dr namugari
JF-Expert Member
- Nov 19, 2022
- 9,412
- 15,995
Juzi kulitokea tukio la kushangaza kidogo. Jamaa mmoja mida ya saa kumi na moja jioni aliagiza k.vant kubwa katika moja ya grocery inayopatikana maeneo ya ilazo extension Dodoma.
Mwanamke aliyekuwa mmiliki wa grocery na duka hiyo alimjibu jamaa yule shiti sana hadi kupelekea jamaa yule kunyanyuka na kisha kumzibua makofi mazito na kupelekea mwanamke kuanguka na Kisha kuingia ndani kulia na Kisha kuchukuwa simu kumpigia mume wake kuwa nimepigwa makofi.
Basi jamaa mumewake akawasha gari akaja eneo la tukio kuja kumuona aliye mtandika mkewe makofi. Jamaa alifika na kuoneshwa mtu yule na kisha kumfata.
Jama mume: Wewe vipi mbona unampiga mke wangu makofi?
Jamaa jeshi: Kwani wee unataka nini?
Jamaa mume: Unanijua mimi ni nani?
Jamaa jeshi: Kwani wewe unajua mimi ni nani?
Jamaa mume: Nitakufanya kitu kibaya ujute kuzaliwa.
Jamaa jeshi: Fanya chochote hata sasa, huna cha kunifanya na ole wako usoge hapa nitakumwaga ubongo na chupa hii pumbafu sana! Ndio muwe mnawafundisha wake zenu adabu vinginevyo tutawaumiza sana na hakuna cha kutufanya.
Basi tukaingilia kati jamani acheni hizo siyo poa ni vyema kujua ilikuaje hadi mke kupigwa makofi. Bwana huyu hajalewa hata kidgo labda katukanwa, basi jamaa kanywea.
Jeshi kakausha zake kisha kujiondokea zake huku jamaa akibaki hana la kufanya, ikabidi ilifika muda wakafunga duka wakasepa hadi leo yule mwanamke hajaonekana pale.
Tukio la jana tena Simba na Dodoma jiji.
Muhudumu wa grocery hiyo aliyeachiwa baada ya mama yule kwenda kuuguza makofi aliyotandikwa na jeshi nae akatoa boko.
Ilikuwa Muda wa kudai pesa za mpira wa Simba, basi alivyofika kwa mmasai mmoja jina la Musa akampiga kofi la mzaha hivi na kisha kuchezesha mikono kuwa toa pesa toa pesa. Basi Masai alivyopigwa kofi na akaona amedhalilika akasimama kwa hasira kali mno kwa kupigwa kofi na mwanamke tena hadharani.
Mwanamke akijua kuwa Masai hawezi mfanya lolote, alijikuta yuko chini kwa kofi zito aliyotandikwa na Masai hadi sasa shavu la kulia limevimba vibaya.
Natoa rai
Kuwa wanawake kuweni na heshima na muache kujifanya wababe mkidhani kuwa mume au hawara atakusadia pindi ukiyakanyaga kwa wakoraa. Ona sasa dada yule amedhalilika na mume kashindwa kukupigania na huku alikuja kwa mbwembwe tukajuwa patachimbika kumbe hakuna lolote. Aibu sana , huyo mume unamuonaje hivi sasa?
Mwanamke aliyekuwa mmiliki wa grocery na duka hiyo alimjibu jamaa yule shiti sana hadi kupelekea jamaa yule kunyanyuka na kisha kumzibua makofi mazito na kupelekea mwanamke kuanguka na Kisha kuingia ndani kulia na Kisha kuchukuwa simu kumpigia mume wake kuwa nimepigwa makofi.
Basi jamaa mumewake akawasha gari akaja eneo la tukio kuja kumuona aliye mtandika mkewe makofi. Jamaa alifika na kuoneshwa mtu yule na kisha kumfata.
Jama mume: Wewe vipi mbona unampiga mke wangu makofi?
Jamaa jeshi: Kwani wee unataka nini?
Jamaa mume: Unanijua mimi ni nani?
Jamaa jeshi: Kwani wewe unajua mimi ni nani?
Jamaa mume: Nitakufanya kitu kibaya ujute kuzaliwa.
Jamaa jeshi: Fanya chochote hata sasa, huna cha kunifanya na ole wako usoge hapa nitakumwaga ubongo na chupa hii pumbafu sana! Ndio muwe mnawafundisha wake zenu adabu vinginevyo tutawaumiza sana na hakuna cha kutufanya.
Basi tukaingilia kati jamani acheni hizo siyo poa ni vyema kujua ilikuaje hadi mke kupigwa makofi. Bwana huyu hajalewa hata kidgo labda katukanwa, basi jamaa kanywea.
Jeshi kakausha zake kisha kujiondokea zake huku jamaa akibaki hana la kufanya, ikabidi ilifika muda wakafunga duka wakasepa hadi leo yule mwanamke hajaonekana pale.
Tukio la jana tena Simba na Dodoma jiji.
Muhudumu wa grocery hiyo aliyeachiwa baada ya mama yule kwenda kuuguza makofi aliyotandikwa na jeshi nae akatoa boko.
Ilikuwa Muda wa kudai pesa za mpira wa Simba, basi alivyofika kwa mmasai mmoja jina la Musa akampiga kofi la mzaha hivi na kisha kuchezesha mikono kuwa toa pesa toa pesa. Basi Masai alivyopigwa kofi na akaona amedhalilika akasimama kwa hasira kali mno kwa kupigwa kofi na mwanamke tena hadharani.
Mwanamke akijua kuwa Masai hawezi mfanya lolote, alijikuta yuko chini kwa kofi zito aliyotandikwa na Masai hadi sasa shavu la kulia limevimba vibaya.
Natoa rai
Kuwa wanawake kuweni na heshima na muache kujifanya wababe mkidhani kuwa mume au hawara atakusadia pindi ukiyakanyaga kwa wakoraa. Ona sasa dada yule amedhalilika na mume kashindwa kukupigania na huku alikuja kwa mbwembwe tukajuwa patachimbika kumbe hakuna lolote. Aibu sana , huyo mume unamuonaje hivi sasa?