Dk. Kitila Mkumbo hajasoma vema Katiba ya CHADEMA...

Dk. Kitila Mkumbo hajasoma vema Katiba ya CHADEMA...

Nimeamini weak minds discuss other people instead of great ideas. Sikutegemea daktari kuanza kuteswa na nafsi changa za vijana waroho wa madaraka. Sisi laymen tulitegemea watu kama maprof ndo wachore msitari kuwa apa ndipo,apa sipo ila na wao wamenasa ktk wavu wa kuanza kuteswa na wanasiasa uchwara wabinafsi. Sitakaa nikubaliane na siasa izi za kipuuzi,zisizofuata mfumo wowote. Na nyie wanakamati mnaokimbilia kwenye makala mnakosa umaarufu mnaoutaka! Aya chadema shambulianeni mkimaliza mtupe taarifa mmekubaliana au mmekubaliana kutokubaliana. Pole kwa wote mliokuzwa na buzwagi mkadhan mmefika juu kuliko juu zote! Rais ajaye tutamchagua sisi wala si nyie chadema au ccm japokuwa vyama ivi viwili ndo vitatupa rais ,awe anatosha au dhaifu ila atatoka umo umo. Aya umana kwanza!
 
Dr.Kitila mbona aliumbuliwa juzi na mwanafunzi wake wa mwaka wa kwanza kwamba wote ni wavivu wa kuandika na wakiandika wanatoa vitu vya juujuu tu kama hiyo makala yake , sasa naanza kuamini yule jamaa aliyechangia mada ni bora kuliko walimu wake.Pole dr.kilila rudi ktk mstari

NAFIKIRI WENGI hammfahamu huyu kitila ila mtakuja mfahamu muda si mrefu...wale waliosoma mlimani kipindi alipokuwa kiongozi wa wanachuo wanafahamu tabia zake za double dealing...ila kwa sasa tuanatarajia achukue kiti kile cha mwigulu pale singida...tujitahidi kumuweka sawa aongeze majimbo,ila kwa uongozi ndani ya sekretariati ya chama hafai. ana tabia za unafiki uliopiptiliza
 
DR Kitila
Kutokea kwenye post yako ambayo si sehemu ya chapisho la kwenye raia mwema.

Nakubaliana na wewe juu ya hoja ya kuchochea Fikra huru, lakini lazima kuwe na utaratibu basi, ama sivyo inakuwa ni Fujo. Nikigusia swala la Zitto kidogo, mpaka sasa hakuna shaka kwamba angalau si CHADEMA wala CCM mwenye uhakika wa kuibuka mshindi mwaka 2015, na mpaka sasa hakuna mwenye uhakika ni nini kitakua kigezo cha ushindi mwaka 2015 kati ya ushawishi wa mgombea au ushawishi wa CHAMA.

Lakini mpaka sasa inaeleweka kwamba CCM imekuwa ikishinda chaguzi nyingi kutokana na jina lake zaidi kulinganisha na nguvu ya ushawishi ya wagombea wake, mategemeo yetu ni kuona viongozi wa chadema wanaelekeza nguvu zao zote kwenye kukijenga chama chao. inapotokea mtu kama ZITTO anatangaza mawazo yake ya kutaka urais katikati ya mchakato kama huu inalazimisha kuhoji "what kind of character is this?". Mtake msitake, kuzipachika sifa ya fikra huru tabia kama hizi ni sawa sawa na kuwafundisha watoto kumuinterapt mzazi au mtu mzima anapokuwa akiongea.

Ndio maana ya kuwa na kanuni,taratibu, sheria, miongozo na viongozi, ili tuweze kuendesha mambo yetu kwa utaratibu na staha ama sivyo hata kama mtu atajamba wakati watu tunakula pia liwe ni jambo lisilostahili kuuliza, NANI HUYO???
 
NAFIKIRI WENGI hammfahamu huyu kitila ila mtakuja mfahamu muda si mrefu...wale waliosoma mlimani kipindi alipokuwa kiongozi wa wanachuo wanafahamu tabia zake za double dealing...ila kwa sasa tuanatarajia achukue kiti kile cha mwigulu pale singida...tujitahidi kumuweka sawa aongeze majimbo,ila kwa uongozi ndani ya sekretariati ya chama hafai. ana tabia za unafiki uliopiptiliza

Sidhani kama ni mnafiki.
 
Nimeamini weak minds discuss other people instead of great ideas. Sikutegemea daktari kuanza kuteswa na nafsi changa za vijana waroho wa madaraka. Sisi laymen tulitegemea watu kama maprof ndo wachore msitari kuwa apa ndipo,apa sipo ila na wao wamenasa ktk wavu wa kuanza kuteswa na wanasiasa uchwara wabinafsi. Sitakaa nikubaliane na siasa izi za kipuuzi,zisizofuata mfumo wowote. Na nyie wanakamati mnaokimbilia kwenye makala mnakosa umaarufu mnaoutaka! Aya chadema shambulianeni mkimaliza mtupe taarifa mmekubaliana au mmekubaliana kutokubaliana. Pole kwa wote mliokuzwa na buzwagi mkadhan mmefika juu kuliko juu zote! Rais ajaye tutamchagua sisi wala si nyie chadema au ccm japokuwa vyama ivi viwili ndo vitatupa rais ,awe anatosha au dhaifu ila atatoka umo umo. Aya umana kwanza!

Kama haukuwahi kuwachunguza, walimu wengi isipokuwa mmoja wao Nyerere ni watu waoga sana kuvuka mstari, wako very theoretical. Ukimpata mwalimu anayesema "kuna njia nyingi sana za kwenda mjini lakini tutumie njia hii" na kila siku akatumia njia hiyo. Niite nimuone.
 
HASWA!!!
kama vile uko akilini mwangu.
Mie huwa nikikutana na wanachama hawa au wakereketwa mara zote nawaambia, Wajitambue kuwa sasa maneno yao ya kienyeji bila mpangilio ndio kifo chao,
Watofautishe wakereketwa na wanachama, offcourse na critics wa ukweli.
Hawa wasemaji please waweze kufikia kiwango/ level ya utambuzi ya wantanzania, sasa wanaongea kwa level ya chini mno.

Ni kweli Wanazania tunataka mabadiliko, ila wengi bado tunahitaji mtu wa wa kuaminika kifikra kutupeleka huko, lazima aongee tumsikie

Kila mmoja CDM ni mjuaji ajabu!!

Asante kwa kuliweka hili
Chama kina nia nzuri, kina viongozi wazuri tu, halafu wengi, lakini sasa, hakuna control, hakuna utaratibu,
Hatuoni filosofia ya chama ikikiongoza,
tunaona magumzo, kama vile kimechanganyikiwa kwa mafanikio madogo,

Inabidi wale wanaoitwa THINK TANKS wao wakae wajue namna ya kucontain hii confusion

Napenda kudediketi ujumbe huu kwa zitto kabwe na dr kitila mkumbo wote wakiwa dar es salaa.
 
Sidhani kama ni mnafiki.


ndugu... wengi wetu huwa ni vigumu kubadilika hulka au tabia zetu...fundamental character which defines us lies deep inside us and once u get few mins to have a deep reflections of yourself and close friends around you then wiill be in position to realise that. niliposema jamaa ni mnafiki sio jambo baya ni tabia yake tu na unajua unafiki una sehemu ya msaada katika jamii yetu. tungekuwa na jamii yote au viongozi wote ni wawazi wapo very transparent ,pasingekalika.

wengi tuna sehemu/percent fulani ya unafiki lakini sio sehemu kubwa ya matendo yetu.

jiangalie na utaliona hilo...sehemu za kazi , mitaani na maeneo mengi.

makala ya kitila inaonyesha hilo najaribu kuwa balanced ktk wale wanaomuunga mkono zitto na wanaomshutumu lakini ndani zaidi utafahamu linajichomoza suala la yeye kutoweka wapi msimamo wake halisi...mnafiki huwa hana msimamo wa dhati ,huwa anajaribu kupendezesha kila upande.
na unafiki mwingine nikkukumbushe pale alipotoa makala kwenye raia mwema inayoelezea msuguano kati ya mkiti na makamu mkti wa bavicha...alitoa makala isiyo na umuhimu wakati yeye ana nafasi ya kutoa ushauri ule ndani ya vikao vya chama. sasa kwanini akaanika wakati ule ushauri wake kwenye makala ya gazeti?

jenerali ulimwengu aliwahi kuandika siku za nyuma kuwa wengi wa rafiki zake wakikutana na kubalishana mawazo,alikuta hata kama wamepoteana miaka 10,20,30 tangu enzi za shule au kazi...wengi hulka na tabia zao ni zile zile....watabadilika tu kwa ongezeko la mwwili au ndevu au mvi lakini tabia za ndani nyingi ni zile zile...kama mtu ni introvert/extrovert/hypocrite/transparent/mean/sadist ataendelea kuwa vile vile.


nikupe mfano zaidi...kuelekea uchaguzi wa mwaka 2005...Ben R Mtobwa aliaandika kitabu fulani hivi kuhusu J.K

akatoa hadithi kidogo za J.K za kule msoga....akamnukuu mzee mmoja wa kijiijjini pale akisimulia jinsi ambavyo wakati ule JK akiwa mtoto katika michezo ya kuwinda porini ,ukigombana naye hata kama itapita wiki au muda kadhaa, atakutafuta na kurevenge. ama kama ulimpiga,atakupiga pia. mfano huu kwanini aliutoa? labda hakushtuka kama sio kitu kizuri cha kuandika lakini aliandika kwa sababu aliona it is worthy of story sababu watoto kawaida wakigombana baada ya masaa au siku moja hilo linapita au linasahaulika ...lakini si kwa mtoto JK ,,,NDIO MAANA akaona hio ni stori.

sitaki nikuulize swali kuwa JK katika utu uzima wake amebadilika.

have a reflection.
 
ASALAMU WANA JF. Napenda kuchukuwa nafasi hii kumfahamisha dk.kitila mkumbo kuhusu taarifa yake aliyo itoa ktk gazeti la raia mwema ktk hoja yake kuwa kutangaza niya mapema mwana chama wa chadema hakuna makosa tena sio uvunjaji wa katba ya chama.

Katka hili Dk. Mkumbo hayupo sahihi ukweli ni kwamba katba ya chadema imeelezea utaratibu wa uchaguzi na mamlaka ya kutangaza ratiba ya uchaguzi ndani ya chama tena imeweka wazi kikao chenye mamlaka ya kupanga kutangaza ratiba ya uchaguzi ndani ya chama uwe ni uchaguzi wa viongozi wa chama au wawa kirishi wa chama ktk serikali hivyo mwanachama tena ni kiongozi yeyote akijitangaza kugombea wakati kikao chenye mamlaka hakija toa tangazo la uchaguzi ni kinyume cha katba ya chadema pia ni kukiuka maadili ya chama mimi nawashauri kwanza someni katba kwa utulivu someni kazi za baraza kuu na kazi za kamati kuu.

Ndio sasa mtowe ushauri sipo kwa marumbano ila natekeleza wajibu wa katba ya chadema. Pia katba inapatikana ktk www.chadema.com. nawasilisha

Kutoa tangazo la kugombea ni tofauti na kutangaza nia mkuu usitake kutuburuza humu JF. ZITTO na wengine ndani ya CDM wametangaza nia ya kugombea lakini hawajabisha hodi katika ofisi za CDM zinazohusika na utoaji wa fomu za kugombea.
 
Napenda kudediketi ujumbe huu kwa zitto kabwe na dr kitila mkumbo wote wakiwa dar es salaa.

Mkumbo na ZITTO wako sawa kabisa, hawajapiga hodi popote kuchukua fomu unahangaikaje na mtu wa aina hiyo.
 
Nadhani Dr anaweza eleweka tofauti lakini katiba haijaonyesha muda wa kutangaza nia. Katika sura ya 6.3.1. utaona maelezo ya jumla wa jinsi ya kupata viongozi.

Hivyo, kutangaza nia sio kosa kwa sababu mwisho ni utaratibu wa kichama utachukuliwa. Kumbuka huwezi kuomba kugombea bila kufanya nia.

Kama kuna makosa basi marekebisho ya katiba kwa baadaye izingatie hili.

Kutangaza nia si kosa kufuatana na katiba. Mtoa mada ameshindwa kutofautisha kati ya KUTANGAZA NIA na KAMATI KUU KUKAA KUPITISHA WAGOMBEA.
 
why is this an issue in the first place??
I hate myself for keeping coming to this irrelevant issue

kwenye mdahalo jpili kna mwanafunzi wa mwaka wa kwanza aliwasema kwa jazba sana walimu wake kuwa hawaandiki makala.

Mimi nadhani wanaandika, na pia wanandika magazetini makala kama hizi.

Kama nyimbo za bongo fleva zinavyokosa depth, ndio na maandishi ya wahadhiri pia nayakuwa hivyo hivyo, ni jamii nzima inaelekea huko

udhaifu

- utoaji elimu, afya, maamuzi, utekelezaji, nk

God bless us

Kuna namna Jenerali Ulimwengu alisema hapo nyuma wakati wa kujadili namna wanavyopendekeza mchakato wa kutafuta katiba mpya uwe, sikumbuki maneno, ila ni kama vile mahali pa kutokea ni padogo sana, kama vile tumeshanaswa.
 
why is this an issue in the first place??
I hate myself for keeping coming to this irrelevant issue

kwenye mdahalo jpili kna mwanafunzi wa mwaka wa kwanza aliwasema kwa jazba sana walimu wake kuwa hawaandiki makala.

Mimi nadhani wanaandika, na pia wanandika magazetini makala kama hizi.

Kama nyimbo za bongo fleva zinavyokosa depth, ndio na maandishi ya wahadhiri pia nayakuwa hivyo hivyo, ni jamii nzima inaelekea huko

udhaifu

- utoaji elimu, afya, maamuzi, utekelezaji, nk

God bless us

Kuna namna Jenerali Ulimwengu alisema hapo nyuma wakati wa kujadili namna wanavyopendekeza mchakato wa kutafuta katiba mpya uwe, sikumbuki maneno, ila ni kama vile mahali pa kutokea ni padogo sana, kama vile tumeshanaswa.

Unamaanisha nini "... Mahali pa kutokea ni padogo sana, kama vile tumeshanaswa." ???
 
..........hebu tuonyesheni vipengele vya katiba vinasemaje...........
 
Unamaanisha nini "... Mahali pa kutokea ni padogo sana, kama vile tumeshanaswa." ???


Sikumbuki alitumia maneno gani, alitumia very strong words!
Ila imestick akilini mwangu hadi leo.
Kuwa ethics hakuna kwa mtu yoyote hapa TZ, nani yuko radhi kwa level hii ya ethichs tuliofikia kuweka sheria/ mikakati/ katiba ya kumbana, Lazima tu tutajiwekea loopholes za kila mtu binafsi kuendeleza utaratibu huu wa kurelax,

Nikiandika na kusoma naona nimeishusha hadhi ile comment yake,
Tunaweza kweli kuwa tena moral beings?
mie hata sioni tena,

LakiManake inabidi personal overhaul ya mtu binafsi, ambayo sijui nani yuko tayari seriously kuiTEKELEZA.
offcourse tunataka kila mtu abadilike.
 
Sikumbuki alitumia maneno gani, alitumia very strong words!
Ila imestick akilini mwangu hadi leo.
Kuwa ethics hakuna kwa mtu yoyote hapa TZ, nani yuko radhi kwa level hii ya ethichs tuliofikia kuweka sheria/ mikakati/ katiba ya kumbana, Lazima tu tutajiwekea loopholes za kila mtu binafsi kuendeleza utaratibu huu wa kurelax,

Nikiandika na kusoma naona nimeishusha hadhi ile comment yake,
Tunaweza kweli kuwa tena moral beings?
mie hata sioni tena,

LakiManake inabidi personal overhaul ya mtu binafsi, ambayo sijui nani yuko tayari seriously kuiTEKELEZA.
offcourse tunataka kila mtu abadilike.

Inaonekana amekata tamaa vibaya sana. Nakushauri uwe una msikiliza kwa makini sana huyu Jamaa sababu na yeye ni mmoja ya watu ambao wamekwishakupata fursa ya uongozi kwenye taifa letu sasa kwa nini hatumkumbuki angalau kama sokoine sielewi, labda sababu hajafa.

Kimsingi Haika naona kama unafanya makosa makubwa sana kukubaliana na maelezo ya huyu Jamaa. nahisi kama anatutukana au ni kweli huyu jamaa sio mtanzania.
 
Inaonekana amekata tamaa vibaya sana. Nakushauri uwe una msikiliza kwa makini sana huyu Jamaa sababu na yeye ni mmoja ya watu ambao wamekwishakupata fursa ya uongozi kwenye taifa letu sasa kwa nini hatumkumbuki angalau kama sokoine sielewi, labda sababu hajafa.

Kimsingi Haika naona kama unafanya makosa makubwa sana kukubaliana na maelezo ya huyu Jamaa. nahisi kama anatutukana au ni kweli huyu jamaa sio mtanzania.

no umenipata vibaya,
take it as a challenge when ur making decisions,
usijipendelee on issues which ur weak.
Just stand strong and and make GREAT decisions.
And be ready to change to fit them
Do not make soft decisions ambazo wewe ndo unadhani utaziweza, challenge your self to be better!!
Though it will hurt you (PAIN!) are you ready?
Mfano kazi ulio nayo, rushwa ndogondogo, elimu na vyeti vyetu, hospitali, usawa?? kufanya kazi kwa juhudi kwa faida ya TAIFA, nk
 
unaporuhusu kila mtu atangaze nia kwa sasa unatoa nafasi kwa watu kuanza kujijenga binafs ndani ya chama ili aweze kuteuliwa na chama badala ya kukijenga chama nje hivyo nguvu kubwa inatumika kujijenga ainafsi
 
Nadhani Dr anaweza eleweka tofauti lakini katiba haijaonyesha muda wa kutangaza nia. Katika sura ya 6.3.1. utaona maelezo ya jumla wa jinsi ya kupata viongozi.

Hivyo, kutangaza nia sio kosa kwa sababu mwisho ni utaratibu wa kichama utachukuliwa. Kumbuka huwezi kuomba kugombea bila kufanya nia.

Kama kuna makosa basi marekebisho ya katiba kwa baadaye izingatie hili.

Sio kila kitu kinakuwa kwenye katiba...kwa mfano katiba ya nchi haioneshi muda mwafaka wa binti kupata ujauzito, lakini hii haizui watu kumshangaa na hata kumlaumu binti kupata ujauzito kwa wakati usio muafaka. Wakati mwingine kuna mambo yanayotakiwa kutuongoza kama utamaduni (malezi?), utaratibu, kanuni na pengine hata mazoea tu na hapa kinachotakiwa ni common sense tu.
 
Sawa mkuu do we have basis to say yes/no? Sasa hapo panahitajika kitu cha ziada na uwezo wa viongozi kueleza misimamo ya chama hasa katika vikao halali. Kwa wakati huu, ni vizuri tujiepushe na haya.

Tunaweza kuleta impression mbaya kwa chama. Chama kiwe na utaratibu wa kufanya internal evaluations ya wenye nia hasa ngazi za chini (Majimbo, wilaya, kata na msingi) angalau miaka miwili kabla, ili kumonita potentials wake wa baadaye na kuepuka kukurupuka na wagombea wenye nia mbaya na chama


Sio kila kitu kinakuwa kwenye katiba...kwa mfano katiba ya nchi haioneshi muda mwafaka wa binti kupata ujauzito, lakini hii haizui watu kumshangaa na hata kumlaumu binti kupata ujauzito kwa wakati usio muafaka. Wakati mwingine kuna mambo yanayotakiwa kutuongoza kama utamaduni (malezi?), utaratibu, kanuni na pengine hata mazoea tu na hapa kinachotakiwa ni common sense tu.
 
Back
Top Bottom