PARADIGM
JF-Expert Member
- Sep 9, 2014
- 2,774
- 1,829
Huyo.mtu mliachana ingawa hujaeleza nani alimuacha mwenzake. Ghafla umemuibukia, ulitegemea akwambie nini? Kama angeanza yeye kukwambia hivyo bila wewe kumtumia sms angekuwa anamaanisha hivyo. Ila we baada ya kukaa muda mrefu umemkumbuka na inaonekana baso unampenda. Kwahiyo ndiyo maana kila wakati unataka kusikia unachotaka kusikia. Je mlikaa tena kumaliza tofauti zenu baada ya kutengana. Kama si hivyo basi huyo ana mtu wake na hataki kujiingiza kwenye mawasiliano yatakayomgharimu uhusiano wake kwa mtu wake wa sasa. Kwahiyo wewe tafuta mtu uolewe la sivyo mtafute mkutane ana kwa ana akupe msimamo wake inagawa nadhani hautakuwa positive kama unavyotaka.