Dk. Charles Kimei apewe nishani ya kitaifa

Dk. Charles Kimei apewe nishani ya kitaifa

Katika watanzania waliofanya vizuri ni DK Charles Kimei.Kwa uwezo wake mkubwa wa kuibadilisha benki ya CRDB iliyokuwa chumba cha maiti na kuifanya iwe benki bora yenye matawi ndani na nje ya nchi.
Ni CEO ambaye kaonyesha kuwa haogopi ushindani na aweza shindana kibiashara ya kibenki na benki yoyote iwe ya ndani au nje ndani na nje ya nchi.
Ameijengea hadhi CRDB na kuifanya benki bora mbele za wananchi wengi ambao zamani ukitaja CRDB watu wangeuliza ndio mdudu gani huyo

Hongera yake , hata mimi Kimei nina mkubali sana kwa ni Mangi anayejua nini maana ya kuwa ceo.
 
Last edited by a moderator:
Mm simuungi mkono Kimei japo n mteja wa CRDB.HAIWAJALI WATU WA CHINI,WANA RIBA KUBWA TOFAUTI NA NMB,AJIRA ZA KIKABIRA KWA KIAS KIKUBWA, WANAPENDA KUJISIFIA KWA SHEREHE NA MAKMGAMANO.WANA MATUMIZI MAKUBWA NDO MANA HATA RIBA IPO JUU.INATUMIKA KIFISADI SANA CRDB.HASITAHIRI .

Wee hujui hata unaloongea. Sherehe na makongamano na matumizi yao yanakuhusu nini? Eti wanapenda kujisifia, wivu wa kike huo.
 
anastahili pongezi coz ameitoa point A to B,tuachage maneno mengi watz,je,crdb ingekuwa imekufa au inayumba mngesemaje?
 
anastahili pongezi coz ameitoa point A to B,tuachage maneno mengi watz,je,crdb ingekuwa imekufa au inayumba mngesemaje?

Mtanzania haeleweki mkuu, NBC imeuziwa makaburu inafanya vibaya wanapiga kelele. CRDB anaendesha mtanzania kwa mafanikio wanauliza ni kabila gani! Ajabu kabisa.
 
Kwa huo uandishi 'mbovu' hata kama una hoja unaonekana 'pumba' tu...hata hivyo, huna hoja zaidi ya bla bla blaah! CRDB ingekuwa na waajiriwa wasio na uwezo sababu ya kubebana kikabila, wangekuwa wana matumizi mabovu ya fedha kwa kuendekeza sherehe na kujisifia, ingekuwa inatumika kifisadi...basi benki isingekuwa na mafanikio yote hayo yanayosemwa!

Wewe ni ----- tu, ni sawa na mwanafunzi mjinga anayekuwa makini kusikiliza makosa ya mwalimu kuliko mada anayofundishwa.Unaweza kusherekea mafanikio uliyoyapata kwa kuibia watu.N bank ya kifisadi utakuwa haujui kwa sbbu ya uboya wako.Ajira zake sawa na uhamiaji, mwz huyo na akina Rosta.Ni watz wangapi wamefikiwa na CRDB ukilinganisha na NMB licha ya ukongwe wake?
 
Wanaona Kikwete na Diamond tu. Watu wenye mazuri hawaoni
 
Ameifanya NHC kuwa ya matajiri badala ya kuhudumia watu wa hali ya kawaida (wafanyakazi). Sioni cha kumsifu huyu ni fisadi mwingine tu. Nyumba wanazojenga za gharama nafuu million 60-80. Mfanyakazi wa umma Tz mwenye mshahara(masihara) wa laki tatu ataweza? Angekuwa na mpango wa kuwawezesha watu wa kada hii, ningemwona wa maana. NHC ni shirika la umma lakini sasa limekuwa kama la mfanyabishara binafsi anayeangalia faida tu.

Nilitegemea NHC ndio ikope Bank na kujenga hizo nyumba. Wafanyakazi na watanzania wengine wa kipato cha chini wapange na kulipa kidogo kidogo hadi wafikie kuzimiki hizo nyumba. Malipo yawe hadi miaka ishirini.

NHC inajengewa uwezo sasa.Iliyumba, sasa inafufuka.Tutaona matunda yake muda si mwingi.CRDB ilelenga maendeleo ya watu wa chini hasa vijijini, leo target imekuwa matajiri na watu wa kati.UPATIKANAJI WA MIKOPO KWA WATU WA CHINI NI MGUMU KUPITIA CRDB.
 
Mimi ni mteja wa CRDB lakini huyu bwana hakukana pale alipotuhumiwa kuhusika na kutoa pesa aliyopewa ZITTO KABWE ili kuihujumu CHADEMA,

Zile zilikuwa ni pesa za wateja kwa kupitia mlango wa TISS.

Tena ile taarifa ambayo alishindwa kuikana licha ya kutaja ofis yake (CRDB) pia imetaja jina lake. Kuwa mheshimiwa fulani alipokutana na ZITTO alimpa maagizo kesho yake aende CRDB aonane na Dr. Kimei kuna mzigo atapewa!!!!!!

Na kweli alipewa pesa nyingi ndani ya Briefscase nyekundu.


Je anafaa kuwa GAVANA BOT???????

au anastahili kupata sifa mnayomwaga hapa kishabiki?????


Sijui amewatuma ili mumpigie debe hapa JF!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Hii tuzo ni sawa kabisa kwa mtu sahihi,siyo zile anazopewa Mengi wakati hana biashara inayoeleweka.Dr.Kimei kathibitisha kuwa watanzania weusi tunaweza
Hahaaaaaa...wewe ushuzi kweli.....Mengi hana biashara za kueleweka?..IPP Media..Bonite...Migodi ya madini...ni mfanyabiashara mzalendo saaana kuliko hao matajiri wakubwa wa ki asia ambao hawaiangalii jamii wao wanapiga pesa tu,mengi anatujengea hospitali ya moyo moshi,anasaidia mayatima na wasiojiweza bola kuangalia rangi,dini au itikadi,SALUTE BABA MENGI!
 
Punguza wivu mkuu. Nenda shule kasome kitu sahihi.

Siwezi kuwa na wivu kwa Kimei kupewa tuzo.Isitoshe ninayo elimu ya kutosha kwa mazngra haya.Siwazi hata siku moja kufanya kaz bank yoyote.Tusimkweze Kimei kwa sifa ambazo hana.Amehamisha malengo msingi ya kuanzishwa bank hyo.NA NI BANK INATUMIKA NA MAFISADI!!
 
Wee hujui hata unaloongea. Sherehe na makongamano na matumizi yao yanakuhusu nini? Eti wanapenda kujisifia, wivu wa kike huo.

Yanaongeza gharama za uendeshaji zinazogharamiwa na riba wanayotoza.Tutaona bank inafanya vizuri kwa kuwa na viwango nafuu vya riba na ikiwalenga watu wa chini na kati kama ulivyokuwa msingi wake.GHARAMA KUBWA ZA UENDESHAJI MZIGO ANABEBESHWA MTEJA.HEKO NMB!!HII NDO BANK YA MFANO,KWANZA BADO CHANGA UKILINGANISHA NA CRDB LAKN INAFANYA VIZURI.
 
Yanaongeza gharama za uendeshaji zinazogharamiwa na riba wanayotoza.Tutaona bank inafanya vizuri kwa kuwa na viwango nafuu vya riba na ikiwalenga watu wa chini na kati kama ulivyokuwa msingi wake.GHARAMA KUBWA ZA UENDESHAJI MZIGO ANABEBESHWA MTEJA.HEKO NMB!!HII NDO BANK YA MFANO,KWANZA BADO CHANGA UKILINGANISHA NA CRDB LAKN INAFANYA VIZURI.
Acha kujidanganya wewe na hiyo NMB yako. Riba za benk zote kubwa tanzania hazipishani. Kama unabisha mtafute mtu anyejua amortization halafu kaombe loan repayment schedule toka benk hizo fanya ulinganisho. Utofauti ni less than 1%. Na usijidanganye kuwa opereshion cost ndo zinapandisha rate. Tatizo ni market forces na BoT wenyewe.
 
Inaaminika kuwa huyu ndie alihusika kutoa pesa ya kuihujumu chadema kupitia Zitto

Baadhi ya watu wana ajenda, wanapenda wasighuswe lakn wao wazodoe wengne.WAPO WATANZANIA WENGI WA KUTOLEA MFANO HATA MSECHU KIJANA ALIYEFUFUA NHC,WAKUU WA PENSION FUNDS, TUNAONA INVESTMENTS WANAZOFANYA NCHINI NA UBORESHAJI WA MAFAO.N.K.Anapgwa debe Kimei kwa ushabki wa kimaeneo, angeipenyeza basi CRDB kwenye soko la Kenya tuone umahri wake.
 
Acha kujidanganya wewe na hiyo NMB yako. Riba za benk zote kubwa tanzania hazipishani. Kama unabisha mtafute mtu anyejua amortization halafu kaombe loan repayment schedule toka benk hizo fanya ulinganisho. Utofauti ni less than 1%. Na usijidanganye kuwa opereshion cost ndo zinapandisha rate. Tatizo ni market forces na BoT wenyewe.

Moja ya kazi ya riba ni kugharamia uendeshaji na upatikanaji wa faida.KWA FAIDA WANAYOJIVUNIA KUPATA INGETOSHA KUPUNGUZA GHARAMA ZA MIKOPO.
 
Back
Top Bottom