Dini vs Ushirikina: Kwanini ningechagua ushirikina

Dini vs Ushirikina: Kwanini ningechagua ushirikina

Dini ni njia buniwa ya mwanadamu ya kumtafuta Mungu iliyoshindwa vibaya kabisa..chochote afanyacho mwanadamu chini ya jua hakina ukamilifu wa kimungu kwakuwa mwanadamu mwenyewe si mkamilifu.
Naomba ushahidi na utoe mfano kuthibitisha ya kuwa dini ni njia iliyo buniwa na mwanadamu na ilianzaje anzaje ?
 
Ndio sababu ninaamini washirikina ndio washindi wa maisha hapa duniani. Kiongozi wa dini anakemea ushirikina huku akiwa amebeba bonge la hirizi kiunoni , Nia yake anataka wengi wafunge macho na kuomba huku yeye akipeta. Amini usiamini kila penye kitu kizuri kuna shetani . Kumbuka shetani alimwambia nabii Issa kwamba utajiri wa dunia ni wake. Wewe zingatia "life is a game, play it."
 
Maslahi yangu kiroho: mimi ni mshika dini kwa imani na dhehebu langu na nina hofu na Mungu
Huu ni uongo wa kauli na matendo au unaidanganya nafsi yako.

Huwezi kuwa mshika dini ukawa mshirikina,sababu ushirikina unakutoa katika dini hasa dini ya Uislamu.

Swali langu ni Wewe ni dini gani na dhehebu gani na kwanini upo kwenye dini hiyo na dhehebu hilo ?
 
Ushirikina haujawahi kufanya mambo mabaya hivyo kama yaliyofanya kwa kutumia dini...lakini ushirikina unatumiwa vibaya na wanadini kama pitio na kimbilio la kutupia lawama na mabaya yote kuficha madhaifu yao kwenye dini
Ushirikina wenyewe ni jambo baya,vipi ufanye baya lingine zaidi yake.

Kwanza tujikite katika usuli,huku ndiyo mambo huzalikana,ushirikina ni nini ?
 
Huu ni uongo wa kauli na matendo au unaidanganya nafsi yako.

Huwezi kuwa mshika dini ukawa mshirikina,sababu ushirikina unakutoa katika dini hasa dini ya Uislamu.

Swali langu ni Wewe ni dini gani na dhehebu gani na kwanini upo kwenye dini hiyo na dhehebu hilo ?
Mwamba jiandae uende Masjid huku utachafuka roho yako na swaumu hii Kali aisee!
😂😂😂😂😂😆
 
Maslahi yangu kiroho: mimi ni mshika dini kwa imani na dhehebu langu na nina hofu na Mungu

Dini ni njia buniwa ya mwanadamu ya kumtafuta Mungu iliyoshindwa vibaya kabisa..chochote afanyacho mwanadamu chini ya jua hakina ukamilifu wa kimungu kwakuwa mwanadamu mwenyewe si mkamilifu.

Ni katika kutengeneza huo mfumo uitwao dini binadamu anajikuta anajichanganya mwenyewe ama kutofautiana na mwenzake, ama kabila na kabila, imani na imani... Kufikia hapo ndio zikaanza kufumuka dini na imani za kila aina

Wanaomtaja na kumwamini Mungu wakawa na dini zao nyingi tu lakini ndani yao wakipingana wenyewe kwa wenyewe. Walioona kwa Mungu hakuwatoshi nao wakaanzisha dini zao lakini nao hawakuishia pema..ni mitufuano tuu...!!!Kila dini sasa bila kujali ni ya kumtaja Mungu mmoja ama miungu wakawa na mitume na manabii wao.. Na kila dini inawaheshimu na kuwatii sana sana

Ni kupitia michakato hiyo ya kidini kujitangaza na kutaka kukubalika zaidi ndani ya jamii mbalimbali duniania...Dini imejikuta kwenye mtanziko mkubwa wa mambo mabaya kabisa duniani.

Ni kwa kupitia dini hizo mamilioni wamepoteza maisha yao kwa vita ya kidini ama kuuawa kwenye mabishano ya kidini.

Ni kupitia dini hizo watu kwa maelfu wamepotea na kupotezwa na wasionekane tena.

Ni kupitia dini hizo mamilioni ya watu duniani wamepitia madhila na mateso makubwa sana.

Ni kupitia dini hizo mamilioni ya watu duniani, wameteswa, wamenyanyaswa na kudhalilishwa kwa kiwango kisichomithilika
Dini badala ya kuwa suluhisho imegeuka kuwa jinamizi litishalo ndani ya jamii mbalimbali

Ushirikina haujawahi kufanya mambo mabaya hivyo kama yaliyofanya kwa kutumia dini...lakini ushirikina unatumiwa vibaya na wanadini kama pitio na kimbilio la kutupia lawama na mabaya yote kuficha madhaifu yao kwenye dini

Inachekesha mno kiongozi wa dini anaposimama kwenye madhabahu na kuanza kukemea ushirikina kumbe jana yake tu alikuwa huko ama naye ni agent na muumini mwaminifu wa ushikirikina.. Viongozi wa dini zote hizi zinazoamini katika Mungu mmoja ndio kundi linaloongoza kwa kwenda kwa waganga wa kienyeji na ni waumini wakubwa wa ushirikina..!

Kila nikipima haya mawili katika mizania ya haki bado USHIRIKINA una nafuu kubwa katika uhalisia wake kuliko hiki kitu kizuri kiitwacho dini!
Enlightened beliefs
Primitive way of believing!

Deduced facts vs confusive facts!!

But to be more realistic-Mshana has built up a case to debate!
 
Shukrani kwa wito. Ila kabla sijaendelea mbali zaidi,jambo ulilo liandika linapaswa zaidi ulielezee kwa ushahidi na si kama ulivyo fanya wewe.

Swali la kwanza ni Ushirikina ni nini na ipi historia yake ?

Swali la pili ni Dini ni nini ?
Swali la kwanza kuhusu ushirikina nadhani tumeshajadili sana kule
Swali la pili kuhusu dini nimeshalijibu kwenye mada kuu.. Hebu chukua muda kuisoma tena tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ni uongo wa kauli na matendo au unaidanganya nafsi yako.

Huwezi kuwa mshika dini ukawa mshirikina,sababu ushirikina unakutoa katika dini hasa dini ya Uislamu.

Swali langu ni Wewe ni dini gani na dhehebu gani na kwanini upo kwenye dini hiyo na dhehebu hilo ?
Haya ni maslahi yangu kiroho na nilitangaza kabla mwanzoni kabisa mwa post... Sasa ukinibishia na kusema ni uongo nitashindwa kukuelewa
Mimi kuwa na imani yangu na dini yangu hakunizuii kujadili madhaifu yangu yake labda tu nikubali kukaa ndani ya duara nisihoji chochote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushirikina wenyewe ni jambo baya,vipi ufanye baya lingine zaidi yake.

Kwanza tujikite katika usuli,huku ndiyo mambo huzalikana,ushirikina ni nini ?
Nimesema tukilinganisha haya mawili kwenye mizania ya haki dini ina mabaya mengi kuliko ushirikina..na mifano hai nimetoa
Ushirikina ni mkusanyiko wa uchawi, ulozi, uganga wa kienyeji, na mambo yote yanayofanana na hayo bila kusahau kuwanga..!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa waktisto Mungu hapiganiwi dini sababu biblia inatamka vita ni ya Bwana sio mwanadamu Istael walimshinda farao na jeshi lake hila kurusha hata jiwe au kofi.Wasio na Mungu ndio utasikia napigania mwenyezi Mungu
Ushawahi kwenda kwa whitchdoctor!
Najua utasema hapana,lakini ukweli unaujua
Mwenyewe!

Ova
 
Back
Top Bottom