Dk Bana wa REDET/UDSM unashangaza!

Dk Bana wa REDET/UDSM unashangaza!

Ibrah

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2007
Posts
2,730
Reaction score
536
Nimesoma ktk MWANANCHI leo kuhusu sakata la posho mpya za Wabunge na na Ndugai kumshukia Sumaye. MWANANCHI walitaka maoni ya Dk Bana wa UDSM.
Badala ya kutoa maoni yake juu ya 'mzozo' wa Ndugai na Sumaye, Dk Bana amembeza na kumshambulia Sumaye ati anasema hayo kwa kuwa ana uchungu wa kuikosa nafasi ya Urais baada ya kushindwa na Kikwete ktk uchaguzi wa ndani wa CCM!
Najiuliza huu ndio uchambuzi wa Dk, Mhadhiri Mwandamizi wa Siasa UDSM! Kumbe si ajabu NORAD kusitisha ufadhili REDET, Dk Bana is biased!
 
Ulichoshangaa ndio hakionekani, manake hao wote wako kwenye payroll moja halafu wanashambuliana.
 
Hao waandishi wa habari nao kwanini wanamtafuta Bana kila wakati kusikia maoni yake?

Huyu mzee mie sioni utaalamu wake zaidi tu ya kujipendekezapendekeza tu kwa CCM.
 
Kwa wasomi wa namna hii haishangazi UDSM ni mojawapo ya vyuo vinavyoshika mkia Africa
 
Huyo jamaa siku mkimsikia ameongea point, mnitafute niwape weekend treat, Matema Beach. All paid by me.
 
Huyo Bana ni kilaaza tu kama Nungai.Nimepata majibu kwa nini UDSM inazidi kuporomoka kila kukicha.
 
Unajua bwana hata waandishi wa habari nao wana vyama vyao na watu wanaowapa pesa ili kuchukua habari! Na hao wanaowatuma hao waandishi wa habari kwa Dr. Bana (Kilaza) wanajua kwamba huyu jamaa ni mropokaji anatoa majibu bila ya kufikiri kwa ufasaha. Yan ukimsikiliza utafikiri hata huo udr. wake ni kama wa JK vile (yan wakupewa/kununua), Hakuna uhusiana wa kisomo chake na matamshi yake. Inabidi tutafute chuo alichomalizia huyu bwana! Kweli mtu kama huyu anamshauri rais? yan ni kama zero + zero
 
nilimshusha thaman alipoenda kwa vyombo vya habari na kutoa result za tafiti mpya redet iliyofanya, tafiti yenyewe ilikua inapima umaarufu na kukubalika kwa rais kikwete! nikajiuliza ivi hii ndo shabaha ya elimu aliyopewa na nyerere huyu mzee kuweatuymikia watanzania? dokta mzima una commit resources kufanya tafiti kama hiyo? ivi title za tafiti hazipimwi kama zina tija kwa jamii au la kabla hazijafanywa? sasa kupima kukubalika kwa kikwete kunawasaidia nini watanzania dhidi ya mfumuko wa bei na kupanda kwa gharama za maisha? kweli ukistaajab ya musa utayaona ya .........................
 
Nimesoma ktk MWANANCHI leo kuhusu sakata la posho mpya za Wabunge na na Ndugai kumshukia Sumaye. MWANANCHI walitaka maoni ya Dk Bana wa UDSM.
Badala ya kutoa maoni yake juu ya 'mzozo' wa Ndugai na Sumaye, Dk Bana amembeza na kumshambulia Sumaye ati anasema hayo kwa kuwa ana uchungu wa kuikosa nafasi ya Urais baada ya kushindwa na Kikwete ktk uchaguzi wa ndani wa CCM!
Najiuliza huu ndio uchambuzi wa Dk, Mhadhiri Mwandamizi wa Siasa UDSM! Kumbe si ajabu NORAD kusitisha ufadhili REDET, Dk Bana is biased!
Katika wahadhiri wachambuzi wa siasa sijawahi kuona wa hovyo kama Bana, ameleweshwa u-ccm na ndio maana hata hana ubavu wa kuchambua kwakuwa uchambuzi wa siasa za nchi yetu mara nyingi unailemea ccm
 
Huyu DR. BANA a.k.a KILAZA ananiuzi sana, yaani uchambuzi wake ni wa kI-CCM zaidi na siku zote ninapofungua luninga yangu na kukuta huyu Dr. anaongea, aslan! nabadilisha channel au naendelea kufanya issue zingine. Lakini, nilishawahi kumhoji ktk darasa tukiwa watu wachache (special programme) kuwa KWANINI mara nyingi akihojiwa anapendelea sana kutetea serikali, kweli majibu yake yaliniudhi kwani alijibu kuwa "Wengi tunadanganywa na vyama vya upinzani, na hatuoni maendeleo makubwa yaliyofikiwa na serikali inayotawala". Nilikuja kugundua kuwa Mzee huyu Dr. ni mshauri wa president kwenye masuala ya siasa na Mipango etc. ndio maana anadefend sana serikali kwani yeye ndiye mshauri ktk mambo hayo yanayofanya na serikali. Alaaniwe na usomi wake.
 
Kwa wasiomjua Dr. Bana, ndio mnaodhania, anajipendekeza, au anajikomba komba kwa CCM/JK. No. Kwa sisi tunamjua na kuijua REDET, tangu kitambo jinsi inavyofanya kazi nzuri haswa zile opinion polls zake, zilivyofanya kazi nzuri kwa CCM kwa kufanya kazi ya trend set ya ushindi hadi kupelekea Prof. Rwekaza kupewa asante ya U-VC, hivyo DR. Bana ni strategist mzuri anaejua aseme nini ili watawala wafurahi.

Mimi kama mshabiki wa Lowassa, naishauri ile kamati yake ya urais 2015, tuitumie na REDET vizuri, watutengenezee opinion poll yetu kuonyesha 2015, Watanzania wanamtaka Lowassa ili kujenga trend ya ushindi, tena akishashinda, Dr. Bana ndio anachukua nafasi ya VC kama asante yake!.
 
Kwa wasiomjua Dr. Bana, ndio mnaodhania, anajipendekeza, au anajikomba komba kwa CCM/JK. No. Kwa sisi tunamjua na kuijua REDET, tangu kitambo jinsi inavyofanya kazi nzuri haswa zile opinion polls zake, zilivyofanya kazi nzuri kwa CCM kwa kufanya kazi ya trend set ya ushindi hadi kupelekea Prof. Rwekaza kupewa asante ya U-VC, hivyo DR. Bana ni strategist mzuri anaejua aseme nini ili watawala wafurahi.

Mimi kama mshabiki wa Lowassa, naishauri ile kamati yake ya urais 2015, tuitumie na REDET vizuri, watutengenezee opinion poll yetu kuonyesha 2015, Watanzania wanamtaka Lowassa ili kujenga trend ya ushindi, tena akishashinda, Dr. Bana ndio anachukua nafasi ya VC kama asante yake!.

We Pasco, upo serious au just joking?

Vyovyote vile Bana ni disgrace kwa wasomi wetu wa juu kabisa. Ukimsikiliza sana Bana kwa makini unagundua kabisa kwamba kama hawa ndo wasomi wetu, basi kitu hakiko sawa katika mfumo wa elimu zetu za juu tunazozitoa kwa watoto wetu na kwa vizazi vyetu vijavyo. Hivi political theorists wanaotakiwa kuzalishwa pale Mlimani wanamtegemea Bana wa an opinion poll NGO ya REDET? Dr mtu mzima kabisa anajitamba na kupata credit kwa tule turesearch twa questionnaires kuwauliza watu kama Kikwete anakubalika au vipi halafu na nyie mnasema ni strategist wa maana?
 
Hivi Dr. Bana (a.k.a. Rugimbana) amesomea shule zipi O-level na A-level na alifaulu katika madaraja (divisions & points) gani kabla ya kwenda UDSM?
 
Hivi Dr. Bana (a.k.a. Rugimbana) amesomea shule zipi O-level na A-level na alifaulu katika madaraja (divisions & points) gani kabla ya kwenda UDSM?
dr bana hakuwahi kusoma A level aliku mwal mkuu wa shle ya msigi
Drbana
 
Back
Top Bottom