Dodoma: Serikali yajipanga kupangua Ripoti

Dodoma: Serikali yajipanga kupangua Ripoti

Kinachoisumbua serikali na wanachohangaikia sasa ni namna ya kulisafisha kanisa katoliki na MKOMBOZI kwa tuhuma zilizopo. Watu na hata baadhi ya wabunge wanafikiri hekaheka hizi ni za kuwanusuru MUSOMABOYS na Pinda, Hapana hawa si muhimu na wanaweza kung'olewa tu, tatizo ni je Taswira ya Kanisa inasafishwaje mbele ya jamii kwa upuuzi uliofanywa na AG! KANISA ni muhimu kuliko CHAMA mbele ya SERIKALI!!!!
 
Tunataka hoja zijibiwe,sio kujibu mapigo kwa kukashifu,kwamba ooh Zitto alipewaga hiki,ooh katumwa na Mkono.hapana jibu hoja kwanza

Wanaleta majibu ya kitoto sana. Kwani Zitto aliyotoa ni maoni yake? Yale ni maoni ya PAC ambayo wajumbe wengi ni kutoka CCM na wame base katika ripoti na mahojiano ya wataalamu ambao ni CAG,PCCB na TRA. Pia utetezi wa serikali alioutoa Muhongo hawajazungumzia sababu za migawo ya fedha hizo kwa watendaji serikalini waliohusika na kazia hiyo.
 
hili linaonekana ni tatizo lilioota mizizi katika nchi yetu, mfano huko chadema unakaribia mwaka wa 20 sasa ila wagombea urais ni wale wale
Kweli wewe ni punga. Hata huelewi unasema nini. Chadema imeshiriki uchaguzi wa Rais mara mbili tuu na imesimamisha wagombea wawili tofauti sasa unaposema ni wale wale akina nani? Kama uwezo wako wa ku chambua mambo ni mdogo hili jukwaa halikufai nenda kwingine kunako stahili upeo wako.
 
Ajabu professor mzima anadai kwa kuwa ni deni basi hizo si pesa za serikali . Hata sijui u-professor aliupataje . Maswali magumu yeye anatoa majibu mepesi ... Jibu la kijinga kabisa ..
Liwe deni lisiwe deni bado ni fedha za serikali labda Kama tanesco ni kampuni ya mtu binafsi ..
 
Hakuna mwizi anaekosa sababu ya kujitetea,
Pia tambueni kwamba nchi hii siyo ya watu wachache wenye haki ya kujichotea pesa za uma, na matumizi mabaya ya madaraka, wakati hospitali hakuna madawa raiya walio wapigia kura wanakufa wao wana tibiwa ulaya hata mafua, mlala hoi ambae hana hata uwezo wa kupata milo miwili kwa siku ana lazimishawa na serikali achangie madawati, mabaara nK,
Ebu tuwe na uchungu na watu hawa, Taifa linaelekea wapi?
Ulisha wahi jiuliza kwanini Mungu aliweka Tanzanite, Mbuga za wanyama bora duniani, na Mlilima kilimanjaro hapa Tanzania???
Tufaham kuwa si mpango wa Mungu Mtanzania yeyote apate shida, vinginevyo hizo maliazili adimu duniani zingikuwa ulaya na si Tanzania.
Ni mimi na wewe kutafakari na kujiuliza ni wapi tumemkosea Mungu.
 
kiukweli prof. muhongo ameishia kutoa historia ya sakata la escrow na kumshambulia MKONO na kampuni yake ya UWAKILI. alipaswa kujibu hoja ya uchotwaji ya mipesa kwenye akaunti hiyo. Eti si pesa ya Umma? kweli kwani TANESCO wanalipwagwa na nani? kwa nn umeme ni ghali?
 
Back
Top Bottom