Diwani wa kata ya kibaoni ifakara na kashfa ya ufiadi

miti

Senior Member
Jun 16, 2012
136
23
wana JF habari zenu. ninabarua mbayo nimeipata inayohusu ufisadi wa diwani ambayo nimeshindwa kuiskani kutokana na kutokuwa na scana, il imenibdi niiandike kama ilivvo
CHAMA CHA MAPINDUZI

OFISI YA KATA, YA KIBAONI

S.L.P 29,

KIBAONI – IFAKARA .

18/11/2012
KUMB NO. CCM/KBN/KM/1/12
KATIBU CCM MKOA
MOROGORO
YAH: MALALAMIKO MUHIMU KUTOKA CCM KATA KIBAONI WILAYA YA KILOMBERO
Somo la hapo juu lajieleza kama inavyosomeka Halmashauri ya CCM Kata ya Kibaoni iliketi 07/11/2012 na kuangalia mwenendo mbovu wa Diwani Msika kwa kutokuwa mwaminifu katika utendaji wa kazi na tuhuma nyingi za pesa zilizoliwa za michango ya wananchi na wahisani. Pamoja na mihutasari mingi kuletwa wilayani lakini hakuna hatua zilizochukuliwa. Hivyo Halmashauri ya chama Kata ya Kibaoni imepoteza kabisa imani na Diwani wao Msika. Mpaka tunaleta taarifa kwenu Mkoani Wilaya wajua matatizo ya Diwani huyo hivyo ni mategemeo yetu mtatusaidia katika hilo.NB: Halmashauri kuu ya Kata imependekeza kumsimamisha Diwani huyu kwa nia ya kukinusuru chama.


KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
NAKALA:-
1. MWENYEKITI CCM MKOA MOROGORO - KWA UFUATILIAJI
2. KATIBU CCM (W) KILOMBERO

 
Mangulla, Kinana na Nape sasa ni wakati wa vitendo kama mlivyoahidi na sio maneno matupu.

Mfukuzeni sasa huyo diwani ili msafishe chama chenu.
 
Nangojea taarifa za uchunguzi zenye mashiko alafu nitachangia hoja.

Barua yao haina vielelezo muhimu zinazoendana na tuhuma
 
Back
Top Bottom