Dk. Bana ataka kugombea ubunge kupitia CHADEMA

Dk. Bana ataka kugombea ubunge kupitia CHADEMA

Simchezo

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2012
Posts
463
Reaction score
374
Katika gazeti la mwananchi la leo amesikika Dk. Benson Bana akisema ana mpango wa kugombea ubunge jimbo la Bukoba vijijini kwa tiketi ya Chadema.Hii imekaaje wadau?


...Kadhalika, Dk Bana alikanusha tuhuma zilizotolewa na Dk Slaa dhidi yake akisema hajawahi kuwa na uhusiano na Twaweza huku akidai kuwa hata yeye mwenyewe anatamani CCM itoke madarakani miaka mitano tu, ili wananchi wapate uongozi tofauti.

"Kwa kweli ningekuwa na simu ya Dk Slaa ningempigia. Chadema na Ukawa wakijipanga wanaweza kuchukua nchi maana wana ushawishi mkubwa kwenye vyombo vya habari na makundi ya jamii.

"Kosa walilolifanya ni kumtimua Zitto Kabwe, ni kama vile Barcelona bila (Lionel) Messi. CCM sasa hivi imechokwa wananchi wanataka kuona uongozi tofauti," alisema Dk Bana.

Alisema kitendo cha Chadema kumhusisha na CCM kitakwamisha mpango wake wa kujiunga na chama hicho ili agombee ubunge katika Jimbo la Bukoba Vijijini... "Ingawa familia yangu haipendi niingie kwenye siasa, bado naendelea kufikiri, lakini kwa mambo haya (Chadema) watanikubali kweli?" alihoji.

Chanzo: Gazeti Mwananchi | 14 Novemba,2014
 
Weka source vizuri. Dr. Bana (Prof.) huwa anajipambanua kama mtu neutral.
 
Katika gazeti la mwananchi la leo amesikika Dk Benson Bana akisema ana mpango wa kugombea ubunge jimbo la Bukoba vijijini kwa tiketi ya Chadema.Hii imekaaje wadau?

Sidhani kama CDM ni wajinga kiasi hiki?! Huyu atauza jimbo kwa ma-CCM zero hours, kama CDM wakifanya makosa hayo ya kumsimamisha.
 
Mwehu huyu bukoba vijijini inahitaji jembe wa kusaidia maendeleo ya jimbo
 
..."Kosa walilolifanya ni kumtimua Zitto Kabwe, ni kama vile Barcelona bila (Lionel) Messi...

Nakubaliana na Prof. Bana, CHADEMA walifanya kosa kubwa sana kumfukuza Zitto,maana toka wameenza naye migogoro umaarufu wa CHADEMA umeporomoka vibaya sana kama Liverpool msimu huu baada ya kumuuza Luis Suarez.
 
Gazeti la tarehe ngapi hilo

La leo tar 14. Nov. 2014
 
Bukoba Vijijini ni stori ya miamba miwili (Rweikiza vs Karamagi) kati ya hawa mmoja ni mbunge tayari kupitia CCM
 
Huyu alikuwa akikwepa kujibu tuhuma za Email yake kwa Lowassa kuhusu utafiti wa twaweza ........
 
Atuthibishie kwamba hana kadi ya ccm nasi tumpe ushahidi kwamba anayo huyu Bana
 
Mi natamani apande boda boda afu aanguke iwake moto nguo zake zotee ziungue afu yeye awe hai tujue ukweli wa huyu bana maana simwamini kabisaa
 
Aache mambo yake ya kilaghai nani asiyejua kuwa yeye ni CCM damu.
 
Back
Top Bottom