Dkt. Abbas: Tusimparure Rais, tumpetipeti

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,185
103,685
Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi wakati wa uzinduzi wa Royal Tour Dodoma leo amempongeza Rais Samia kwa kazi kubwa aliyoifanya wakati wa utengenezwaji wa Filamu hiyo "Tumpongeze Rais wetu, nitawapa mikasa miwili"

"Kuna sehemu Rais anavua samaki ilikuwa Pemba, za ndani tu ni kwamba ilimchukua Rais kutwa nzima kurekodi tukio la kuvua samaki, tulipofika Pemba tukakuta Bahari ina mawimbi makubwa, mwingine angesema tuondoke ila Rais akasema tusubiri akatutania 'wengine sio Watu wa Pwani hamjui kuwa Bahari ikifika saa nane tisa inatulia', Rais akasubiri tangu saa 4 asubuhi hadi saa 9 kwenda saa 10 alasiri, makofi kwa Rais"

"Kingine ni siku alipokuwa anaingiza voice over kuna masimulizi yalifanyika field mengine alirekodi Ofisi kwake, Mimi ni miongoni mwa Waumini wa shughuli za Ikulu maana ukinywa juisi au kula samaki Ikulu ni juisi au samaki muhimu kuliko wote Duniani , tulijiandaa na wenzangu tukasema tume-miss Juisi na samaki wa Ikulu, kufika Ikulu Rais alirekodi voice over kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 2 usiku bila kupata chakula cha mchana zaidi ya korosho na juisi tu"

"Wengine tunarajia pilau litakuja lakini wapi Rais anapiga kazi, saa 2 usiku amemaliza kazi tukaagana hakuna lunch wala dinner, huyu Mimi ningedhani ni Kiongozi ambaye badala ya kumparura tungempetipeti kwasababu wako miongoni mwetu wangepata hiyo nafasi Rais wa Nchi unarekodi Royal Tour angeweza kuitisha pilau, ugali na nyama, chips kuku lakini Rais Samia yupo kazini ameweka pembeni masuala mengine yote"

My Take
Sioni tofauti ya KM na hawa Chawa wa mitandaoni
 
Nukuu zako zimeondoa vitu muhimu vya kuoanisha mada na kichwa cha mada. Sijasikiliza alichosema KM lakini kupitia nukuu zako naona kuna hujakisema
 
Namuunga mkono Dr. Abbas

Tanzania tumebahatika kupata rais mwanamke, she is a woman, a lady, mambo ya kupetiwa petiwa ni mahitaji ya wanawake wote Duniani, hivyo kila mtu kwa upande wake.

Sisi media hata mwenyewe katuasa bayana kabisa tukimkuna vizuri, she'll scratch back, ila tukimpara... media tusimpare Ila pia...

P
 
Tumpake vilainishi maza yenu.
Hapana Mkuu, hii mitandao isikudanganye sana kujiona uko salama hadi kuvuka mipaka ya kukosa heshima kiasi hicho Kaka.

Kumbuka hata nawe una Mama, hata kama haupendezwi na Mama yetu "Rais wa TZ sasa" basi jitahidi kuepuka mihemuko ya hasira kali ili mdomo usiponze kichwa.
 
Namuunga mkono Dr. Abbas

Tanzania tumebahatika kupata rais mwanamke, she is a woman, a lady, mambo ya kupetiwa petiwa ni mahitaji ya wanawake wote Duniani, hivyo kila mtu kwa upande wake.

Sisi media hata mwenyewe katuasa bayana kabisa tukimkuna vizuri, she'll scratch back, ila tukimpara... media tusimpare Ila pia...

P
Ukishakuwa kiingozi mkuu watuwote wanategemea kuona huduma yakiwango cha juu kutoka kwako sababu wewe ndio mtu bora kuliko wote, hakuna excuse za genda me ama ke, kama unavyo sema hapo.

Ningekuwa na maamuzi nisinge ruhusu rais wangu kucheza hiyo filam.
 
Wajenge sanamu tuwe tunaliabudu maana naona sifa wanazompa hazitoshi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom