Dr Bashiru wewe ndio unaingia kwenye Historia kuwa Katibu Mkuu uliyefeli kuliko Makatibu wakuu wote, Siasa zako zilikuwa za kununua Wapinzani, kuwalazimisha Wapinzani na Sio kuwashawishi watu wakipende Chama chetu cha Mapinduzi CCM, umesahau?
Bashiru wewe ndiye uliwanyima Uhuru wazee wetu akina Membe, Kinana, Mzee Makamba ukiwaziba mdomo wa kutoa hata mawazo yao mujarabu wa ajili ya Chama na Serikali yetu, je na uhalali gani wa kutukemea tusipongeze "upiga mwingi" wa Mama Samia?
Bashiru na genge lenu tunafahamu hamfurahii huu Uhuru anaoutoa Rais Samia mnataka kuturudisha huko nyuma kwa Wapinzani kukimbia Nchi, mnataka kuturudisha kwenye Nchi ya "Free Fulani katekwa," viroba vya maiti zimeokotwa baharini? Wakosoaji wamebambikiziwa kesi? Wamehohiwa uraia wao?.....