VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,866
Baada ya jana PAC kuwasilisha Ripoti ya Escrow,leo ni zamu ya Serikali. Serikali imejiandaa kupangua hoja za PAC. Kujisafisha na kuepusha kuvunjika kwa Serikali. Mikutano mbalimbali ya ndani imefanyika kuamkia leo kujiandaa na mpambano wa leo. Imeafikikiwa kuwa kila mmoja ajibu mapigo yake.Akishindwa ajiuzulu mwenyewe.
Watajwa wa jana wamejipanga na kupangika. Wamewekana sawa mahali fulani fulani. Walipeana tuition usiku kucha. Hakuna hata mmoja,kutokana na vikao vya jana usiku, aliye tayari kujiuzulu kama ilivyopendekezwa na PAC.Na leo wataanza wao kabla ya Mjadala wa Wabunge wote. Kuna nyaraka wamezipata toka sehemu mbalimbali na wameapa kuzitumia kujilinda.
Leo ndiyo leo. Usicheze mbali,unga robo!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (Dodoma kwa kazi maalum)
Watajwa wa jana wamejipanga na kupangika. Wamewekana sawa mahali fulani fulani. Walipeana tuition usiku kucha. Hakuna hata mmoja,kutokana na vikao vya jana usiku, aliye tayari kujiuzulu kama ilivyopendekezwa na PAC.Na leo wataanza wao kabla ya Mjadala wa Wabunge wote. Kuna nyaraka wamezipata toka sehemu mbalimbali na wameapa kuzitumia kujilinda.
Leo ndiyo leo. Usicheze mbali,unga robo!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (Dodoma kwa kazi maalum)