Difference between AC and DC currents

Dr Dre

JF-Expert Member
May 23, 2015
2,556
2,585
Wakuu habari zenu ,naomba ufafanuzi wa tofauti kati ya umeme wa dc na ac ,kwamaana kuna watu hapa wanabishana kweli wengine wanasema dc ndiyo unaotumika kucharge cm wengine wanabisha ,pia je umeme wa tanesco ni ac au dc ,na wa sola je nao ni dc au ac?,na unaotumika ndani ya cm ni upi?
 
Wakuu habari zenu ,naomba ufafanuzi wa tofauti kati ya umeme wa dc na ac ,kwamaana kuna watu hapa wanabishana kweli wengine wanasema dc ndiyo unaotumika kucharge cm wengine wanabisha ,pia je umeme wa tanesco ni ac au dc ,na wa sola je nao ni dc au ac?,na unaotumika ndani ya cm ni upi?

dc maana yake direct current, ac ni alternating current. Current ni mtiririko wa chembe chembe ziitwazo electrons kwenye nyaya. dc mtitiriko ni mbele kwa mbele bali ac mtiriko ni mbele nyuma wastani mara 50 kwa sekundi. Umeme wa kuchagi cm dc baada ya kugeuzwa kutoka ac na charger. umeme wa solar ni dc hata hivo unawe kugeuzwa na convertor kuwa ac. Umeme wa tanesco ni ac.
 
Mkuu simplemind nadhani kakupa majibu labda cha kuongezea Simu inaweza chargiwa kwa both ac au dc itategemea na chazo cha pawa ulichonacho ila tu simu inatumia battery ambayo ina supply Direct current yani Dc kwa solar panel,Battery na Dynamo umeme wake ni Dc na alternator ambayo ni Generator inayofua Ac zipo pia za Dc izo generator ila Tanesco wana supply Ac

Labda kwa kifupi tukisema Dc na Ac tunaa maanisha nini Ac ni mtiririko wa umeme katika directon tofauti yani to na fro au mbele na nyuma electrons zina flow ivo but kwa Dc yenyewe zina flow mbele tuu. uploadfromtaptalk1447012394917.png
 
Wakuu...maelezo yote nimeyapenda ila ninapata shida ya lugha mnayotumia kuelezea hizo AC na DC.

Mnaposema AC inakwenda mbele nyuma, DC mbele kwa mbele mnamaanisha nini??? Na hasa hiyo mbele nyuma.

Alternating Current(AC) - Mkondo geu
Direct Current(DC) - Mkondo mnyoofu.

Nadhani AC inapotumika kuwasha balbu ile kama mtungi yenye filament, balbu huwaka na kuzima mara 50 kwa sekunde moja, hii ni kwa mfumo wa TZ na baadhi ya nchu tutumiazo 50Hz.

DC inapotumika kuwasha balbu iliyo kama mtungi, balbu itawaka bila kuzima kwa muda itakayokuwa imeungwa kwenye chanzi cha DC.

Sehemu kubwa ya vifaa vya electronics vinatumia DC supply i.e TV, Radio, Simu, n.k Unaweza ona supply ya TANESCO ndio inayoingia kwenye vifaa vyako(Tanesco ina-supply AC) ila kimsingi ni kwasababu si ghali sana kusambaza AC kama ilivyo DC, hivyo vifaa vingi vya electronics vinapokea AC kwa TRANSFORMER, AC inapoozwa pengine kutoka 240VAC mpaka 24V au 12VAC kwa transformer kisha unapitishwa kwenye RECTIFIERS(Diodes) zilizoungwa na capacitor kwaajili ya kubadili kutoka AC kwenda DC kisha kutumika ndani ya kifaa husika kama ni radio au chochote.

Umeme wa DC unahifadhika, AC hauhifadhiki.

Nadhani hiyo pia itasaidia kuelezea hiyo tofauti ya AC na DC.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom