lyasi
JF-Expert Member
- Sep 23, 2015
- 362
- 383
Kwa mziki wa kitanzania asikudanganye mtu juu ya uhusika wa the late Ruge, ukiwa karibu na watu walioko kwenye industry hii ndo wanajua umuhimu wake katika mafanikio ya msanii mmoja mmoja. The man was born tactics and strategist.Yaani watu mnavyomu-overate Ruge!! Hivi baada ya Nenda Kamwambie, ikaja Mbagala ikafuata Nitarejea iliyokuwa ndani ya albamu halafu bado mnataka kutuaminisha ni Ruge ndie alimtangaza Diamond?!
Diamond akiwa mpya kabisa, akapata mchongo wa kuzunguka Tanzania mzima na CCM huku mwaka huo huo akizoa tuzo za kutosha za akili lakini bado mnataka kutuaminisha hiyo ilikuwa ni kazi ya Ruge?!
Swali ambalo sasa cjajibiwa ni moja! Hivi huyu Ruge ambae alikuwa na uwezo mkubwa kiasi hicho kwanini hadi kifo chake alishindwa kufanya hayo kwa Barnaba ambae uwezo wake kila mtu anaujua?!
Guys, acheni uongo! Ruge kaanza kujipeleka kwa Diamond wakati Diamond tayari keshakuwa lulu! Nasema kujipeleka kwa sababu THT iliyokuwa chini ya Ruge iliwahi kumkataa Diamond kwa hoja kwamba hajui kuimba!!
Kuhusu kuondoka Harmonize WCB, ni mtu wa ajabu tu ndie atapinga kuondoka kwake! Mimi binafsi, aondoke asiondoke hanipunguzii chochote kwa sababu mimi sio shabiki wake! Na tatizo langu kwake namuona ni kama copy tu ya Diamond kwa kila kitu, kuanzia kuimba hadi lifestyle!!
Hata hivyo nimekuwa too concerned na uondokaji wake, hoja ikiwa ni: Anaondoka kwa sababu anaamini anakoenda kutamwendeleza zaidi kwa career yake au anaondoka kwa kuvimba tu na kujiona yeye ni mkubwa!
Kama anaondoka kwa kuvimba tu na kujiona he's too big basi atakuwa stupid manake hata wasanii wakubwa duniani na wenyewe wapo chini ya label!. This is not about being TOO BIG au kuwa mkali kwenye mic bali uwezo wa wanaomuzunguka kwenye tasnia mzima ya muziki!