Dk. Bana ataka kugombea ubunge kupitia CHADEMA

Dk. Bana ataka kugombea ubunge kupitia CHADEMA

Katika gazeti la mwananchi la leo amesikika Dk. Benson Bana akisema ana mpango wa kugombea ubunge jimbo la Bukoba vijijini kwa tiketi ya Chadema.Hii imekaaje wadau?



Chanzo: Gazeti Mwananchi | 14 Novemba,2014

Namba ya Dr Slaa ni 0783 967519.
 
Bunsen Burner kada wa ccm. Amepiga prpaganda kipindi chote cha JK hakuonekana wa maana. Sasa ananza kujikomba ccm. Huyo hana tofauti na Shibuda. Aende ACT au TLP
 
Huyu Bana ni Tapeli mkubwa.Afadhali ya Shibuda kuliko huyu
 
mara nyingi kauli zake zinaonyesha ni mwanaccm, chadema haiwezi kumteua kugombea ubunge
 
Asubiri baada ya miaka 20 atafikiriwa
 
hivi ni vituko sasa mumtoe zitto alafu mumwingize dr bana inachekesha sana.maana kazi ya zitto na dr bana kwenye siasa za tanzania ni moja
 
anataka kutokea kwenye media hana lolote, huo ndo uchafu wenyewe tumemkataa aliyechafuka sembuse uchafu wenyewe?
 
Nakubaliana na Prof. Bana, CHADEMA walifanya kosa kubwa sana kumfukuza Zitto,maana toka wameenza naye migogoro umaarufu wa CHADEMA umeporomoka vibaya sana kama Liverpool msimu huu baada ya kumuuza Luis Suarez.

Can u see what u've written?!? CDM bila hako kasaliti ndo imezidi kupaa. Uchaguzi wa mitaa CDM ilikuwa tayari imeshakatia pini hako kasaliti na bado imepaa. Na utaona Graph yake inavyo shoot baada ya uchaguzi mkuu. Unaweza kudhihirisha umaarufu wa CDM umeporomoka vp!? ACT-Mawese na magamba mnachekesha sana
 
Wana chadema nimesoma katika gazeti la mwananchi la jana Dr Bana akilalamikia kauli ya Dr slaa kumhusisha na ccm katika matokeo ya utafiti yaliyotangazwa juzi.

Katika kauli aliyoitoa Dr Slaa alisema haya amini matokeo ya utafiti huo Kutokana na kumhusisha Dr Bana na taasisi yake.

Dr slaa aliongeza kuwa kabla matokeo ya utafiti huo kuwekwa hadharani alikuwa ameshapata na kuyasoma na katika utafiti wake alibaini kuwa yalikuwa na mkono wa kigogo mmoja wa serikali.

Dr slaa aliongeza kuwa alipata nakala ya barua pepe iliyotoka kwa kigogo huyo ikiishukuru taasisi hiyo kwa kazi nzuri Waliyofanya na mambo yamekwenda kama walivyo panga.

Katika utetezi wa Dr Bana anamlalamikia Dr Slaa kwa kumhusisha na ccm na kuongeza kuwa hata yeye anatamani Ccm iondoke madarakani japo kwa miaka mitano tu ili watanzania waone tofauti.

Dr Bana anaseme kauli iliyotolewa na Dr Slaa imemfadhaisha sana kwakuwa anampango wa kugombea ubunge kupitia chadema lakini kwa sasa anawasiwasi kama atapokelewa vizuri na wana chadema kutokana na kauli alitoitoa Dr Slaa.

Cdm dhambi ya usaliti itawatesa mno,mnatapatapa sana na bado mpk kieleweke
 
Weka source vizuri. Dr. Bana (Prof.) huwa anajipambanua kama mtu neutral.

Dkt Bana hana hata chembe ya 'neutrality'. Pamoja na kujipambanua kama msomi wa sayansi ya siasa ameshindwa hata kufanya uchambuzi ambao ni 'balanced'. Wakati wa BMK hakuona tatizo la kuwekwa pembeni kwa rasimu ya Warioba; badala yake alitetea kitendo hicho kuwa ni halali kwa kigezo cha 'tyranny of numbers'. Sidhani kama CDM wamekosa watu wa kusimamisha huko Bukoba mpaka wamsimamishe Dr. Bana.
 
Katika gazeti la mwananchi la leo amesikika Dk. Benson Bana akisema ana mpango wa kugombea ubunge jimbo la Bukoba vijijini kwa tiketi ya Chadema.Hii imekaaje wadau?



Chanzo: Gazeti Mwananchi | 14 Novemba,2014

Kwa nia njema kabisa namshauri akasaidiane na Zitto na profesa mwenzake Kitila Mkumbo kujijenga ACT
 
Pandiki lile zee nani analitaka?akagombee kwa chama chake cha ccm au aende ACT
 
Mimi namkaribisha ila tu ajue ndani ya chadema hatigawani vyeo
 
Nakubaliana na Prof. Bana, CHADEMA walifanya kosa kubwa sana kumfukuza Zitto,maana toka wameenza naye migogoro umaarufu wa CHADEMA umeporomoka vibaya sana kama Liverpool msimu huu baada ya kumuuza Luis Suarez.
hawajafanya kosa...zito kajifukuzisha mwenyewe kwa kuvunja katiba ya chama huku akijua kufanya vile atakuwa kajifukuza....kiukweli zzk alianzisha chama ndani ya chama....ndo maana baada ya siku sita kapata cheo ambacho hakipo....kiongozi mkuu....kumbuka katiba ya actttt inasema mwanachama anaruhusiwa kugombea uongozi akiwa na umri usiopungua miezi sita chamani...jiulize zzzzkkkk katimiza lini hiyo miezi?
 
Back
Top Bottom