zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 19,039
- 28,689
UTANGULIZI
Habari za jioni wana jukwaa pendwa kufuatia maoni kwenye huu uzi
Wafahamu viumbe watatu wa kutisha wa baharini - JamiiForums kuna baadhi ya watu walinitaka niandae uzi maalum ili niweze kuelezea viumbe hivi vyenye utata kidogo kwenye Biblia. kama kawaida natoa rai uzi huu ni kwa minajili ya kujifunza tu na kujadiliana ili tuweze kuongeza maarifa ila sio uwanja wa mabishano ya kidini so sitegemei kejeli,matusi dhidi ya dini za watu wala vitabu vya dini ya yeyote.
NB: uzi huu nimeugawa katika post mbili ili iwe rahisi kusomeka na isichoshe msomaji
Kwa kusema hayo sasa tunaweza kuendelea.
UNICORN
Neno hili limetokana na neno re'em kiebrania na kigiriki MONOC’EROS ambalo kwa hapo nyuma ilifahamika kama farasi mkubwa sana mwenye pembe moja ya mbele ambaye anatazamiwa kuwa na nguvu sana kuliko wanyama wengi. Anazungumziwa kwenye Hesabu 23:22 na 24:8, ambapo Biblia inafananisha nguvu za Mungu kama nguvu za Unicorn hapa duniani.
Pia kumb. La torati 33:17, zaburi 22: 21 na 92:10 yanaongelea pembe la huyo unicorn ilivyo na nguvu.
Pia Ayubu 9:10 na 39:10 zote zinaongelea jinsi ilivyo ngumu kumkamata mnyama huyu.
Kuna wengine watasema kwamba tunasoma biblia kama gazeti ila hapa biblia iko wazi kabisa kupitia Isaya 34:17 kuwa Unicorn alikuwa mnyama na imemuweka hapa kundi moja na wanyama wengine kama ng'ombe hivyo sio lugha ya picha kabisa.
Ingawa hakuna ushahidi wa kisayansi wa farasi wenye pembe yaani unicorns ila kuna vifaru wa huko siberia,Urusi ambao kisayansi wanatajwa kuwahi kuwepo hapa duniani hivyo kuna baadhi wanasema huenda ndio unicorns walioongelewa kwenye Biblia!!
DRAGONS
Dragons wameongelewa kwenye Isaya 43:20,34:14 na Micah 1:8 kama mnyama mkali ,hatari na anayenguruma huko porini. Pia isaya 91:13 na 27:1 pia zinamzungumzia kama kiumbe anayetawala na baharini pia kwa utisho mkubwa. Kiebrania jina lililotumika ni Tannin likimaanisha mnyama wa jamii kama joka ila lina miguu na mabawa. Kuna watu pia wanaweza sema ni lugha ya picha ila Isaya 13:21-22 inataja kikundi cha wanyama ambao mpaka leo wapo na mmoja anayetajwa ni Dragon hivyo sitegemei hoja hii itumike, ila swali ni je mnyama huyu amewahi kuwepo duniani na kama ametoweka nini kilisababisha??
COCKATRICE
Ni mnyama jamii ya nyoka ila ana kiwiliwili cha jogoo yaani nusu jogoo nusu nyoka na anatajwa kwenye biblia Cockatrice anatajwa kwenye isaya 11:8, 59:5,14:29. Jina lake kwenye Biblia limetokana na neno la kiebrania tse-pha ambalo kwenye kamusi ya kiebrania linazungumziwa kama Joka lenye mwili wa kuku ambalo ukiliangalia tu unakauka na jinsi pekee ya kuliua ni kulireflect yaani kama kutumia kioo au chochote kitakachomfanya ajiangalie mwenyewe. Ingawa hakuna ushahidi wa kisayansi wa uwepo wake ila amezungumziwa sana kwenye maandiko. Mfano hapa katajwa kwenye mfano huu wa Nabii Isaya juu ya wafilisti.
Isaya 14:29
29 Usifurahi, Ee Ufilisti, pia wote,Kwa sababu fimbo ile iliyokupiga imevunjika;Maana katika shina la nyoka atatoka fira,Na uzao wake ni joka la moto arukaye (Dragon kwa bible ya kingereza)
SATYR
Neno hili kwenye biblia limetokana na jina la kiebrania sa'iyr ambalo kwenye kamusi ya kiebrania walikuwa viumbe ambao walikuwa ni jamii ya watu lakini wana kiwiliwili cha farasi au mbuzi yaani nusu mtu nusu farasi. Kwenye Biblia wanatajwa kwenye kitabu cha Isaya 13:21 na 34:14 kama viumbe wa porini na ambao Nabii Isaya alitabiri kuwa ufalme wa Babeli utaangushwa siku moja na kwenye mfano huo akaeleza kwamba hatoishi mtu bali wanyama wa mwituni kama simba,bundi na huyo SATYR kwahiyo mpaka hapa inaonyesha haikuwa lugha ya picha tu bali Isaya aliongelea mnyama ambaye alimfahamu na kumsikia ndio maana akamtolea mfano.
Isaya 13:21
21 Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini (satyr) watacheza huko.
Did they exist??
Habari za jioni wana jukwaa pendwa kufuatia maoni kwenye huu uzi
Wafahamu viumbe watatu wa kutisha wa baharini - JamiiForums kuna baadhi ya watu walinitaka niandae uzi maalum ili niweze kuelezea viumbe hivi vyenye utata kidogo kwenye Biblia. kama kawaida natoa rai uzi huu ni kwa minajili ya kujifunza tu na kujadiliana ili tuweze kuongeza maarifa ila sio uwanja wa mabishano ya kidini so sitegemei kejeli,matusi dhidi ya dini za watu wala vitabu vya dini ya yeyote.
NB: uzi huu nimeugawa katika post mbili ili iwe rahisi kusomeka na isichoshe msomaji
Kwa kusema hayo sasa tunaweza kuendelea.
UNICORN
Neno hili limetokana na neno re'em kiebrania na kigiriki MONOC’EROS ambalo kwa hapo nyuma ilifahamika kama farasi mkubwa sana mwenye pembe moja ya mbele ambaye anatazamiwa kuwa na nguvu sana kuliko wanyama wengi. Anazungumziwa kwenye Hesabu 23:22 na 24:8, ambapo Biblia inafananisha nguvu za Mungu kama nguvu za Unicorn hapa duniani.
Pia kumb. La torati 33:17, zaburi 22: 21 na 92:10 yanaongelea pembe la huyo unicorn ilivyo na nguvu.
Pia Ayubu 9:10 na 39:10 zote zinaongelea jinsi ilivyo ngumu kumkamata mnyama huyu.
Kuna wengine watasema kwamba tunasoma biblia kama gazeti ila hapa biblia iko wazi kabisa kupitia Isaya 34:17 kuwa Unicorn alikuwa mnyama na imemuweka hapa kundi moja na wanyama wengine kama ng'ombe hivyo sio lugha ya picha kabisa.
Ingawa hakuna ushahidi wa kisayansi wa farasi wenye pembe yaani unicorns ila kuna vifaru wa huko siberia,Urusi ambao kisayansi wanatajwa kuwahi kuwepo hapa duniani hivyo kuna baadhi wanasema huenda ndio unicorns walioongelewa kwenye Biblia!!
DRAGONS
Dragons wameongelewa kwenye Isaya 43:20,34:14 na Micah 1:8 kama mnyama mkali ,hatari na anayenguruma huko porini. Pia isaya 91:13 na 27:1 pia zinamzungumzia kama kiumbe anayetawala na baharini pia kwa utisho mkubwa. Kiebrania jina lililotumika ni Tannin likimaanisha mnyama wa jamii kama joka ila lina miguu na mabawa. Kuna watu pia wanaweza sema ni lugha ya picha ila Isaya 13:21-22 inataja kikundi cha wanyama ambao mpaka leo wapo na mmoja anayetajwa ni Dragon hivyo sitegemei hoja hii itumike, ila swali ni je mnyama huyu amewahi kuwepo duniani na kama ametoweka nini kilisababisha??
COCKATRICE
Ni mnyama jamii ya nyoka ila ana kiwiliwili cha jogoo yaani nusu jogoo nusu nyoka na anatajwa kwenye biblia Cockatrice anatajwa kwenye isaya 11:8, 59:5,14:29. Jina lake kwenye Biblia limetokana na neno la kiebrania tse-pha ambalo kwenye kamusi ya kiebrania linazungumziwa kama Joka lenye mwili wa kuku ambalo ukiliangalia tu unakauka na jinsi pekee ya kuliua ni kulireflect yaani kama kutumia kioo au chochote kitakachomfanya ajiangalie mwenyewe. Ingawa hakuna ushahidi wa kisayansi wa uwepo wake ila amezungumziwa sana kwenye maandiko. Mfano hapa katajwa kwenye mfano huu wa Nabii Isaya juu ya wafilisti.
Isaya 14:29
29 Usifurahi, Ee Ufilisti, pia wote,Kwa sababu fimbo ile iliyokupiga imevunjika;Maana katika shina la nyoka atatoka fira,Na uzao wake ni joka la moto arukaye (Dragon kwa bible ya kingereza)
SATYR
Neno hili kwenye biblia limetokana na jina la kiebrania sa'iyr ambalo kwenye kamusi ya kiebrania walikuwa viumbe ambao walikuwa ni jamii ya watu lakini wana kiwiliwili cha farasi au mbuzi yaani nusu mtu nusu farasi. Kwenye Biblia wanatajwa kwenye kitabu cha Isaya 13:21 na 34:14 kama viumbe wa porini na ambao Nabii Isaya alitabiri kuwa ufalme wa Babeli utaangushwa siku moja na kwenye mfano huo akaeleza kwamba hatoishi mtu bali wanyama wa mwituni kama simba,bundi na huyo SATYR kwahiyo mpaka hapa inaonyesha haikuwa lugha ya picha tu bali Isaya aliongelea mnyama ambaye alimfahamu na kumsikia ndio maana akamtolea mfano.
Isaya 13:21
21 Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini (satyr) watacheza huko.
Did they exist??