Diamond Platnumz atua na Rolls Royce 2021

Franky Samuel

JF-Expert Member
Oct 10, 2018
4,912
12,988
Hayawi hayawi sasa yamekuwa. Hili ndilo gari jipya la diamondplatnumz. Ni Rolls Royce 2021. Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika inatajwa kuwa gari hili limeingia Tanzania siku za hivi karibuni

Inasemekana gari hili Rolls Royce 2021 imemgharimu #Diamond zaidi ya Shilingi Bilioni Moja za Kitanzania. Rolls Royce 2021 itaungana na magari mengine mawili ya kifahari #Cadillac ambayo Diamond ameyanunua mwaka huu

Good News ni kwamba Diamond mwenyewe ameshatua Tanzania akitokea nchini Marekani ambapo alikuwa kwenye shughuli za kimuziki

=======


Diamond-Platnumz.jpg

Staa wa Muziki Barani Afrika na CEO wa #WasafiMedia, SIMBA @diamondplatnumz ameamua kuvuta Ndinga ya ndoto yake Rolls Royce Cullinan SUV ya Mwaka 2021.

Gari hiyo yenye thamani zaidi ya Dola Za Kimarekani 650,000 (Tsh . Bilioni 1.5 kabla ya Ushuru), imepokelewa leo Kutoka Bandarini na Staa huyo baada ya kuiagiza tangu Mwezi uliopita.

Diamond alishawahi kuweka wazi muda mrefu kuwa Gari ya ndoto zake ni @rollsroycecars, hivyo sasa anaweza kulala usingizi Mnono kwasababu ametimiza moja ya ndoto zake.

Hii inakua Gari ya 3 ya kifahari kwa @diamondplatnumz kununua ndani ya Kipindi cha Miezi Miwili baada ya Kuvuta Cadillac Escalades mbili Wiki kadhaa zilizopita.

Big Congratulations kwa SIMBA !

Chanzo: Wasafi Media
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom