Dk Slaa kuanika hadharani nchi nzima posho za wabunge

Mtanzania

JF-Expert Member
May 4, 2006
4,816
678
Dr. Slaa, mimi nakuunga miguu na mikono yote juu ya hili.
Dk Slaa kuanika hadharani nchi nzima posho za wabunge

Na Mussa Juma, Arusha.
MBUNGE wa jimbo la Karatu, Dk Willibrod Slaa (Chadema) amewataka?baadhi ya wabunge wanaomshutumu kwa kutangaza hadharani mishahara na posho za wabunge, kukaa kimya kwani amepanga kutembea nchi nzima na kutangaza mishahara hiyo ili wananchi wajue jinsi ambavyo nchi yao inaliwa na wachache.

Dk Slaa pia alisema licha ya kutangaza malipo hayo ili wananchi wayapinge kwa nguvu pia anapinga kutokatwa kodi mishahara na marupurupu yote ya wabunge jambo ambalo kwa mwezi linalipotezea taifa mabilioni ya fedha ambayo yangeweza kusaidia huduma za jamii.

"Nchi hii wanasema ni masikini, fikiria kuna wabunge 320 walipwe posho wakiwa Dodoma 135,000 kwa siku, mwisho wa mwezi milioni saba ambazo ni kiasi kidogo tu kinakatwa kodi. Hili ni jambo la ajabu?Ebu tazama maisha ya Watanzania vijijini na wamuogope Mungu," alisema Dk Slaa.

Akizungumza katika mikutano ya hadhara katika jimbo lake la Karatu, Dk Slaa alisema nia yake ya kutangaza posho, mishahara pamoja na marupurupu ya wabunge ni kuibua mjadala wa kitaifa ili malipo hayo ya wabunge na maofisa wengine wa serikali kupunguzwa.

Kwa kutumia mikutano ya 'Operation Sangara' nitatembea nchi nzima kufafanua jambo hili hata kama wakinifukuza bungeni sintojali kwani mimi nina dhamira ya kweli ya kuwatetea Watanzania wote," alisema akifafanua:


"Hawa wanaonipinga kwanza wanaishi Dar es Saalam, kwenye majimbo yao hawaendi, wanaogopa kutoa misaada kwa wapiga kura wao.?p> ?p> Alisema Rais Jakaya Kikwete aunde tume maalum ya kupitia maslahi ya wabunge na watumishi wote wa umma kwani sasa kuna tofauti kubwa sana ya mishahara jambo ambalo ni hatari kwa taifa.

Sasa jaribu kufikiria mishahara ya walimu wetu, madaktari, polisi ni sawa na posho ya siku ya mbunge au posho ya siku moja ya kiongozi anayehudhuria kikao cha bodi?Hili jambo hatari sana?na tusijifananishe na wabunge wa Kenya na Uganda, wao wana uchumi na taratibu za malipo tofauti na sisi,?alisema Dk Slaa.

Dk Slaa ambaye pia ni Katibu mkuu wa Chadema, alisema lazima tume au kamati maalum iundwe sasa kabla hali haijakuwa mbaya zaidi, ili kila mtumishi wa umma alipwe kutokana na ujuzi wake na uzoefu wake, sio sasa kundi moja linanufaika zaidi.

Akizungumzia tuhuma za baadhi ya wabunge kuwa ni mmoja wa wajumbe wa kamati ya bunge iliyopitisha nyongeza ya posho na marupurupu ya wabunge, Dk Slaa alikanusha na kudai kamati ya bunge inayotajwa haikuwahi kujadili suala la posho na malipo ya wabunge.

Ile kamati wanayoitaja ilikuwa inaongozwa na Job Ndugai ilikuwa ni ya kujifunza kanuni za bunge ambazo zinatumika katika nchi mbali mbali.


Kuna wabunge wanataka kupotosha hoja yangu, jambo hili lina msukumo wa watu wachache na lilijadiliwa katika Kamisheni ya bunge na mimi na wenzangu Chadema tunalipinga,?alisema Dk Slaa.


Alisema tangu mwaka 2006 amekuwa akilalamika bungeni juu ya malipo manono ya wabunge na watumishi wa kada za juu wa serikali, lakini amekuwa haeleweki isipokuwa amefarijika sasa Watanzania wameanza kumuelewa.


Alisema katika kikao kijacho cha bunge pia atalizungumza suala hilo la mishahara na posho za wabunge kupunguzwa na kukatwa kodi bila ya kificho na bila kumuogopa mtu yeyote.



Dk Slaa alipinga utetezi wa wabunge kuwa wana majukumu makubwa jimboni na kudai wengi wa wabunge wanaishi jijini Dar es Salaam na hakuna taarifa ya mahesabu ambayo wanatoa jinsi wanavyotumia fedha zao.
 
Ni vizuri tujue na wabunge wengine waende kwenye majimbo yao wafafanue kuhusu hii mishahara waache kulalamika ni kweli ni mikubwa mno. na kama kweli haikatwi kodi huu ni unyonyaji, ndio maana wengi wao wanalala bungeni kwani wanauhakika maisha mswano.

Mishahara haijawahi kuwa siri hususan ya watumishi wa umma isipokuwa TZ.
USA wanasiasa ni rahisi sana kujua mishahara yao kwani ni lazima waijulishe serikali juu ya mapato yao kila mwaka. Tujue fedha zetu wanazokula kila mwezi wanafanya kazi kwa mishahara hiyo au wanatuibia fedha na kazi zero.

Dr bingwa analipwa chini ya milioni moja na nusu mmbunge millioni saba plus marupurupu anaondoka na wastani wa zaidi ya millioni kumi kwa mwezi.

kazi kweli, sasa tunaona sababu kwanini kila mtu anataka kuwa mbunge.
 
Sawa Slaa,
Tuko na wewe BEGA KWA BEGA. Tungelipata wengine wakusaidie kwa hili, lohh kungelifumuka mabadilko makubwa sana. Kweli kuna haja ya kumpa kazi kubwa zaidi Slaa.
 
Date::4/4/2009

Dk Slaa kuanika hadharani nchi nzima posho za wabunge

Na Mussa Juma, Arusha

Mwananchi

MBUNGE wa jimbo la Karatu, Dk Willibrod Slaa (Chadema) amewataka baadhi ya wabunge wanaomshutumu kwa kutangaza hadharani mishahara na posho za wabunge, kukaa kimya kwani amepanga kutembea nchi nzima na kutangaza mishahara hiyo ili wananchi wajue jinsi ambavyo nchi yao inaliwa na wachache.

Dk Slaa pia alisema licha ya kutangaza malipo hayo ili wananchi wayapinge kwa nguvu pia anapinga kutokatwa kodi mishahara na marupurupu yote ya wabunge jambo ambalo kwa mwezi linalipotezea taifa mabilioni ya fedha ambayo yangeweza kusaidia huduma za jamii.

"Nchi hii wanasema masikini, fikiria kuna wabunge 320 walipwe posho wakiwa Dodoma 135,000 kwa siku, mwisho wa mwezi milioni saba ambazo ni kiasi kidogo tu kinakatwa kodi. Hili ni jambo la ajabu… Ebu tazama maisha ya Watanzania vijijini na wamuogope Mungu," alisema Dk Slaa.

Akizungumza katika mikutano ya hadhara katika jimbo lake la Karatu, Dk Slaa alisema nia yake ya kutangaza posho, mishahara pamoja na marupurupu ya wabunge ni kuibua mjadala wa kitaifa ili malipo hayo ya wabunge na maofisa wengine wa serikali kupunguzwa.


“Kwa kutumia mikutano ya 'Operation Sangara' nitatembea nchi nzima kufafanua jambo hili hata kama wakinifukuza bungeni sintojali kwani mimi nina dhamira ya kweli ya kuwatetea Watanzania wote," alisema akifafanua:

"Hawa wanaonipinga kwanza wanaishi Dar es Saalam, kwenye majimbo yao hawaendi, wanaogopa kutoa misaada kwa wapiga kura wao.”

Alisema Rais Jakaya Kikwete aunde tume maalum ya kupitia maslahi ya wabunge na watumishi wote wa umma kwani sasa kuna tofauti kubwa sana ya mishahara jambo ambalo ni hatari kwa taifa.


“Sasa jaribu kufikiria mishahara ya walimu wetu, madaktari, polisi ni sawa na posho ya siku ya mbunge au posho ya siku moja ya kiongozi anayehudhuria kikao cha bodi… Hili jambo hatari sana na tusijifananishe na wabunge wa Kenya na Uganda, wao wana uchumi na taratibu za malipo tofauti na sisi,” alisema Dk Slaa.

Dk Slaa ambaye pia ni Katibu mkuu wa Chadema, alisema lazima tume au kamati maalum iundwe sasa kabla hali haijakuwa mbaya zaidi, ili kila mtumishi wa umma alipwe kutokana na ujuzi wake na uzoefu wake, sio sasa kundi moja linanufaika zaidi.

Akizungumzia tuhuma za baadhi ya wabunge kuwa ni mmoja wa wajumbe wa kamati ya bunge iliyopitisha nyongeza ya posho na marupurupu ya wabunge, Dk Slaa alikanusha na kudai kamati ya bunge inayotajwa haikuwahi kujadili suala la posho na malipo ya wabunge.

Ile kamati wanayoitaja ilikuwa inaongozwa na Job Ndugai ilikuwa ni ya kujifunza kanuni za bunge ambazo zinatumika katika nchi mbali mbali.

“Kuna wabunge wanataka kupotosha hoja yangu….jambo hili lina msukumo wa watu wachache na lilijadiliwa katika Kamisheni ya bunge na mimi na wenzangu Chadema tunalipinga,” alisema Dk Slaa.

Alisema tangu mwaka 2006 amekuwa akilalamika bungeni juu ya malipo manono ya wabunge na watumishi wa kada za juu wa serikali, lakini amekuwa haeleweki isipokuwa amefarijika sasa Watanzania wameanza kumuelewa.

Alisema katika kikao kijacho cha bunge pia atalizungumza suala hilo la mishahara na posho za wabunge kupunguzwa na kukatwa kodi bila ya kificho na bila kumuogopa mtu yeyote.


Dk Slaa alipinga utetezi wa wabunge kuwa wana majukumu makubwa jimboni na kudai wengi wa wabunge wanaishi jijini Dar es Salaam na hakuna taarifa ya mahesabu ambayo wanatoa jinsi wanavyotumia fedha zao.

 
Dr Slaa usisahau kuwaelezea Watanzania na zile shilingi milioni 40 ambazo kila mbunge anapewa baada ya Bunge kuvunjwa miezi michache kabla ya uchaguzi Mkuu. Hizo milioni 40 kwa Wabunge 320 ni pesa nyingi mno nazo kuna haja ya kuzipunguza kwa kiasi kikubwa.
 
Bubu Kwa Kopy na Paste zako....Unaharibu Forums..unaona kama unajenga kumbe unaharibu. Hii mada tayari Mtanzania Kaiweka..wewe bila kuangalia unakuja weka. Unaona umejijengea Hati Miliki ya Kukopy na paste news za magazeti....

Nitaendelea kukuunyoosha...before kukopy na kupaste na kujifanya kubold..kuweka color na mistari..please angalia kwanza!!!!
 
Ni vizuri ikiwa ataliweka wazi lakini mradi asilitumie hili kama ni sera ya CCM au ni matakwa ya Rais, au ni RA ndie aliyetengeneza hayo marupurupu.

Mimi ningependelea kuona wabunge wanafanya shughuli zao kwa kujitolea kama wafanyavyo mabalozi (wajumbe) wa nyumba kumi, na ikiwezekana isiwe kazi ya mshahara wala marupurupu kabisa.

Na wawekewe kantini na nyumba za kulala wageni wanapokuwa Bungeni, wanaporudi majimboni kwao watumie pesa zao kuwakilisha wananchi na ataeona hawezi aachie wengine watafanya.

Lakini kuna kazi kweli hapo kwani wanaojipangia hizi sheria ni wao wenyewe.

Nnachosema na yeye asitumie haya marupurupu kuwa ni njia ya mkato kuelekea 2010. Anapowapelekea wananchi hii habari awaambie wanachi kuwawekea sharti wagombea ubunge wa jimbo lao ya kuwa, sharti la kuchaguliwa kwao ni kuwa akifika tu bungeni apigie kura kukwata marupurupu yake yote na itungwe sheria mpya kuhusu hilo!

Ikiwa hivyo itakuwa swaaafi kweli.
 
Bubu Kwa Kopy na Paste zako....Unaharibu Forums..unaona kama unajenga kumbe unaharibu. Hii mada tayari Mtanzania Kaiweka..wewe bila kuangalia unakuja weka. Unaona umejijengea Hati Miliki ya Kukopy na paste news za magazeti....

Nitaendelea kukuunyoosha...before kukopy na kupaste na kujifanya kubold..kuweka color na mistari..please angalia kwanza!!!!

Chuma

Hebu acha uzabinazabina, bubu anafanya ngazi nzuri sana hapa. Na anatumia muda mwingi kutufanya tuone maeneo yenye mkazo ya habari.

Sasa kama hakuona kwa bahati mbaya kama kuna post nyingine tayari si uwaambie kuistaraabu tu moderators waunganishe thread badala ya kumshambulia hivyo!

Mbona unamfuata fuata hivyo, au ali bold mistari kwenye habari iligusa hisia zako nini?

Halafu hivi Chuma maanake nini? Ni chuma ya tendo la kuchuma kama vile mboga au ni chuma ya chuma cha pua?

Asha
 
cha msingi hapa sio kuwa kuna mtu anacopy na kupaste ila ni umuhimu wa habari yenyewe kwetu sisi. kwani kwenye habari kama hizi kuna copy rights protection. tuache mambo hayo hata wewe unaruhusiwa kucopy na kupaste.
 
Bubu Kwa Kopy na Paste zako....Unaharibu Forums..unaona kama unajenga kumbe unaharibu. Hii mada tayari Mtanzania Kaiweka..wewe bila kuangalia unakuja weka. Unaona umejijengea Hati Miliki ya Kukopy na paste news za magazeti....

Nitaendelea kukuunyoosha...before kukopy na kupaste na kujifanya kubold..kuweka color na mistari..please angalia kwanza!!!!

i will have to disagree with u..wengine hatuko bongo na hatuna access ya kusoma haya magazeti mengine..this copy and paste is appreciated!!
 
Bubu Kwa Kopy na Paste zako....Unaharibu Forums..unaona kama unajenga kumbe unaharibu. Hii mada tayari Mtanzania Kaiweka..wewe bila kuangalia unakuja weka. Unaona umejijengea Hati Miliki ya Kukopy na paste news za magazeti....

Nitaendelea kukuunyoosha...before kukopy na kupaste na kujifanya kubold..kuweka color na mistari..please angalia kwanza!!!!

Roho mbaya tu, nothing else!!
 
Kweli inasikitisha mishahara na posho ni makubwa ikilinganisha na hali halisi ya uchumi.Ni kichekesho kwa kuringanisha mishahara ya nchi jirani .Kila nchi inataratibu zake za kupanga mishahara.Kwanini tukimbilie kutazama nchi jirani katika swala la mishahara posho na marupurupu tu!? Kwanini tusitafute mifano yao katika utendaji kazi katika kunyanyua maisha ya mwananchi wa kawaida na mataifa yao kiuchumi kwa ujumla .Nchi yetu imekua na bahati ya kutokua na vita nchi yetu inarasilimali za kutosha(Madini,mbuga za asili,maziwa,mito) lakini walalahoi hawanufaiki wanaonufaika ni Viongozi wetu wakiwemo wabunge .Uchumi wetu unapiga makitaimu alimu yetu inapimwa kwa kuongeza idadi ya madarasa yasiyo na vitabu,vifaa vya kufundishiwa wala walimu.Huduma ya afya inapimwa kwa kujenga majengo yasio na dawa,vifaa au madaktari majengo na madarasa ambayo uwekaji wa misingi na ufunguliwa kwa mbwebwe!Wenzetu majirani ambao kwa baadhi ya nchi zilikua katika vita na hazina rasilimali kama tulizonazo lakini sasa wanatupita.Kwa wabunge hao kupata mishara na posho hizo huwenda pia ni kubwa lakini wanastahili kwani kunamatokeo yanayoonekana.Mishahara na posho kama hiyo kwa wabunge mimi naichukulia kama ruswa inayotolewa na serikali ili kuwanyamazisha.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Bubu Kwa Kopy na Paste zako....Unaharibu Forums..unaona kama unajenga kumbe unaharibu. Hii mada tayari Mtanzania Kaiweka..wewe bila kuangalia unakuja weka. Unaona umejijengea Hati Miliki ya Kukopy na paste news za magazeti....

Nitaendelea kukuunyoosha...before kukopy na kupaste na kujifanya kubold..kuweka color na mistari..please angalia kwanza!!!!

Wewe fisadi hebu nyamaza watu wamechoka na kelele zako za kitaahira. Huna chochote unachoandika hapa ila ni kulalamika kila kukicha. Mtu mzima hovyooo!!!! Hiyo kampeni yako dhidi yangu ya kutaka kuwatetea mafisadi wenzako haitafika kokote mimi kucopy na paste kama kazi maana ni RUKHSA!!!! Sema lingine la maana kama huna ila kulalamika tu...basi KAA KIMYA.
 
Kuna kila sababu ya kuunda tume ya Wataalamu toka TRA na waangalie ni kuanzia lini Wabunge walikuwa hawalipi kodi na mapato yao toka wakati huo hadi hii leo ni kiasi gani. Halafu walipishwe kodi waliyokwepa kulipa tangu wakati huo hadi hii leo. Huu ni wizi wa mchana kweupe, wakati wa Tanzania wenye vipato ambavyo hafikii hata shilingi 100,000 kwa mwezi wanalipishwa kodi Wabunge wenye mishahara ya shilingi milioni 7 hawalipi hata senti tano katika kodi. Nina wasi wasi labda hata Rais na Marais wastaafu hawalipi kodi. Huu mfumo wa kuwabebesha Watanzania gharama kubwa za hawa viongozi usitishwe mara moja.
 
Bubu Kwa Kopy na Paste zako....Unaharibu Forums..unaona kama unajenga kumbe unaharibu. Hii mada tayari Mtanzania Kaiweka..wewe bila kuangalia unakuja weka. Unaona umejijengea Hati Miliki ya Kukopy na paste news za magazeti....

Nitaendelea kukuunyoosha...before kukopy na kupaste na kujifanya kubold..kuweka color na mistari..please angalia kwanza!!!!

Si wote wenye access na hayo magazeti unayozungumzia! Kwangu mimi anachokifanya B A K ni bora mara mia zaidi ya unachokifanya wewe. Kama umesoma habari hii kwa Mtanzania basi iruke tuachie sisi ambao hatujaisoma. Hamna kinachoharibika.

Bubu Ataka Kusema. Usivunjike moyo. Unatusaidia wengi.

Amandla.........
 
Waungwana,

Ahsante sana kwa kunipa support kuhusu 'kucopy and paste' zangu hapa jamvini. Inatia moyo kuna kwamba kumbe kuna baadhi yenu mnazippreciate hizi habari ninazotuma hapa nami nitaendelea kufanya hivyo mpaka hapo wenye ukumbi waamue vinginevyo kuhusiana na 'kucopy and paste'. Kwa mara nyngine tena ahsante sana.

Jumapili njema.
 
Mheshimiwa Slaa,

Usiishie kwenye mishahara ya wabunge tu bali iweke wazi mishahara ya viongozi wote wanaolipwa kutokana na bajeti ya serikali. Na wisho wa mwaka wote watueleze watumiaje hayo mamilioni. Kama wanapewa posho ya kuajiri dereva watueleze wamemwajiri nani na wanamlipa ngapi n.k. Maelezo yahusishe na kiasi cha kodi wanacholipa.

Amandla...........
 
Lakini hapa naona inazaliwa paradox nyingine... mara nyingi tumekuwa tukilalamika kuwa viongozi wanamiliki mali za thamani kubwa kuliko vipato vyao. Lakini hapa inaonyesha kuwa kumbe vipato vyao ni vikubwa sana. je, inaweza kuwa yale malalamiko ya wali hayana msingi sana?
 
Dr. Slaa mkuu nazidi kukupongeza kwa kila hoja unayowakilisha..Siwezi kutoa mfano wako na hakika kila siku unanigusa sana pale panapowakera wananchi!..
Hongera mkuu wangu tuko pamoja...
 
Back
Top Bottom