Dk. Slaa: JK ameliingiza taifa vitani

Status
Not open for further replies.

CHADEMA mnahusika sana matukio hayo, sasa ndiyo watu wanajua ni jinsi gani mlivyokuwa mkitetekeleza mauaji ili kuisingizia serikali na vyombo vyake, sasa mtakoma.
 
Siasa za fujo za hawa CHADEMA hazitapewa nafasi katika kisiwa chetu cha amani.
 
JK ,atajutia kauli yake hii, ngoja mtaona , haoni uhuru anasota huko The Hegue bila hata kutoa kauli tata kama hii ya kwake ? Ingekuwaje angel iwaki kutoa kauli yenye kuakisi kama hii?
 
bange zinapulizwa na lema pale kijenge mwanama, mara moja moja dr.slaa anamgongea lema pafu ndio mana slaa akili zimemruka

Huwezi ukahamasisha raia wako wadhuriane halafu ukajiona kuwa uko salama kichwani mwako.
 
Siasa za fujo za hawa CHADEMA hazitapewa nafasi katika kisiwa chetu cha amani.
Jk asifikiri kwa kauli hii yeye na CCM watakuwa salama, maana kuna vijana wengi sana ni machinga wanadhulimiwa ni suala la kuwaambia jibuni mapigo nchi I tazama hii,ajisahihishe huyu ...
 
Slaa ni mnafiki na ni mfitinishaji, mbona lema na mbowe walimfanyia vurugu aliyekuwa mwenyekiti cdm arusha mwaka jana lakini alinyamazia. Nyani kawaida hucheka ----- la mwenzie wakati yeye analo. Slaa akome kutuchonganisha wa tz kwa kupotosha kauli ya jk.
 
Mungu ameaamuwa kuwaumbua CCM kwa kuwaweka hadharani baada ya kuendesha mauaji kwa kificho na kudhuru watu kwa kificho.Mungu amechoka na vitendo vichafu vya maccm amemuwa kuwaumbua ili kila mtu ajue uchafu wanao ufanya gizani.
 
“Waswahili wanasema ukishangaa ya Musa utaona ya Firauni. Hivi karibuni tulishangaa kauli ya Pinda kutaka polisi wawapige tu wapinzani, leo rais naye anawataka CCM waache unyonge, wajibu mapigo. Hii ni hatari sana,” alisema Dk. Slaa.

Nikuulize mheshimiwa Slaa, je inawezekana kujibu mapigo ambayo hayapo? Basi mkitaka asiwepo wa kujibu mapigo, basi msianzishe hayo mapigo. Na akina CCM pia inawahusu, kama mkihimizana kujibu mapigo, mkumbuke pia wengine watakaa kwa tahadhari kujibu mapigo pia iwapo mtayaanzisha. Kwa hiyo mheshimiwa Slaa unaonywa usianzishe mapigo maana yatajibiwa, lakini pia nawe jiandae kujibu mapigo kama yataanzishwa maana sasa ruksa imetolewa ya kujibu mapigo. What is good for the goose is good for the gander.

Maana yake: asiwepo wa kuanzisha mapigo maana yatajibiwa pande zote. Tuache unyonge, wote kabisa.
 
Akili ya magamba ni ndogo sana, mnaacha kujadili jambo la msingi lililoigusa taifa mnaishia kupiga propaganda kuhusu Dr Slaa, hivi nyie vijana mmeweka akili wapi, mnafikiri utekelezaji wa kauli ya machafuko uliotolewa na Rais kikwete, nyie mtapona, jihadharini sana ndugu zangu, tunashabikia vitu vingine ambavyo havina msingi wowote, wametoa maoni watu wengi hapo, lakini inaonekana Dr Slaa anawauma sana, mtaipata fresh, hatutishwi na kauli za mwenyekiti wenu wa magamba, eti kisa yeye ni rais, sasa jaribuni kuleta ujinga muone, kupitia kura mmeshindwa, sasa mmeanza michezo isiyostahili, heri nife nikipigania haki, kuliko kuishi kwa manyanyaso na viisho kiasi hiki, hatutarudi nyuma kamwe, Mungu yu pamoja nasi, tuliishasema, ccm ndio wanaovuruga amani ya nchii hii.
 

Kama munaona mwenye kiti wenu yuko sahihi kwa kauli ya kuhamasisha raia wake wauane mshaurini akapambane na Kagame.Mbona Kagame kila siku ana mtusi lakini hamchukulii hatua zozote au amegundua kuwa Kagame ni maji marefu ana taka kuwaonea raia ambao wamekosa mtetezi ambae ana weza akawatetea?au mwenyekiti wenu ana ogopa ng'ombe na kuonea mbuzi?.
 
Huyu mkwer.e ni janga kwa kauli zake za ngomani kwenye taifa...Mungu tunusuru.
 
Mtaji mkubwa wa siasa za chadema ni vurugu na maandamano, sasa na nyie mkijibiwa kwa mbinu zenu mnaanza kulia lia, tunataka siasa za hoja na si vurugu, imefikia mahali chadema mkatambua kwamba hii nchi ni ya wote, na si chadema pekee wenye haki ya kuishi humu tanzania, na hakuna mahali popote ambapo haki inapatikana kwa vurugu, mara zote mazungumzo ndio njia sahihi, sasa mjifunze kuacha vurugu mkae tujadiliane kama taifa...
 
Siungi mkono alichosema Kikwete,ninalaani!ila nawaomba vyama upinzani waache vurugu tuone hao CCM,watamchokonoa nani

MKUU, iko hivi, kama ilivyo ngumu kukubali kunyang'anywa kitu ulichokizowea, ndivyo ilivyo kwa maccm. Hawana Haya wala Aibu, yatakufuata tu hata nyumbani kukuchokoza. Camp zao za Green guard wamejaza magaidi, ambao baadae ndio watakaokuja kuwa waasi.Walishawaambia wananchi wasiichague CHADEMA kwani wakifanya hivyo nchi itaingia vitani, cha kujiuliza nchi ingeingia vitani na nani?Nani angeanzisha vita?Kwa nini aanzishe vita?Je CHADEMA wangeweza kujianzishia vita na kujipiga wenyewe?CCM tumewachoka, angalieni KANU waliko, ndo kaburi lenu hilo, nao waliyafanya hayohayo wakati wakitawala, leo hii wako wapi?
 
kweli bwana
 

Mwenyekiti wenu ana ona ni bora aishi kwa amani na Kagame kuliko kuishi kwa amani na raia wake.
 
Watanzania tukatae uchochezi kutoka upande wowote hawa wote wanao sema haya wana faida na vurugu ndio mana wana shabikia na kuyakuza ili itoke vurugu au vita ambayo kwao ina weza kua na faida.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…