunguka mji mzima kwa kuonesha vifaa vyao vya kivita ni dalili za uoga.

“Kitika kitendo ambacho kimefanya na Jeshi la Polisi ni dalili uoga na inaonesha ni jinsi gani BAVICHA walivyo na nguvu kiasi cha kulitikisa jeshi hadi kufikia hatua ya kufanya vitisho,” amesema Sosopi.
Watu waongo jamani full propaganda. Mimi nipo Dodoma si kweli kinachoelezwa hali shwari kabisa na sijaelewa Dodoma ipi inaongelewa
 
Kamanda wa Polisi amepanic mziki wa Bavicha umemuogopesha ameamua hadi kutoa ndani silaha yake mwisho anayoiaminia.
 
Siko Dodoma, niko zangu kwangu Shinyanga sebuleni naangalia taarifa ya habari kupitia luninga kiukweli nimecheka sana na kushangaa sana msafara wa msururu wa magari ya polisi na maelezo ya wahusika waliyoyatoa baada ya kuulizwa nini maana ya hii kitu hii na wao kujibu eti ni mazoezi ya kawaida ya jeshi la polisi kuonesha liko imara!!

Mimi hata sikuwaamini na haraka haraka nika connect na mkutano wa CCM wa trh 23/7/2016 vs Tishio la vijana wa BAVICHA - CHADEMA vs Tamko la ovyo la polisi hao hao la "marufuku ya mikutano ya kisiasa iwe ya ndani au nje na maandamano ya vyama vya kisiasa!!" kwa sababu wanazodai za eti ni za kiusalama na watu kula ugali wa ajabu ulioua watu hukohuko Dodoma!!

Kiukweli utawala huu wa awamu ya tano wa John Pombe Magufuli unahangaika na kutumia nguvu nyingi kwelikweli KUJITETEA na KUJILINDA kwa mambo ya ovyo na ya kipuuzi kabisa. Hebu soma na sikiliza kauli za RPC huyu wa Dodoma...hazina kitu....busara yote iko miguuni. Ni kauli za ovyo ktk ulimwengu huu wa kitaaluma!!

Kwa kutofikiri kwao vyema, wanaishia kutoa matamko na matendo ya hovyo yanayo - "violate" sheria, taratibu na katiba ya nchi wao wenyewe na kuishia kutumia nguvu kubwa na nyingi pasipo akili za kiweledi kujilinda na kutetea maamuzi yao wao wenyewe na kusahau kuwa UKITENDA WEMA na HAKI kwa watu, basi AMANI na UTULIVU vinakuwa ni TUNDA la hiyo HAKI!!

Ama kweli huku ni kujidanganya na kujichanganya kwingi kusiko na ulazima wowote kwa viongozi wetu wa awamu hii. Na hakika wanalo na miaka hii mitano watatumia muda na nguvu nyingi sana KUJILINDA na KUJITETEA kwa MAKOSA wanayoyatengeneza wao wenyewe kwa sbb ya woga wao badala ya kukaa chini, kubuni na kuandaa mikakati ya maendeleo ya watu waliowachagua...!!

Na huu ni uthibitisho wa wazi kuwa wako kwenye nafasi hizo za uongozi kwa njia zisizo halali!!

Kiongozi/viongozi waliochaguliwa kihalali kamwe hawana HOFU, siku zote na wakati wowote WANAJIAMINI hawahitaji kulindwa na MAJESHI na MAPOLISI kwa chochote wanachofanya na MAHALI POPOTE kwa sbb wananchi wao wenyewe waliowachagua WATAWALINDA!!

Poleni sana CCM na serikali mnayoiongoza......hakika awamu hii mnalo na mmelibeba kisawasawa!!
 
Back
Top Bottom