Dodoma: Mwigulu, Serukamba na Nkamia matatani!

Dodoma: Mwigulu, Serukamba na Nkamia matatani!

Ila nakumbuka kwenye kikao cha NEC Kikwete alimpa kibali Nchemba cha kutukana bungeni na kusisitiza wabunge wote wa ccm watumie style hii ya Mwigulu Nchemba kujibu hoja za chadema,

Style hii mpya ya Serukamba inaonyesha dhahiri kuwa inamfurahisha sana JK kama mwenyekiti wa CCM.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Makubwa haya. Tunajua na kuthibitishwa bungeni kuwa JK ni muasisi, mratibu na mkurugenzi mtendaji wa udine. Je imekuwa hivyo pia kwa matusi ya Bungeni?
 
Hili ndio Bunge la ukweli.....bunge la Ukraine

529566_10200428088418024_512944390_n.jpg


kuna mbunge mwingine wa nyuma sijui mkono umefikaje hapo?
 
Kwa mtu mwenye akili timamu anaweza kutambua kuwa kitendo wanachotufanyia wabunge sisi watanzania ni mzaha na utani mpaka baadhi ya mawaziri.

Ni mwananchi gani aliyesota kwenye mstari tangu asubuhi atumie demokrasia yake ya kupiga kura halafu ategemee kusikia maneno kama:


1.Siongei na mbwa,naongea na mwenye mbwa
2."....mtoto wa Dr. Slaa ana wiki mbili..."
3."...pumbavu...."
4."....huyu niachieni mimi na mwigulu..."
5.----y you...!
6."....kuna wabunge wana mimba zisizo tarajiwa....." nk.
Najua kuna watu walikuwa wanatumia lugha za picha kumaanisha jambo fulani,ni sawa, lakini kwa hali nchi ilivyo sasa,nadhani wabunge hawa wangejikita kujadili matatizo ya wananchi na nchi kwa ujumla kuliko kuonyeshana ufundi wa kuongea na kushambuliana wao kwa wao.

Pili nilitaka kujua kama wabunge hawa wapotumia muda huu kulumbana kwa matusi,je,majimboni kwao hali ikoje katika mabo haya?
1.barabara
2.elimu
3.afya
4.mfumuko wa bei
5. maji
6.watoto na wazee wenye mazingira magumu nk.
Tatu,kwanini wasijadili hali amani ya nchi,anguko la elimu,mikataba mibovu,ufisadi, utendaji mbovu,mafuriko,nk?
Mawazo yangu,kama hali ni hii ni heri nchi kutokuwa na bunge,na itafutwe namna nyingine ya kujadili na kuendesha nchi kuliko kuwalipa watu kwa kodi zetu ,lakini kazi yao nikuonyeshana ufundi wa matusi.

Aksante.













K
Kuna uwezekano mkubwa Wabunge Mwigulu Nchemba,Peter Serukamba na Juma Nkamia wakahojiwa na Kamati Maalum ya Nidhamu ya Wabunge wa CCM kwa kile kinachosemwa kuwa ni kukichafua chama-CCM. Wabunge hao,kwa nyakati tofauti,wamesikika wakitukana na kutumia lugha ya kuudhi Bungeni. Nani atawagusa watukanaji hawa? Taarifa zaidi zitafuata kadiri zitakavyopatikana. VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam(sasa Dodoma)
 
nani kakwambia kwamba wana wa mfalme wanaweza kuchukuliwa hatua za kinidhamu??? ni sisi wananchi wapenda mabadiriko tunaoweza kuwachukulia hatua kupitia sanduku la kura! kipindi cha kampeni wakija kuomba kura tunawapokea kwa kelele kama za mbwa anayebweka maana mbunge mwenzao alitamka Bungeni kwamba hawezi kuongea na mbwa bali mwenye mbwa!
 
Hili ndio Bunge la ukweli.....bunge la Ukraine

529566_10200428088418024_512944390_n.jpg
Nakumbuka hii ni baada ya kiongozi wa upinzani kutoa hotuba yake kwa lugha la ki-Russia. Hilo tu lilitosha kusababaisha ngumi kurushwa ukumbini. Ingekuwa ni upuuzi kama wa akina Chemba nadhani watu wangerushiwa risasi.
 
Sidhani kama ndani ya CCM kuna mtu hata mmoja mwenye jeuri ya kulisimamia hilo. Kama kweli kungekuwa na nafasi ya kamati ya nidhamu kufanya lolote, basi ingeshakuwa ilimchukulia hatua Lusinde baada ya matusi yake yale ya Arumeru.
To me, CCM na matusi ni chanda na pete. Na ninafikiri hii style ya sasa imesukwa na chama chenyewe kama mbinu mojawapo ya kuikabili CHADEMA. So sitarajii kwamba CCM kuna hata mmoja mwenye hekima ya kuweza kuhoji haya.
Landa Filikunjombe lakini naye wameishamkana kuwa sio CCM tena!.
 
Sidhani kama ndani ya CCM kuna mtu hata mmoja mwenye jeuri ya kulisimamia hilo. Kama kweli kungekuwa na nafasi ya kamati ya nidhamu kufanya lolote, basi ingeshakuwa ilimchukulia hatua Lusinde baada ya matusi yake yale ya Arumeru.
To me, CCM na matusi ni chanda na pete. Na ninafikiri hii style ya sasa imesukwa na chama chenyewe kama mbinu mojawapo ya kuikabili CHADEMA. So sitarajii kwamba CCM kuna hata mmoja mwenye hekima ya kuweza kuhoji haya.
Labda Filikunjombe, lakini naye wameisha mkana kuwa sio mwenzao!. MaCCM bwana wanajitenga na ukweli wowote ule.
 
Ngoja tusubiri,lakini napata mashaka kama kweli watafanya hivyo yaani kuwahoji,maana kama lengo ni kujisafisha mble ya watanzania walioshuhudia matusi hayo yakiporomoshwa walitakiwa maspika kuwachukulia hatua za kinidhamu haraka tena hadharani kama walivyowafanyia kina Lissu,kinyume chake wakapotezea leo hata wakijifanya kuwaita kwenye kamati ya siasa bado haitakuwa sabuni ya kuwatakatisha kwa uchafu unaonuka mbele za watanzania.
 
Kuna uwezekano mkubwa Wabunge Mwigulu Nchemba,Peter Serukamba na Juma Nkamia wakahojiwa na Kamati Maalum ya Nidhamu ya Wabunge wa CCM kwa kile kinachosemwa kuwa ni kukichafua chama-CCM. Wabunge hao,kwa nyakati tofauti,wamesikika wakitukana na kutumia lugha ya kuudhi Bungeni. Nani atawagusa watukanaji hawa? Taarifa zaidi zitafuata kadiri zitakavyopatikana. VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba, Nadhani hivyo ni viini macho tu.
 
Last edited by a moderator:
Nadhani hivyo ni viini macho tu. Lkn hata hivyo hukumu yao yaja si wanadhani wananchi wamewachagua kuoneshana ufahari wa matusi badala ya masuala muhimu ya wananchi. Siku hizi sifa pekee ya promotion ktk chama hicho ni kiasi gani mtu ni bingwa wa kuporomosha matusi kwa wapinzani. Kweli mwovu mti hauzai matunda bora kamwe.
 
Nawaambia waache uwendawazimu! kama ni vikao wawafanyia Mbwa mkubwa na mbwa msaidizi ndio wanaowaachia hao mbwa waliotajwa kwa majina yao kuki-Serukamba chama chao!.
 
Kuna uwezekano mkubwa Wabunge Mwigulu Nchemba,Peter Serukamba na Juma Nkamia wakahojiwa na Kamati Maalum ya Nidhamu ya Wabunge wa CCM kwa kile kinachosemwa kuwa ni kukichafua chama-CCM. Wabunge hao,kwa nyakati tofauti,wamesikika wakitukana na kutumia lugha ya kuudhi Bungeni. Nani atawagusa watukanaji hawa? Taarifa zaidi zitafuata kadiri zitakavyopatikana. VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba, Nadhani hivyo ni viini macho tu.

Lkn hawa waliomba radhi live tuliona ,wale wengine wavuta bangi tumeona kabisa wakifanya fujo.
 
Last edited by a moderator:
January ,m ametulia sana jamani utafikiri amesomea hekima na busara yani yuko kimya hataki kelele kabisa.
 
Back
Top Bottom