Dodoma: Rais Magufuli apokea ripoti ya uhakiki wa vyeti vya watumishi wa umma, awataka wajitumbue

Du mtaani kwetu salamu zimerudi, unasalimiwa kama unadaiwa wakati mwanzo salam ni nadra...presha ndo usiseme,viwanja vinauzwa bei ndogo,matangazo ya nauza godoro na vyombo vya ndani ndo yamezidi yaani ni ndani ya mwaka tu humu hivi miaka mitano impact zitaongezeka?
Kazi ipo mwaka huu
 
Inawezekana wakaleta hatari unazani Lakini itakuwa aibu kama majeshi yetu yatashindwa kuwadhibiti watu watakao fanya vitendo vya uhalifu!!!
Hataivo nafasi ipo warudi shule kwa maana hakuna namna tena na elimu haina mwisho!!!
 
Yaani mnavyowapa vichwa hao watu mbona mara kibao hku kitaa wanapigwa tu? sema ss akishapigwa anaenda kuita wenzie ila c kweli kwamba hawapigiki ifike sehemu tuheshimiane kila mmoja ajue nafasi ya mwenzie ktk jamii sio kutishiana tishiana tukae hatuna amani eti kisa wao kutumbuliwa bc km vp kada zote waachwe wafanye kazi na vyeti feki tusipendelee iwe fair kwa wote!
 
Si kweli. Wengi wenye vyeti feki ni watu wenye elimu ya chini kama madereva, walimu wa shule za msingi, manesi n.k... Waliofanikiwa kufika chuo kikuu na vyeti vyao feki ni wachache sana...
 
Hili swala la vyeti lisiwe la double standard. Lifanyike kwa haki bila kujali majeshi au wanasiasa
 
Hili ni jaribio kubwa sana kwa serikali na ndio maana awamu ya nne waliligusa wakaamua 'kulipotezea'.
Linanikumbusha Biblia Takatuifu pale Yesu anaposema kuwa Mungu amuepushe na kikombe kile (kama ingewezekana) lakini akakumbuka kwamba Station aliyokuwa amepewa ni ya juu mno na asingeifikia bila 'kukinywea' ..na pale akakubali kuwa "Ila ni kwa mapenzi Yako".

Sio kwamba nimejigeuza muhubiri bali najaribu kuangalia ni busara gani itumike kulimaliza suala hili.
Presentation of any false information ikijumlisha na documents ni kosa na lazima pawe na mwanzo wa kulionyesha kuwa hili ni kosa, na hapo unapoanzia huo mwanzo ni wapi kama sio leo!?
Na hili ndilo linapelekea tatizo lingine ...kuwa unao wafanyakazi na 'wanafikia malengo' kila uchao lakini ghafla unagundua kuwa wamedanganya, tukumbuke hapa kuwa uongo ni uongo tu. Kwa hiyo unawafukuza alafu unaenda kutangaza ajira za muda ili kuziba pengo lao, hapa utaulizwa ni kwa nini usingeliwatumia hawa hawa kwa 'mfumo maalumu' ili wakati wakiondoka basi wengine wafanye 'automatic replacement'.

Alafu suala lingine, hawa watu walikuwa wanafanya kazi na 'kufikia malengo ya serikali', tunaweza kushangaa baadae kuwa walikuwa wana deliver kuwazidi wenye vyeti halali lakini elimu fake. Mfano wa hili ni kama sekta binafsi ambako STD VII na Form IV failure wanafanya vizuri zaidi wakati graduates wakichechemea! Let us wait and see.
 
Siku atakapogeukia kwako kwa kisingizio kingine usiache kupost tena. Anachofanya Mzee wenu kama ingekua Ni mpira Ni anapoteza muda, mkija kutahamaki refa anamaliza mpira.
Kwa nini usipoteze muda wakati hadi mapunziko umefunga goli tano bila? Au unahitaji sare baada ya nyumbani kupata goli tano bila. Mh Magufuli kwa mwaka wa kwanza tu kaanzisha utekelezaji wa asilimia 80 ya mambo yaliopo katika ilani ya uchaguzi ya ccm 2015/2020.
 
Back
Top Bottom