Dkt. Mwakyembe aandika waraka wa siri!

Huu ni ****** na uzandiki mwingine wa mafisadi kupitia gazeti "lao" hili. Kama waraka huo umesambazwa kwa ndugu na jamaa na wananchi vipi uwe siri ya kutouanika na kutotaja undani wa waraka huo. Mwenyewe katoa tamko lake kwa maandishi moja kwa moja kwa vyombo vya habari vyote ili visimung'unye maneno au kupindisha - vipi leo chombo hiki kijifanye kinajua zaidi ya wanavyojua wengi - acheni kufanya biashara au kucheza siasa kwa mgongo wa afya za watu.
 
"Vyanzo vyetu vya habari kutoka kwa ndugu na marafiki wa karibu wa Dk. Mwakyembe vilisema kuwa, naibu waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, amefikia hatua ya kuandika waraka huo kwa lengo la kutaka kuijulisha familia yake na taifa"

CDM=Tanzania Daima=Wazushi,waongo,Wanafiki
 
MwakyembeSema.jpg


Dk. Mwakyembe sasa aandika waraka wa siri

• AUSAMBAZA KWA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI ZAKE WA KARIBU
NAIBU Waziri wa Ujenzi anayeugua ugonjwa uliozusha utata mkubwa serikalini, Dk. Harrison Mwakyembe, ameandika waraka mahususi unaoeleza kile anachokiamini kuwa ni chanzo cha ugonjwa wake, Tanzania Daima Jumatano limebaini. Waraka huo ambao gazeti hili limeuona mbali ya kueleza kile ambacho Mwakyembe mwenyewe anaamini kuwa ni chanzo cha ugonjwa wake, unaeleza pia jinsi alivyoanza kuugua, watu anaowashuku kuwa nyuma ya mpango huo, siku na tarehe aliyodhani kuwa ndiyo aliyowekewa sumu hiyo.

Kama hiyo haitoshi, Mwakyembe katika waraka wake huo pasipo kueleza chanzo halisi cha undani wa taarifa zake, anaeleza mbinu iliyotumika kumdhuru na mahala mpango huo wa kumdhuru ulipopangwa. Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kwamba Dk. Mwakyembe ambaye kwa sasa yuko nchini India ameusambaza waraka huo kwa ndugu, jamaa na marafiki zake wa karibu. Katika waraka huo, Dk. Mwakyembe anaeleza kwamba anaamini alipewa sumu hiyo akiwa ofisini kwake huku akitaja majina ya watu anaowatuhumu kuwa nyuma ya mpango huo ambao gazeti hili kwa sasa linahifadhi majina yao.


Kwa mujibu wa Dk. Mwakyembe, mara tu baada ya kuwekewa sumu hiyo alianza kuwashwa mwili kabla ya hali kuendelea kuzorota na kuwa mbaya. Akionekana kujibu hoja za Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, mwanasiasa huyo katika waraka wake anaeleza kwamba hakuwekewa sumu hiyo kwenye chakula, bali kwenye sabuni na kitaulo cha kujifutia, ambacho huwekwa kwenye chumba maalumu ofisini kwake kwa ajili ya kusafisha mikono na huduma nyingine awapo ofisini.


Vyanzo vyetu vya habari kutoka kwa ndugu na marafiki wa karibu wa Dk. Mwakyembe vilisema kuwa, naibu waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, amefikia hatua ya kuandika waraka huo kwa lengo la kutaka kuijulisha familia yake na taifa kile anachoamini anakabiliana nacho endapo atapoteza maisha kabla ya ukweli kamili kubainishwa. Hata hivyo, kutokana na ukweli kwamba suala hilo la afya ya Dk. Mwakyembe liko katika hatua za uchunguzi, Tanzania Daima Jumatano haliwezi kuandika kwa undani kuhusu waraka huo kwa sasa.


Ukiacha hilo, Dk. Mwakyembe katika waraka huo ameelezea historia ya maisha yake kisiasa na mikasa iliyompata kiasi cha kujijengea maadui.
Ameeleza jinsi alivyonusurika kuuawa mara kadhaa na kwamba taarifa zote za mikasa yake aliziripoti polisi, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa na Jeshi hilo la Polisi.

Baadhi ya mikasa aliyoitaja kwenye waraka huo ni pamoja na tukio la kunusurika kuuawa kwenye ajali ya gari iliyotokea Mei 21, mwaka 2009. Ajali hiyo ilitokea eneo la Ihemi, kilomita 40 kutoka Iringa mjini akiwa safarini kutokea Mbeya kwenda Dar es Salaam. Kwa mujibu wa waraka huo, gari alilokuwa akisafiria aina ya Toyota Land Cruiser T 362 ACH, liliacha njia saa moja asubuhi baada ya kukanyaga shimo na tairi ya upande wa kulia kuchomoka na dereva wake, Joseph Msuya (30), kupoteza mwelekeo kabla ya gari hilo kutoka nje ya barabara upande wa kushoto na kuparamia mti kisha kupinduka.


Ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa Dk. Mwakyembe akijaribu kulipita lori kabla ya kukanyaga shimo hilo. Anasema katika ajali hiyo aliokolewa na wasamaria wema pamoja na trafiki wawili waliokuwa kwenye basi dogo waliokuwa wakisafiri kutoka Iringa kwenda Njombe. Anasema katika waraka huo kuwa, baada ya ajali hiyo alilazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa kutokana na kuumia taya kisha alihamishiwa Dar es Salaam kwa matibabu zaidi. Kwa mujibu wa waraka huo, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema, aliunda tume iliyoongozwa na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani wakati huo, Kamanda James Kombe, kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.


Matokeo yalionesha kwamba ilisababishwa na uzembe wa dereva wake, Msuya wakati Dk. Mwakyembe akiamini kwamba ajali hiyo ilipangwa.
Februari 9, mwaka 2011, Dk. Mwakyembe aliandika barua kwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema, akimpa taarifa juu ya kuwapo kwa njama za kutaka kumuua yeye pamoja na viongozi wengine.

Wengine aliowataja katika barua hiyo ni pamoja na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela. Katika orodha hiyo ya Mwakyembe kwa IGP, hadi sasa kiongozi mwingine ambaye anaumwa ni Profesa Mark Mwandosya.

Waandishi wa Habari wa Tanzania na Wahariri wao ni wa kuwahurumia. Eti ni waraka wa siri; tena wanoa ndugu zake; tena gazeti linao; Sasa kuna siri tena hapo? Au ni majungu ya kuuzia magazeti?

Kwa suala la ajali ya Ihemi Iringa; Si kweli kwamba alipangiwa Lorry kwa sababu hizi hapa; Na kama uchunguzi wa Polisi kwamba ajali ile ni Uzembe wa Dereva, basi JF iandae wachunguzi binafsi wakafanye hata practice kuona kama kuna njama ilikuwepo.
1. Tanzania tunaendesha magari upande wa kushoto wa barabara (Left side of road driving);
2. magari yetu (na hata la Mwakyembe) ni Right hand driving (yaani Usukani upo Kulia mwa gari)
3. Ukitaka kulipita gari (kama siyo double ways kama barabara nyingi za Dar) lazima ulipite upande wake wa kushoto
Hivyo basi
1a. Kwa shimo aliloliingia dereva wa Mwakyembe pale Ihemi (kilomita 40 kutoka Iringa Mjini) lilikuwa upande wa kushoto (ukingoni) wa barabara (Ukitokea Mbeya) na kulia (ukingoni) wa barabara kama unatoka Iringa.
1b. Lile shimo lilikuwa pale kwa muda mrefu zaidi ya miezi minne (nililifahamu sababu nilikuwa na trip nyingi za maeneo ya Ifunda/Ihemi nikiendesha gari yangu
1c. Dereva wa Mwakyembe ni mzoefu na ile barabara kwa sababu amepita njia hiyo kwa muda mrefu hivyo alifahamu kama kabla ya kumaliza mteremko kuna shimo (tena kubwa kabisa siyo la kitoto)
1d. kama alitaka kulipita lorry kwa upande wa kushoto, huo ndo uzembe Klass 1.

2a. Mwakyembe alitoka Kyela jana yake jioni na kulala makambako kwa sababu walikuwa wamechelewa
2b. kwa kulala makambako walichoka na Hivyo mapema asubuhi walipoanza safari; mwakyembe alilala usingizi hadi wanapofika Ihemi (kilomita 120 kutoka Makambao)
2c. Dereva kwa uzembe naye alikuwa amelala (amesinzia) (hapa asitudanganye) kwa uchovu

3a. Ajali ingekuwa aligonga Lorry kwa nyuma ningekubali kwamba mwenye lorry alimtegeshe';
3b. Lorry kutosimama si hoja maana kuna ajali ngapi zinatokea na wengine wanaendelea na safari; watu wanaogopa kuuziwa kesi kama hii jamaa wa lorry angesimama basi angeuziwa kesi mbaya
3c. Askari waliomwokoa ndio waliotoa taarifa ya uchunguzi wa chanzo cha ajali kwa hiyo Mwakyembe hawezi kuwasifia kwa kumwokoa then akakataa taarifa ya uchunguzi wao wa ajali maana hawakuwa wanakwenda Njombe bali kwenye kituo chao cha kazi (barabarani) mara nyingi husimama Ifunda karibu na shule ya Sekondari.

Maswali ya kujiuliza
1. kama dereva alikuwa Oka na Mwakyembe mwenyewe; kwa nini hawakusoma namba ya usajili ya Lorry
2. Kwa nini basi hata wasikumbuke tu Lorry lilkuwa na rangi gani?
3. Kwa nini dereva wa Mwakyembe atake kulipita Lorry mteremkoni wakati sheria za usalama haziruhusu kupita gari katika mteremko mkali kama ule wa Ihemi?

Mhariri wa gazeti na waandishi wake wote hawana maana hata kidogo maana wameconcentrate kuleta historia ya ajali ya zamani badala ya kujuza walichodhani wangesema. huu ni Ujinga na umbumbumbu.

Kupewa sumu kwa Mwakyembe; Kwa vile anasema haikuwekwa kwenye chakula basi na kwa kuwa aliwekewa kwenye sabuni na kitambaa maalum cha kunawia kwenye chumba maalum ofisini kwake; Maana yake ni kuwa
1. Mhudumu wa ofisini kwake ndiye mhusika mkuu
2. Yule mtu wake aliyemwamini kuwa atamsaidia ofisini kwake (maana hana imani na wengine) ndiye aliyemwekea sumu
3. Kama hivyo vitu anatoka navyo nyumbani kwake maana ofisini kwake hawaamini; basi watu wa nyumbani kwake aliowaandikia huo wosia ndio waliomwekea sumu.

Pole Mwakyembe; lakini tunahitaji ukweli wa haya matukio kuliko kutumia matukio haya kujenga chuki. tunajua Mafia wapo lakini kwa nini iwe kwa kiasi cha chuki kujengwa hivi?
 
[B said:
falesy[/B];3368485]Waandishi wa Habari wa Tanzania na Wahariri wao ni wa kuwahurumia. Eti ni waraka wa siri; tena wanoa ndugu zake; tena gazeti linao; Sasa kuna siri tena hapo? Au ni majungu ya kuuzia magazeti?

Kwa suala la ajali ya Ihemi Iringa; Si kweli kwamba alipangiwa Lorry kwa sababu hizi hapa; Na kama uchunguzi wa Polisi kwamba ajali ile ni Uzembe wa Dereva, basi JF iandae wachunguzi binafsi wakafanye hata practice kuona kama kuna njama ilikuwepo.
1. Tanzania tunaendesha magari upande wa kushoto wa barabara (Left side of road driving);
2. magari yetu (na hata la Mwakyembe) ni Right hand driving (yaani Usukani upo Kulia mwa gari)
3. Ukitaka kulipita gari (kama siyo double ways kama barabara nyingi za Dar) lazima ulipite upande wake wa kushoto
Hivyo basi
1a. Kwa shimo aliloliingia dereva wa Mwakyembe pale Ihemi (kilomita 40 kutoka Iringa Mjini) lilikuwa upande wa kushoto (ukingoni) wa barabara (Ukitokea Mbeya) na kulia (ukingoni) wa barabara kama unatoka Iringa.
1b. Lile shimo lilikuwa pale kwa muda mrefu zaidi ya miezi minne (nililifahamu sababu nilikuwa na trip nyingi za maeneo ya Ifunda/Ihemi nikiendesha gari yangu
1c. Dereva wa Mwakyembe ni mzoefu na ile barabara kwa sababu amepita njia hiyo kwa muda mrefu hivyo alifahamu kama kabla ya kumaliza mteremko kuna shimo (tena kubwa kabisa siyo la kitoto)
1d. kama alitaka kulipita lorry kwa upande wa kushoto, huo ndo uzembe Klass 1.

2a. Mwakyembe alitoka Kyela jana yake jioni na kulala makambako kwa sababu walikuwa wamechelewa
2b. kwa kulala makambako walichoka na Hivyo mapema asubuhi walipoanza safari; mwakyembe alilala usingizi hadi wanapofika Ihemi (kilomita 120 kutoka Makambao)
2c. Dereva kwa uzembe naye alikuwa amelala (amesinzia) (hapa asitudanganye) kwa uchovu

3a. Ajali ingekuwa aligonga Lorry kwa nyuma ningekubali kwamba mwenye lorry alimtegeshe';
3b. Lorry kutosimama si hoja maana kuna ajali ngapi zinatokea na wengine wanaendelea na safari; watu wanaogopa kuuziwa kesi kama hii jamaa wa lorry angesimama basi angeuziwa kesi mbaya
3c. Askari waliomwokoa ndio waliotoa taarifa ya uchunguzi wa chanzo cha ajali kwa hiyo Mwakyembe hawezi kuwasifia kwa kumwokoa then akakataa taarifa ya uchunguzi wao wa ajali maana hawakuwa wanakwenda Njombe bali kwenye kituo chao cha kazi (barabarani) mara nyingi husimama Ifunda karibu na shule ya Sekondari.

Maswali ya kujiuliza
1. kama dereva alikuwa Oka na Mwakyembe mwenyewe; kwa nini hawakusoma namba ya usajili ya Lorry
2. Kwa nini basi hata wasikumbuke tu Lorry lilkuwa na rangi gani?
3. Kwa nini dereva wa Mwakyembe atake kulipita Lorry mteremkoni wakati sheria za usalama haziruhusu kupita gari katika mteremko mkali kama ule wa Ihemi?

Mhariri wa gazeti na waandishi wake wote hawana maana hata kidogo maana wameconcentrate kuleta historia ya ajali ya zamani badala ya kujuza walichodhani wangesema. huu ni Ujinga na umbumbumbu.

Kupewa sumu kwa Mwakyembe; Kwa vile anasema haikuwekwa kwenye chakula basi na kwa kuwa aliwekewa kwenye sabuni na kitambaa maalum cha kunawia kwenye chumba maalum ofisini kwake; Maana yake ni kuwa
1. Mhudumu wa ofisini kwake ndiye mhusika mkuu
2. Yule mtu wake aliyemwamini kuwa atamsaidia ofisini kwake (maana hana imani na wengine) ndiye aliyemwekea sumu
3. Kama hivyo vitu anatoka navyo nyumbani kwake maana ofisini kwake hawaamini; basi watu wa nyumbani kwake aliowaandikia huo wosia ndio waliomwekea sumu.

Pole Mwakyembe; lakini tunahitaji ukweli wa haya matukio kuliko kutumia matukio haya kujenga chuki. tunajua Mafia wapo lakini kwa nini iwe kwa kiasi cha chuki kujengwa hivi?

Hii report imekaa kama ile ya polisi waliyowahi kutoa.

Hapo kwenye BOLD inaelekea wewe ndiye Feleshi Mwenyewe yule DPP wetu, Karibu JF Afande!
 
3. Ukitaka kulipita gari (kama siyo double ways kama barabara nyingi za Dar) lazima ulipite upande wake wa kushoto
fafanua zaidi hapo..
 
Yani unataka ripoti ya ugonjwa wa Mwakyembe iwe hewani? Halafu ikishakuwa hewani wewe itakusaidia nini? Kikubwa unachotakiwa kujua ni kuwa AMEWEKEWA SUMU

Kama hataki ripoti ya ugonjwa wake ifahamike, basi akae kimya hakuna haja ya kupiga kelele kuwa amepewa sumu. Asubiri kifo tu kama wanavyokufa ndugu zetu wengine bila hata kufika India.
 
Every soul will taste death! (Quran 3:185)

Beware of those ho would do anaything to live forever.
 
"Vyanzo vyetu vya habari kutoka kwa ndugu na marafiki wa karibu wa Dk. Mwakyembe vilisema kuwa, naibu waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, amefikia hatua ya kuandika waraka huo kwa lengo la kutaka kuijulisha familia yake na taifa"

CDM=Tanzania Daima=Wazushi,waongo,Wanafiki

Gazet la Uhuru je?
 
"Vyanzo vyetu vya habari kutoka kwa ndugu na marafiki wa karibu wa Dk. Mwakyembe vilisema kuwa, naibu waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, amefikia hatua ya kuandika waraka huo kwa lengo la kutaka kuijulisha familia yake na taifa"


CDM=Tanzania Daima=Wazushi,waongo,Wanafiki



kama ni kujulisha Taifa mbona unawekwa kama siri wakati kasema ni kulijulisha Taifa? nadhani ni swala la kuwekwa hadharani kwani alishatoa ruksa kuwa lengo ni familia na taifa kupata habari

uongozi wa jf mpooooooooooooooooooooooooooooooozi
 
sijawahi kusikia moja kati ya dalili za ngoma ni ngozi kupukutika..get your facts right mkuu...basi hiyo ni aina mpya ya ukimwi

Ndugu yAngu wewe umekariri lazima ngwengwe ufe kwA madonda,au homa tuu.HatA MAfuaaaa yanakuapelekA kAmaa unayo,ni kwambA uakipAtA ugonjwA wowote na if hamnA defence mechAnism mwilini unakwendA nA maji.

Mimi nimekudokezA tuu,ilA kamA unAbishA AyA subiri.Time will tell mkuu
 
Tanzania Daima wanataka ukweli ufahamike. Ngoja tusubiri majibu ya Mwakyembe kama kweli kauandika waraka huo na yaliyomo. Tatizo haeleweki. Akinyamaza tunadhani karidhia? Kamjibu Manumba. Atasema angalau neno moja kuhusu waraka huu.
 
Ingawa siamini kwamba Dr. Mwakyembe ana UKIMWI but to put things in right persepective UKIMWI sio UGONJWA UKIMWI = Ukosefu wa KInga MWIlini (Acquired Immuno Decificient Syndrome = AIDS). Hivyo ukiwa na UKIMWI unaweza kuugua ugonjwa wowote ule including ugonjwa wa ngozi na dalili zake zinategemea na ugonjwa uliougua inaweza pia dalili ikawa ngozi kupukutika!

Tuendelee kutafakari

Endelea kumueliamisha NyAbhingi,maAnA ye kakAriri kuA ukimwi ampaakaA utoke mApele au kifuAa bAsi ndo unA ukimwi nA ndo itakAyokuonadoa..Hatabui kua ukimwi unakujA kwA dizaini nyingi,kama unao hata tumbo likikukamata unaondoka.Mi nimempA dokezo sasa kazi kwake kutAfiti
 
Ndugu yAngu wewe umekariri lazima ngwengwe ufe kwA madonda,au homa tuu.HatA MAfuaaaa yanakuapelekA kAmaa unayo,ni kwambA uakipAtA ugonjwA wowote na if hamnA defence mechAnism mwilini unakwendA nA maji.

Mimi nimekudokezA tuu,ilA kamA unAbishA AyA subiri.Time will tell mkuu
Wahindi wa Appollo hawajaligundua hili? Wanahangaikia nini sasa au ni biashara tu kwa kwenda mbele?
 
Back
Top Bottom