Phb_himself
JF-Expert Member
- Jul 5, 2017
- 222
- 189
Mwanajua imetoka 27 Dec 2020 na JPM kafariki 2021
Weka mstari unaokutatiza mimi nitakupa tafsiriConcept behind?
Mwanajua imetoka 27 Dec 2020 na JPM kafariki 2021
Ndio maana nikakwambia weka mstari ambao huuelewi nikujuze.Kwani alivoimba almasi umeelewa ?
Kamzungumzia Diamond Platnumz miaka mingi mbeleni!
Navoamini mimi Dizasta ni kama time traveller anaandika vitu vya kufikirika sana ni kama utabiri..sometimes concept zake ni kama nabii tunasubiri zitimie
Huu ni mtazamo wangu!
Naheshimu mtazamo wako pia
Ila mwanajua bado inanisumbua natamani nikutane na dizasta nimuulize,alikuwa anamaanisha nini?
Nmepitia comments nyingi YouTube wengi pia wanafikiria “clouds fm” or “JPM
So nawew unaeza share code zako
Ni maoni sio sheria,so be free
Jamaa namkubali sanaNi kweli Jamii imejaa sana ujinga that’s the reason why he’s not famous.
View attachment 2474009
Edger Vicent Mwaipeta (born February 17, 1993), known to one and all as Dizasta Vina, is a hip-hop musician from Mbeya, Tanzania.
He is known for his unique rhyme schemes and unparalleled storytelling.
His style transforms rap into philosophically viable poetry, delivering thought-provoking verses.
Dizasta Vina has managed to continuously issue hit after hit while maintaining a cult-like fan following that has fuelled the rapid rise of both his music and his reputation.
Kwa muda mrefu sana nmekuwa namfuatilia Dizasta toka enzi za Tamaduni,ni mmoja ya ma rapper bora zaidi kuwahi kutokea hapa bongo,uandishi wake na uwezo wa kufikiri umenifanya isipite siku bila kumsikiliza
Tayari anazo album/mixtape kadhaa sokoni
1. The wonder kid
2. The Verteller
Moja yaa ubunifu wake ni kutoa nyimbo zenye mwendelezo yaani kama movie series
-HATIA (1-5)
-No body is safe (1-4)
-Confession (mad son,mad teacher,mad philosopher)
Kama hujapata muda wa kumsikiliza huyu jamaa ebu pita YouTube sikiliza hizo ngoma kuna kitu utapata!
The verteller ni moja ya album bora kwangu 2020
Kama unamkubali dizasta Vina dodosha punchlines
Ambayo unaikubali kutoka kene ngoma zake.
Jamaa kagoma kutuletea tafsiriWalikuja madogo wajanja na mapesa
Wakauliza mama ukivaaje unapendeza
Wakamuahidi ndizi, mawaridi na hariri
Lakini jasiri rangi yake ya asili ilitesa
Jamaa kagoma kutuletea tafsiri



msimuliaji anazaliwa,
msimuliaji anajifunza na
kisha anafanya makosa,
anaingia kwenye mapenzi,
anajuta,
msimuliaji anapata faraja na
mwisho wa siku msimuliaji anakufa.!Sasa mkuu mbona nawewe unachanganya tena madesa, mwanzo unasema ulihisi inaongelewa clouds, badae ukajiridhisha kuwa anaongelewa JPM...!Kapotea tena..
Wakati aliomba line atafsiri
Ngoja nimpe code
Hapo imezungumzwa bongo fleva ya akina janjaro
Amezungumzwa jasiri mwongoza njia
So..ukifatilia vizuri utaona hii ilikuwa “clouds fm” against “music industry”
Dizasta is the master of big words![]()
Sasa mkuu mbona nawewe unachanganya tena madesa, mwanzo unasema ulihisi inaongelewa clouds, badae ukajiridhisha kuwa anaongelewa JPM...!
Hence umerudi tena kwa clouds, itoshe kusema kuwa jamaa katuumiva vichwa na ataendelea kutuumiza vichwa hadi pale atakapoamua mwenyewe kutoa tafsiri rasmi
Naheshimu mawazo yako mkuuOfcoz bado naumiza kichwa kipi hasa kati ya hivo
Maana kwangu vyote vina “click” hizo concept 2
Ndo maana nakaribisha mawazo mbadala na hoja
Ili tupate tafsiri kamili..I’m very flexible
Ili mradi tu mtu aje na hoja! Ili tufungue code
Kama ilivofanyika kene shahidi
Ni mtazamo binafsi na Niko tayari kurekebishwa.
that’s all
"Alizaliwa mashariki alifahamika mahali pote"Concept behind?
Hatia V mkuu, lete madiniAlizaliwa mashariki...... na mwisho alionekana ziwa Tanganyika (magharibi)
.
.
.
Tuliwaonea wivu rafiki zake mekuri na veneranda ( Mercury na Venus )
Haya Tafakari tena.
Halafu nitakwambia HATIA V kagusa nini
Safi mkuu hadi hapo tuko pamoja na uko Sawa na tafsiri ya walio wengi ila kuna sehemu bado panahitaji msaada"Alizaliwa mashariki alifahamika mahali pote"
Hapo zingatia upande ambao jua hutokea alfajiri.
"Alitamalaki nuru ilitua mahali kote"
Hii inajieleza yenyewe.
"Hakuna aliyemgusa kwani alikuwa wa moto sana"
Hii line inaelezea character ya jua.
"Tuliwaonea wivu rafiki zake Mekuli na Veneranda"
Mekuli ni mercury, veneranda ni vernus. Hizi ni sayari zilizo karibu na jua, hivyo kwenye kazi yake ya uandishi kaziweka ni marafiki zake.
"Wazungu walikuja na pozi kibao
Walimkaribia mwisho walibabuka Ngozi zao"
Hii line inaonyesha wana anga wanashindwa kumsogelea kwa sababu ya joto.
"kuna walo'diri kumwita Mungu
Walitukuza walisadiki na kuabudu"
Hii ni kwa wanaoabudu jua.
"Tuliishia kumwona mbali na mwisho kuumia macho"
"Maana alingáa sana kiasi alizificha nyota kama wingu"
"Tulikosea kwani... zile sifa hazivai tena
Imefika jioni na yeye hang'ai tena"
Hapa anaonyesha ilivyofika jioni zile sifa zote za jua zikapotea.
"Najiuliza, alifichwa na ndugu kwenye kaya? Au alinenepa kutoka aliona haya"
Hii ni jioni wanamtafuta jua haonekani tena.
"Nuru yake pahala pote ilitawanyika
Toka mzizima pwani kote alipagawisha
Aliondoka na mwisho alionekana ziwa Tanganyika"
Kigoma kule ndio jua linapozamia "joke" ila utakuwa unajua jua huwa linaishia ziwa tanganyika kigoma huko kwa ukanda wetu.
"Dhahania zimeandikwa alichoka pengine
Aliondoka ili wang'ae nyota wengine"
Hapa ameonyesha kuwa jua ni nyota na anajiuliza usiku ulipofika aliondoka ila wang'ae nyota wengine? Akimaanisha hizi nyota za usiku.
Kwa hizo lines toka nilivyosikia siku ya kwanza niling'amua kuwa muhusika ni jua kama tafsida ambayo unaweza kuiweka kwenye jambo lolote linaloendana na mada.