Jeshi la Polisi mkoani Dodoma leo limefanya mazoezi ya utayari wa kukabiliana na uvunjifu wa amani mkoani humo. Mazoezi hayo yaliongozwa na Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma,Kamanda Lazaro Mambosasa.
Polisi hao waliokuwa kwenye pikipiki,magari ya kutosha na vikosi vya miguu na mbwa walizunguka mitaa mbalimbali ya Dodoma. Kamanda Mambosasa ametoa onyo kali kwa wanaotaka kuvunja amani.
Pia,amekwepa kuyahusisha mazoezi hayo ya utayari na mkutano mkuu maalum wa CCM utakaofanyika tarehe 23 mwezi huu mkoani Dodoma. Amewataka wanaotaka kujua yahusuyo CCM wawasiliane na viongozi wa CCM kwakuwa yeye si Msemaji wa chama hicho.