muonamambo,
Asante sana kwa comment yako. Najua wengi wangelipenda tutoe Tamko haraka haraka. Mambo magumu hayahitaji ushabiki, wala haraka haraka. Tukumbuke haraka haraka haina baraka. Niseme tu uwizi wa kura mwaka huu ni wa kutisha sana. Hivyo tunajiandaa kikamilifu, ili tutakapotoka kusiwe na shaka lolote. Kuna mambo mawili, tunaweza kutoa Tamko la kisiasa na hatimaye Tamko lenye Data. Lakini pia ujue kuwa Tamko la namna hiyo inatolewa siyo na Dr. Slaa, bali na vyombo vya maamuzi ya Chama,kwani katika siasa hakuna jambo muhimu kama kushirikishana. Naomba subiri, si muda mrefu Tamko litatoka. Ninalotaka kuwahakikishia watanzania ni kuwa hatuwezi kuwaangusha kamwe, na wala hatuwezi kuwauza.
Tunawaahidi Watanzania kuwa Wabunge takriban 45 wa Chadema wataendeleza jitihada za kumkomboa Mtanzania. Ajenda ya Wabunge wetu licha ya kushughulikia majimbo yao, lakini Wabunge wa Chadema watakuwa katika ujumla wao Wabunge wa Taifa, na watakuwa wakishughulikia kupitia Bunge maswala ya kitaifa ili hatimaye tufikie lengo letu la kumkomboa Mtanzania, wote wanaohitaji ukombozi yaani wakukulima, wafugaji, wafanyibiashara(wasio mafisadi) kwa lugha ya kawaida Walalahoi. Ninachoomba kwa wote wenye nia njema, tuendelee kushikamana, kushirikiana kwani vita vya ukombozi si vya mtu mmoja wala siyo vya kundi la watu au chama fulani tu, bali wote wenye nia na malengo yanayofanana. Najua tuko wengi wenye nia ya aina hii. Kwa mara nyingine tena, nawashukuru sana Wana JF kwa ushirikiano, ushauri, mawazo japo wakati mwingine yamekuwa very critical yametusaidia sana kujielekeza(focused) na kulenga "real issues". Nawashukuru sana wale wote walioniombea muda wote mkono wangu ulipokuwa umevunjika. Nashukuru mkono unaendelea vizuri, na hata sasa kwa mara ya kwanza leo ninafanya "blind typing" kwa mikono yote miwili. Namshukuru sana Mungu. Mungu awabariki nyote na Mungu ibariki Tanzania.