Kachanchabuseta
JF-Expert Member
- Mar 8, 2010
- 7,269
- 675
Monday, 13 September 2010
NA PETER KATULANDA, MWANZA
Mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA Dk. Willibrod Slaa, ameonyesha kuikubali CCM, baada ya kusifia baadhi ya mipango, ikiwemo ya ujenzi wa shule za msingi na sekondari.
Alitoa sifa hizo mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Mwanza, wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mirongo, wilayani Nyamagana. Dk. Slaa pia alipongeza juhudi za serikali ya CCM katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya barabara.
Aliifagilia Dira ya Maendeleo ya Taifa, Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (MKUKUTA) na Mpango wa Kurasimisha Mali za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), iliyotekelezwa chini ya usimamizi wa serikali ya CCM. Kwa mujibu wa Dk. Slaa, kwa kiwango kikubwa miradi hiyo imefanikiwa.
Katika mkutano huo, watu wengi walikwenda kuona helikopta, ambapo baada ya kuondoka walianza kutawanyika, huku mkutano wa Dk. Slaa ukiendelea. Hali kama hiyo pia ilijitokeza katika mkutano uliofanyika Septemba 10, mwaka huu, katika mikutano iliyofanya wilayani Kwimba.
Baadhi ya waliohudhuria mkutano huo walisema ahadi zake nyingi hazitekelezeki. Kama anafagilia kazi zilizofanywa ana maana anaikubali na kuifagilia CCM imefanya kazi nzuri, alisema mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Mustafa.
Alisema haoni jipya alilonalo Dk. Slaa, zaidi ya hotuba yake kujaa kashfa, badala ya kueleza sera za CHADEMA.
CHANZO: Gazeti la Uhuru
NA PETER KATULANDA, MWANZA
Mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA Dk. Willibrod Slaa, ameonyesha kuikubali CCM, baada ya kusifia baadhi ya mipango, ikiwemo ya ujenzi wa shule za msingi na sekondari.
Alitoa sifa hizo mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Mwanza, wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mirongo, wilayani Nyamagana. Dk. Slaa pia alipongeza juhudi za serikali ya CCM katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya barabara.
Aliifagilia Dira ya Maendeleo ya Taifa, Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (MKUKUTA) na Mpango wa Kurasimisha Mali za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), iliyotekelezwa chini ya usimamizi wa serikali ya CCM. Kwa mujibu wa Dk. Slaa, kwa kiwango kikubwa miradi hiyo imefanikiwa.
Katika mkutano huo, watu wengi walikwenda kuona helikopta, ambapo baada ya kuondoka walianza kutawanyika, huku mkutano wa Dk. Slaa ukiendelea. Hali kama hiyo pia ilijitokeza katika mkutano uliofanyika Septemba 10, mwaka huu, katika mikutano iliyofanya wilayani Kwimba.
Baadhi ya waliohudhuria mkutano huo walisema ahadi zake nyingi hazitekelezeki. Kama anafagilia kazi zilizofanywa ana maana anaikubali na kuifagilia CCM imefanya kazi nzuri, alisema mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Mustafa.
Alisema haoni jipya alilonalo Dk. Slaa, zaidi ya hotuba yake kujaa kashfa, badala ya kueleza sera za CHADEMA.
CHANZO: Gazeti la Uhuru