Hii Dunia ni ndogo sana hawa DKT BASHIRU ALLY na POLEPOLE walifikiria watakuwa viongozi wa maisha.
- Ilifika wakati walikuwa wanatoa hongo na kununua wapinzani hasa wabunge na madiwani.
- Waliahidi vyeo kwa wapinzani wanaokuja CCM bila kujali uwezo wao na nchi kwa ujumla
- Walirekodi kwa kudukuwa simu za Raia binafsi ilimradi tu kwa wao waliowaona kama wapinzani. Hizi rekodi za simu zao ni bila kufuata sheria! lakini walitoa maaagizo hayo
- Waliharibu uchaguzi wa Tanzania 2020 kwa kutoa maelezo kwa polisi na usalama waibe kura tena waziwazi
- Walitaka nchi yetu isiwe na vyama vya upinzani kabisa kinyume na sheria
- Walitaka turudi kwenye ujamaa na kujiweka karibu ya vyama vya kikandamizaji vya China
- Waliwadharau Madaktari na kuweka kampeni zisizo na tafiti kwenye Corana mpaka tukapoteza viongozi wengi wa juu
- Wapinzani walikuwa maadui mpaka kupigwa risasi na vikosi vya usalama wa taifa vya siri.