Dini vs Ushirikina: Kwanini ningechagua ushirikina

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,780
Maslahi yangu kiroho: mimi ni mshika dini kwa imani na dhehebu langu na nina hofu na Mungu

Dini ni njia buniwa ya mwanadamu ya kumtafuta Mungu iliyoshindwa vibaya kabisa; chochote afanyacho mwanadamu chini ya jua hakina ukamilifu wa kimungu kwakuwa mwanadamu mwenyewe si mkamilifu.

Ni katika kutengeneza huo mfumo uitwao dini binadamu anajikuta anajichanganya mwenyewe ama kutofautiana na mwenzake, ama kabila na kabila, imani na imani. Kufikia hapo ndio zikaanza kufumuka dini na imani za kila aina.

Wanaomtaja na kumwamini Mungu wakawa na dini zao nyingi tu lakini ndani yao wakipingana wenyewe kwa wenyewe. Walioona kwa Mungu hakuwatoshi nao wakaanzisha dini zao lakini nao hawakuishia pema, ni mitufuano tu. Kila dini sasa bila kujali ni ya kumtaja Mungu mmoja ama miungu wakawa na mitume na manabii wao. Na kila dini inawaheshimu na kuwatii sana sana.

Ni kupitia michakato hiyo ya kidini kujitangaza na kutaka kukubalika zaidi ndani ya jamii mbalimbali duniania. Dini imejikuta kwenye mtanziko mkubwa wa mambo mabaya kabisa duniani.

Ni kwa kupitia dini hizo mamilioni wamepoteza maisha yao kwa vita ya kidini ama kuuawa kwenye mabishano ya kidini.

Ni kupitia dini hizo watu kwa maelfu wamepotea na kupotezwa na wasionekane tena.

Ni kupitia dini hizo mamilioni ya watu duniani wamepitia madhila na mateso makubwa sana.

Ni kupitia dini hizo mamilioni ya watu duniani, wameteswa, wamenyanyaswa na kudhalilishwa kwa kiwango kisichomithilika
Dini badala ya kuwa suluhisho imegeuka kuwa jinamizi litishalo ndani ya jamii mbalimbali

Ushirikina haujawahi kufanya mambo mabaya hivyo kama yaliyofanya kwa kutumia dini, lakini ushirikina unatumiwa vibaya na wanadini kama pitio na kimbilio la kutupia lawama na mabaya yote kuficha madhaifu yao kwenye dini.

Inachekesha mno kiongozi wa dini anaposimama kwenye madhabahu na kuanza kukemea ushirikina kumbe jana yake tu alikuwa huko ama naye ni agent na muumini mwaminifu wa ushikirikina.. Viongozi wa dini zote hizi zinazoamini katika Mungu mmoja ndio kundi linaloongoza kwa kwenda kwa waganga wa kienyeji na ni waumini wakubwa wa ushirikina!

Kila nikipima haya mawili katika mizania ya haki bado USHIRIKINA una nafuu kubwa katika uhalisia wake kuliko hiki kitu kizuri kiitwacho dini!
 
Hii ni ngumu sana kumeza labda uwe na roho km ya Mshana..hapa panahitaji watu wenye kalama ili kumbadili huyu mwamba...
In terms of mambo mabaya kwa wakati mmoja na yaliyoangamiza watu wengi kwa mara moja uchawi unasubiri mbele ya dini
Tumeshuhudia si mara moja au mbili vita vya kidini vilivyoondoka na roho za malaki wasio na hatia... Je ni wapi umewahi kusikia ushirikina ukiuwa kwa halaiki?
 
Sijui kwanini tunahukumu sana kwenda kwa waganga mkuu? It's the African way of life mpaka mzungu na mwarabu alipokuja kuharamisha. Tuwe proud na mila na tamaduni zetu,sioni shida kwenda kwa mganga as long as siendi kumfanyia mtu ubaya bali kutatua changamoto zangu. Wahindi wamebaki na tamaduni zao,wakorea,wajapani maisha yanasonga ili sisi waafrika tunateseka kweli.
 
Maslahi yangu kiroho: mimi ni mshika dini kwa imani na dhehebu langu na nina hofu na Mungu

Dini ni njia buniwa ya mwanadamu ya kumtafuta Mungu iliyoshindwa vibaya kabisa..chochote afanyacho mwanadamu chini ya jua hakina ukamilifu wa kimungu kwakuwa mwanadamu mwenyewe si mkamilifu
Ni katika kutengeneza huo mfumo uitwao dini binadamu anajikuta anajichanganya mwenyewe ama kutofautiana na mwenzake, ama kabila na kabila, imani na imani... Kufikia hapo ndio zikaanza kufumuka dini na imani za kila aina

Wanaomtaja na kumwamini Mungu wakawa na dini zao nyingi tu lakini ndani yao wakipingana wenyewe kwa wenyewe... Walioona kwa Mungu hakuwatoshi nao wakaanzisha dini zao lakini nao hawakuishia pema..ni mitufuano tuu...!!!Kila dini sasa bila kujali ni ya kumtaja Mungu mmoja ama miungu wakawa na mitume na manabii wao.. Na kila dini inawaheshimu na kuwatii sana sana

Ni kupitia michakato hiyo ya kidini kujitangaza na kutaka kukubalika zaidi ndani ya jamii mbalimbali duniania...Dini imejikuta kwenye mtanziko mkubwa wa mambo mabaya kabisa duniani
Ni kwa kupitia dini hizo mamilioni wamepoteza maisha yao kwa vita ya kidini ama kuuawa kwenye mabishano ya kidini
Ni kupitia dini hizo watu kwa maelfu wamepotea na kupotezwa na wasionekane tena
Ni kupitia dini hizo mamilioni ya watu duniani wamepitia madhila na mateso makubwa sana
Ni kupitia dini hizo mamilioni ya watu duniani, wameteswa, wamenyanyaswa na kudhalilishwa kwa kiwango kisichomithilika
Dini badala ya kuwa suluhisho imegeuka kuwa jinamizi litishalo ndani ya jamii mbalimbali

Ushirikina haujawahi kufanya mambo mabaya hivyo kama yaliyofanya kwa kutumia dini...lakini ushirikina unatumiwa vibaya na wanadini kama pitio na kimbilio la kutupia lawama na mabaya yote kuficha madhaifu yao kwenye dini

Inachekesha mno kiongozi wa dini anaposimama kwenye madhabahu na kuanza kukemea ushirikina kumbe jana yake tu alikuwa huko ama naye ni agent na muumini mwaminifu wa ushikirikina.. Viongozi wa dini zote hizi zinazoamini katika Mungu mmoja ndio kundi linaloongoza kwa kwenda kwa waganga wa kienyeji na ni waumini wakubwa wa ushirikina..!

Kila nikipima haya mawili katika mizania ya haki bado USHIRIKINA una nafuu kubwa katika uhalisia wake kuliko hiki kitu kizuri kiitwacho dini....!


Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi naelewa hivi:
1. Mungu anajifunua kwetu (kwa njia mbalimbali)
2. Tunampokea Mungu kwa i) imani (kama nikitumia mchoro ni mstari wa wima) na ii) wakati huo huo tunatambua kuwa tunaishi na watu wengine katika jumuia na hivyo tunamwendea Mungu kwa pamoja (kuliko mtu binafsi) (kama nikitumia mchoro ni mstari wa mlalo).
3. Hivyo basi, imani is inner expression of our response to God's love/revelation na dini is the external expression of our faith in God. Na imani msingi wake ni trust. Mfano, ukiondoka nyumbani kwenda kazini (ofisini/kwenye biashara) muda wote unapokuwa huko unaamini kwamba ulivyotoka nyumbani asubuhi na sasa unarudi jioni utakuta familia yako/nyumba/mali/mazingira/barabara etc kama ulivyoviacha na imani hiyo hiyo itakufanya utumie aina ya usafiri unaofika huko kwa sababu unaamini ndio utakaokufikisha nyumbani. Pia ukifungua kabati ulikotunza nguo zako unaamini pia utazikuta kama zilivyo na hata utaamini ufunguo unaotumia ndio unaofungua kabati na swichi unayotumia ndiyo itakayowasha umeme na ukilala unaamini pia kesho utaamka ukiwa mzima na kabla ya yote utavaa nguo ambazo unaaminini ni zako na siyo za mwingine etc. Sasa katika yote haya kama kufanya hivyo ndiyo ushirikina, then nitaamini kuwa ushirikina ndio una nafuu kubwa katika uhalisia kuliko dini. Hata kwa wazazi tunaamini ndio waliotuzaa, lakini we don't have any idea how we were born. We don't have any idea how we looked like at the time we were born. We don't know also what size we were at and how we grew to reach the size we have or the age we are at now.
 
Mimi naelewa hivi:
1. Mungu anajifunua kwetu (kwa njia mbalimbali)
2. Tunampokea Mungu kwa i) imani (kama nikitumia mchoro ni mstari wa wima) na ii) wakati huo huo tunatambua kuwa tunaishi na watu wengine katika jumuia na hivyo tunamwendea Mungu kwa pamoja (kuliko mtu binafsi) (kama nikitumia mchoro ni mstari wa mlalo).
3. Hivyo, basi imani is inner expression of our response to God's love/revelation na dini is the external expression of our faith in God. Na imani msingi wake ni trust. Mfano, ukiondoka nyumbani kwenda kazini (ofisini/kwenye biashara) muda wote unapokuwa huko unaamini kwamba ulivyotoka nyumbani asubuhi na sasa unarudi jioni utakuta familia yako/nyumba/mali/mazingira/babarabara etc kama ulivyoviacha na imani hiyo hiyo itakufanya utumie aina ya usafiri unaofika huko kwa sababu unaamini ndio utakaokufikisha nyumbani. Pia ukifungua kabati ulikotunza nguo zako unaamini pia utazikuta kama zilivyo na hata utaamini ufunguo unaotumia ndio unaofungua kabati na swichi unayotumia ndiyo itakayowasha umeme na ukilala unaamini pia kesho utaamka ukiwa mzima na kabla ya yote utavaa nguo ambazo unaaminini ni zako na siyo za mwingine etc. Sasa katika yote haya kama kufanya hivyo ndiyo ushirikina, then nitaamini kuwa ushirikina ndio una nafuu kubwa katika uhalisia kuliko dini. Hata kwa wazazi tunaamini ndio waliotuzaa, lakini we don't have any idea how we were born. We don't have any idea how we looked like at the time we were born. We don't know also what size we were at and how we grew to reach the size we have or the age we are at now.
Hivyo, basi imani is inner expression of our response to God's love/revelation na dini is the external expression of our faith in God. Na imani msingi wake ni trust Magobe T nitakurejea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom