Dk. Slaa: UCHAGUZI WIZI MTUPU

Dk. Slaa: UCHAGUZI WIZI MTUPU

Hii ni zaidi ya kuchakachua bali ni ujambazi wa mchana kweupe. Tunasubiri data kamili zimwagwe ili waumbuke hawa chama cha majambazi
 
CCM SAFARI HII LAZIMA TUWAVUE NGUO WATEMBEE UCHI.
DR. SLAA ANAENDELEA KUKUSANYA NYARAKA ZOTE MUHIMU ZA UCHAGUZI WA MWAKA HUU WA 2010. NINAMWAMINI DR.SLAA KWASABABU NI DR. WA UHAKIKA NAAMINI ATAKAPOTOKA NA RIPOTI YAKE KISHINDO CHAKE KITAKUWA ZAIDI YA EPA!

Tusubirini vitu vinakuja. CCM lazima waumbuke safari hii!!!
 
Kuna jambo moja hadi sasa limenipa shida sana kuelewa. Nakumbuka Dr.Slaa alisema kwamba kuna Kontena limeshikwa mpakani Tunduma likiwa na form za kupigia kura feki kisha uchunguzi ukafanywa na ikaonekana sii kweli bali vilikuwa vipodozi kulingana na madai ya vyombo vya ulinzi.

Sasa ilikuwaje tena kuna form feki zimepatikana mikononi mwa wasimamizi ktk vituo vya kupigia kura (i.e Segerea), Hizi form zimetoka wapi? na mbona hatuna maelezo zaidi kuhusiana na jinai hili la kuwepo vituoni na wahusika wake kuhojiwa hadharani ili tupate kusikia ukweli kuhusiana na form hizo!
 
Yaani watu wa Geita pamoja na matatizo yao ya migodi ikiwemo kunyweshwa maji machafu yenye zebaki (mercury) bado wanaipigia CCM kura nyingi hivyo? Lol! Kweli wajinga ndio waliwao.
 
Haya ni kweli kabisa!
Angalia idadi ya watu waliojiandikisha kupiga kura ni zaidi ya milioni 20, halafu eti waliojitokeza kupiga kura ni milioni 8 tu. Kwa mtu mwenye akili timamu huoni hapa kuna tatizo?
 
namwombea dua mbaya huyu jamaa. Amezidi kuwanyonya watanzania, huu wizi mtupu kabisa. Natamani akalazwe kama demu wake anayeendelea kuugua kitandani. Wanasingizia magonjwa mengine wakati ukweli unajulikana.

Inauma sana tunaibiwa kura hivi tunaona!!! Bora damu imwagike kwa hali hii kuliko kuendelea kuteswa. Angalia bei za vitu zilivyopanda hata serikali haijaundwa bado.
 
CCM kama ungekuwa ni mwanaume, ningekupiga chini siku ya kwanza Sandra-Bullock-Marriage-Trouble.jpg .
 
mimi baada ya kusoma report hii machozi yalinitoka,ninauchungu sana na inchi yangu hasa haya mafisad yanapochakachua kura zetu,mimi nikopamoja na dr slaa 2namuunga
mkono kwa kaz anayoifanya sisi kama wanainchi wazalendo 2potayari kupigana kwaajilietu na vizazi vijavyo.

CCM hatuwatambui kama watawalawetu, safariyao imeishia hapo.
 
Nadhani ukiibiwa kura, lazima una ujinga fulani hivi.Kama kila siku unaibiwa wewe tuna wasiwasi unaweza kuibiwa hata nchi ukiwa madarakani.

Tusipende kuomba huruma, kila tukishinda sawa tukishindwa tumeibiwa, tujipange ili na sisis tuwaibie kama kuiba ni ushindi. Viongozi wetu waache ubabaishaji, tukishindwa watuambie jinsi ya kujipanga.
 
Nadhani ukiibiwa kura, lazima una ujinga fulani hivi.Kama kila siku unaibiwa wewe tuna wasiwasi unaweza kuibiwa hata nchi ukiwa madarakani.

Tusipende kuomba huruma, kila tukishinda sawa tukishindwa tumeibiwa, tujipange ili na sisis tuwaibie kama kuiba ni ushindi. Viongozi wetu waache ubabaishaji, tukishindwa watuambie jinsi ya kujipanga.

Inasikitisha watu ambao tunaweza kuwaita wasomi wakaongea kama wewe.Usilolijua nikama usiku wa giza.
 
Back
Top Bottom