Diwani wa Kata ya Unyambwa katika Manispaa ya Singida, Nd. Shaaban Salumu Satu amemtembezea kipigo cha mbwa mwizi, na matusi ya nguoni, mfanyakazi katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, ndg. Ramadhan Sumwa. Naibu Meya wa Manispaa hiyo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na anasema wanawapatanisha, lakini chanzo chetu kinaonesha ni kuzidiana dau katika migawo.