Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 (Tanzania Development Vision 2025)...

wizi mtupu mulugo na ndgye kikwete hawana jipya chezea mchna wewe hyo gesi mutaambulia patupu wamepandisha umeme ili waje wawambie tulieni tuchmbe gesi mapema ili umeme ushuke mkae kimya mi ccm na wana ccm cwaelewi bora hii nchi rais awe mubabu asiye natamaa kama sharo kiwete ananunua 2 matenki na semi anawapa miraji na riz nyie munabki munashanglia umavi 2 mi c waafki wanafki hawana mana
 
shida iliyopo weng hudhan kwamba hiyo 2025 basi mahela yanakuwepo mfukon.
xio hvyo watanganyika.
1: tujishughulishe watanganyika. tuthamini muda na pesa. tujitahid kupunguza sherehe hasa uswazi.
2: tuwe makini kwenye uchaguz wa viongoz wa nchi. tuache kuchagua bendera na rangi za vyama bali tuchague mtu
3: atafutae hachoki, akichoka basi ujue ameshapata
"EVERYTHING IZ POSSIBLE UNDER THE SUN"
 
Katika kongamano la Taasisi za kidini nchini, lililofanyika Whitesand mgeni rasmi akiwa Dr J.M Kikwete rais wa J.M Tanzania, Waziri mwenye dhamana ya Madini yetu Prof. Muhongo ametuhakikishia kwamba kufikia mwaka 2025 Tanzania itakuwa imetoka kwenye umasikini nakuwa kwenye kiwango chakati.. Akisema kwakujiamini kuwa Kilimo ambao ndio uti wa mgongo umeshindwa kutukomboa, ufugaji umeshindwa pia, kasema yeye mtu wakanda ya Ziwa uvuvi nao haujawakomboa. Lakini Neema hii ya Gesi asilia itatutoa kwenye umasikini kwani wizara yake haina Mlarushwa, Hakuna Mhaini wala Mlaghai pale Wizarani kwake.
Kwahyo wadau tuombe Mungu mipango iende sawa.

labsa kama ndoato za kuwaondoa mafisadi kwa kura ifikapo 2015 itatimia
 
Hiyo 2025 wewe utakuwepo? Mbona walianza kitambo tambo hizo?

attachment.php


Muhonga alishaahidi kuwa mgao wa umeme utakuwa historia, akaja na stori ya kutopandisha bei za umeme! kunalililowezekana?
 
Ni muongo .....kama kwa Sasa tuna ges lakn tunauziwa ges kwa tsh 64000 kwa kg 15.....amefanya nn luhusu upandaj huo???? Aliahid kua mgao wa umeme ungelua historia katika kpnd cha Mwaka mmoja ulopita kafanua nn??? Stupidity........tumechoka kudanganywa na serikal ya CCM isojal wananchi wake...
 
Kama kutakuwa na mikakati na usimamizi mzuri, yes is possible, vinginevyo ni ndoto za Alinacha.
 
Ila kiukweli hawa viongozi wetu ahadi wanajua kuzitoa tena hasa.. lakin chakushangaza nimetoka kijijini majuzi huko Mbuguni mbona nibora miaka 15 iliopita kuliko sasa!! Watu wamezidi omba omba na hali imezidi kuambaya.. yani sasa hakuna mapambazuko kila wakati nigiza totoro mtu hajui kesho atakula nini..
Tunawaomba viongozi wawe wanatembea mara kwa mara huko vijijini wasisubiri kipindi cha uchaguz.
 
...vipi kuhusu ile ahadi ya 2005-2010 ya maisha bora kwa kila mtanzania imeishia wapi?...
 
Utadai vipi unataka kuipeleka Tanzania 2025 wakati mawazo yako yameganda 1964?

Ni ujinga, ukiniuliza, kwa Mheshimiwa Sitta kudai kwamba uteuzi wake ndani ya CA unaenda sambamba na wingi wa wajumbe toka CCM. Wingi wa wajumbe toka CCM ni ukweli, lakini kama Mheshimiwa Sitta angekuwa na akili na busara kidogo, angetambua kwamba muktadha wa Bunge la Katiba ni tofauti na siasa za kawaida. Isitoshe, lengo la Katiba ni kuipeleka Tanzania miaka 100 ijayo, siyo kuendekeza ujinga na siasa za leo!

Hivi kweli, kama Nyerere angekuwa na akili za kitoto kama hizo za akina Sitta, angeruhusu vyama vingi kweli Tanzania?
 
Yeye asema tutaipeleka Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati 2015-2025.
Naibu waziri wa fedha aliyetokea kugusa mioyo ya watanzania masikini na kufufua matumaini yao ndg Mwigulu Nchemba juzi alikonga nyoyo za wananchi wa Tabora waliofurika Igunga kumsikiliza. Mwigulu aliyekuwa akishangiliwa kila alipofafanua hoja aliwaacha wanaigunga wakibaki makundi makundi mpaka giza lilipoingia wangali viwanja vya Sokoine kutafakari hotuba yake iliyokuwa na sura ya kiongozi wa taifa.

Katika hotuba yake mwigulu alirudiarudia neno "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI IFIKAPO 2025" na kushangiliwa kwa kishindo.

Mwigulu alibainisha kuwa mambo ya msingi kufikia hatua hiyo kuwa ni

1) Maadili na uzalendo wa wasimamizi wa rasilimali za taifa. Mwigulu alisema wanahakikisha kwamba kila fedha inakwenda kutoa huduma iliyokusudiwa, tunahakikisha kodi za wananchi zinakwenda zilipokusudiwa. Tukikusanya fedha kwa ajili ya umeme, tunasimamia iende kwenye umeme, tukikusanya fedha ya barabara tunahakikisha zinakwenda kwenye barabara, hivyohivyo kwenye Afya, elimu nk. Mwaka jana tumegundua tulitoa zaidi ya 48bil kwa ajili ya dawa mawilayan lakkni ni 7bil zilitumika kununua dawa huku kila mgonjwa akienda hospital anahundulika na homa na kuambiwa kanunue dawa kiosk kile, huu ni wizi, kiosk kinatoa wapi dawa ambazo serikali haiwezi kupata kama sio kufanyia biashara dawa zilizonunuliwa kwa kodi za watanzania. Naagiza hili likome na hatua zitachukuliwa, madiwan na vyombo vya dola simamien hili. "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI"

2) Kuachana na kufanya kazi kwa mazoea.

Mabadiliko ni vitendo na yanaonekana kwa kubadili style ya kufanya kazi ili kulinda fedha za umma. Timebadili ulipaji wa mishahara kipambana na mishahara hewa. Tumebaini zaidi ya wafanyakazi elfu kumi na nne (14,000) walioyeyuka tjlipoomba akaunt zao na 1,900 wa keshi nao wameondolewa kwenye malipo. Tumeokoa zaidi ya bilion 40. Naagiza maofisa wote wahakiki watimishi waliopo kazini na walete akaunt. Tukibaini makosa yule aliezembea atafute kazi ya kufanya na hatua zitachukuliwa. Mpk sasa waliozembea tumewapeleka polisi na TAKUKURU wafikishwe mahakamani.

Tumekagua madai tukagundua udanganyifu, kwenye bilion 500 tumegundua halali ni bilion m100 tu, tumeokoa bilion 400 na tumewapeleka polisi wote waliodanganya. Naagiza wakaguzi watimize wajibu wao kabla ya kuleta madai wizani kwangu. Wakileta tutskagua, Tukigundua udanganyifu aliyeleta hiyo atafute kazi nyingine ya kufanya na tutamburuza mahakamani. "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI"

3) Tutapunguza pengo kati ya walionacho na wasionacho kwa kutekeleza vyema sera za kodi.

Tutawatoza kodi matajiri ili fedha hizo tuwasomeshe watoto wa masikini. Tutatoza kodi matajiri ili fedha hizo tupeleke huduma za maji, madawa, umeme na barabara vijijini. Hatuwezi kuwasamehe kodi matajiri mabilioni ya shilingi, wakwepe mabilioni ya shilingi halafu sisi tukimbizane na wajane wanauza matembere kulipa ada elfu 20 mashuleni. Tumefuta misamaha kwa matajiri tuache kuwssumbua wajane na masikini kutafuta elfu 20 za sekondari. "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI"

4) Tutasimamia mgawanyo wa rasilimali ili keki ya Taifa iwanufaishe watanzania wote kwa usawa.

Tumebana matumizi ya serikali yasio ya lazima ili fedha hizo ziende kwenye miradi ya maendeleo. Tutahakiki bajeti za kila taasisi ya umma na kufuta matumizi ya anasa. Hatuwezi kuwa na shirika la umma linatumia fedha kwa anasa huku watoto wakikaa chini. Kupewa kuvuna rasilimali za umma ni dhamana tu sio shamba binafsi na mashirika na taasisi zote za umma mnaokusanya fedha tokea rasilimali za Taifa mlielewe hili. Hatuwezi kuwa na watanzania hapa wanaishi tanzania na wengine wakiishi kama ulaya wakiwa hapahapa kisa wamepewa dhamana ya kusimamia shirika la umma. "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI"

5) Tutatoza kodi kwa matajiri, tuwapinguzie kodi walimu na wafanyakazi wengine, tutatoza kodi tuziwezeshe sekta zinazotoa maisha kwa watanzania wengi ili KUONDOA UHUSIANO WA KUKUA KWA UCHUMI HUKU UMASIKINI NAO UKIKUA.

Tukiwedha fedha kwenye sekta zinazolisha na kuendesha maisha ya watu wengi tutakuza uchumi huku umasikini wa watu wa chini ukipungua.

6) Kuna watu walinunua viwanda vyetu, wamelipa, wamewekeza, wameendeleza, wametengeneza ajira, wameheshimu mikataba, wanalipa kodi nawapongeza sana. Lakini nimeangalia kumbukumbu kwenye mafaili kuna watu walinunua viwanda, hawajawekeza, hawajaviendeleza, wamegeuza viwanda kuwa magodauni, wameuza vyuma chakavu, wamepeperusha ajira, wameua mazao ya wakulima kwa kuua viwanda vya nguo, wameua mazao ya mifugo kwa kuua viwanda vya ngozi, viatu, hawajaheshimu mikataba, hawajalipa serikalini, wametajirika kwa kuchukua mali ya umma. Nawambia wakaangalie upya mikataba inasemaje, vinginevyo wajiandae kisaikolojia.Video inakuji soon
 
2025 mbona mbali? Lakni uzembe kazini au kufanya kazi kwa kiundugu undugu hatufiki popote watakao pata maendeleo ni watu wachache na sio taifa zima.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom