Diamond - Mdogomdogo (Video na Lyrics)

Diamond - Mdogomdogo (Video na Lyrics)

As long as hajaimba matusi sio mbaya kuisikiliza, midundo haiwez fanya nyimbo iwe ya kipuuzi. Diamond hajawahi kuwa nje na jamii yake siku zote ye ni mswahili tu kama sio kwa nyimbo zake basi kwa matendo yake.
 
Kuna KaTrend Kanaendelea.....Vanessa Mdee Na Hawajui,Diamond Na Hii Na Shaa Alishatangulia Na Sugua Gaga.......I'm Not A Fan Of Mchiriku Au Mnanda BUT On A Serious Note,This Was What We Miss From Our Industry.........Owning Up Every Genre In Our Culture.....

truee that watu wanataka tuwe tuna copy tuu miaka yote
 
Alie andika script ya hii video ni mkali sana. Namkubali hata kama sijui ni nani.
Hapa kimataifa wataangalia zaidi quality ya Video ila Audio yake si nzuri kwa wastaarabu, ukiipeleka mbagala mbona wanakula zakutosha sana

nyiee mnavunga wazungu kumbe mmnaishi tandale jivunieni id yenu
 
Acha niipe mda...labda itakuwa kama ya "my no 1"...so far...well its just okay...BRAVO FOR THE VIDEO..
 
nimesikitika sana video ya ukweli halafu wimbo wa kipuuzi

Hata MY NUMBER ONE mliuponda hivohivo.In short sijawahi ona Diamond ametoa wimbo halafu usipondwe,but mwisho wa siku watu wanaziba midomo baada ya mafanikio ya wimbo
 
nashindwa kuelewa mtu anaposema natoa wimbo kwa ajili ya soko la kimataifa....ngoma ikiwa kali hata ukiimba kiyao au kichaga itasikilizwa na kila mtu!huu ni uoga!hii kasumba ndo inayompoteza AY katika ramani ya mziki na anajikuta anatumia pesa nyingi kuandaa mziki wake kuliko anachokipata!diamond asipoangalia hali hii itamkuta!ile ngoma yake mdogo mdogo ni jiwe tosha haikumpasa kutoa na hii!.......nachokiona sasa kwa diamond ni wapishi wengi ambao wanaelekea kuharibu mchuzi!babu tale hawezi kumpelekea diamond kimataifa kwani soko la kimataifa halihiitaji fitna kama soko la nyumbani ambalo babu tale na said fella wamelishika!.....kama inshu ni kuzidi kuliteka soko la kimataifa namshauri apate ushauri toka kwa AY ambaye alijaribu ingawa hakufanikiwa ila njia anazijua ambazo kwa mziki wa diamond atatoboa!......mbinu watumiayo kina babu talle ni SPEND!SPEND!SPEND!...hii inapoelekea itamcost diamond!.........kwa maono yangu baada ya kusikia na kuona hizi ngoma zake mbili naona diamond amefika kikomo!ushauri wangu!kwakuwa amewahi kutoa hits nyingi huu ni muda wa kujifunza kuimba live asijisahau sana stejini kucheza tu kwani kinachomuokoa katika shows zake nyingi ni kwakuwa nyimbo zake zinapendwa na zinajulikana ila uimbaji live ni sifuri!
 
Kwan nyimbo zote mnazozisikiliza huwaga mnazielewa??mbna zngine za kihindi na kizuru bt mnaskiliza na kucheza!!!!!

Cjaelewa cjui beat limezidi maneno yanayotamkwa za kihindi hata sisikilizagi kitu nisichoelewa wamemeza sana maneno
 
Cjaelewa cjui beat limezidi maneno yanayotamkwa za kihindi hata sisikilizagi kitu nisichoelewa wamemeza sana maneno

Okey ngoja nikuambie kitu.muziki ni sanaa inayoitaji ubunifu,msanii anaweza kucheza na beat au mashahiri au akacheza na vyote kwa pamoja,inatagemea yeye na waongozaji wake wanataka nini.so kwa case ya daimond amecheza sana na beat.kama mfuatiliaj wa nyimbo za dancin hall za akina shaggy au bean man na wengine utaliona ilo.sometimes mashairi hayaeleweki bt beat linaonhea na nyimbo ina heat.so ni sanaa tu dadangu
 
I am a big big fan wa diamond, so kabla hamjaanza kunivamia ni make that clear.
Ukiangalia hii video ya mdogo mdogo kama ukitafakari utakuja gundua ni idea ya mwimbo wa AYE wa Davido.why?
Kwenye Aye davido kampenda mke wa mfalme huku diamond mtoto wa mfalme, zote zimetumia midundo ya asili, wameshoot in an african traditional environment.Japo diamond ka diversify kwa kuweka wazungu.Nadhani dangote baada ya kuona aye in mafanikio makubwa na ukiangalia ni miondoko ya kiafrica akaona isiwe tabu na yeye akaintroduce kigodoro
 
Aiseee Daimond hebu punguza kidogo utawaua watu, kuna mijitu humu ishaanza kutoa povu na mwaka huu lazima walazwe ICU kwa preshaa...hahahaha

Kumchukia Diamond ni sawa na kupaka rangi nzuri upepo.
 
nijuacho mim Matola n shabk mkubwa wa Diamond humu JF lakn kama na yeye kasema Mdogomdogo n wimbo wa kawaida bas najirdhsha kuwa ni wimbo wa kawaida kweli..

Jamaa kabugi,,hajafkia haja levo za FEROOZ-NDEGE MTINI..

ingawaje n bonge la video ila hata demu wangu kasema Diamond kaanza kufulia.

Naona povu linawatoka tu leo, jana mlisema Diamond aimbe mziki wa asili asicopy Nigeria sasa leo kafanya hivyo mnaanza kutapatapa..hahahaha
 
Last edited by a moderator:
Aiseee Daimond hebu punguza kidogo utawaua watu, kuna mijitu humu ishaanza kutoa povu na mwaka huu lazima walazwe ICU kwa preshaa...hahahaha

Kumchukia Diamond ni sawa na kupaka rangi nzuri upepo.

hii inanikumbusha hadithi ya mfalme aliyekuwa uchi lakini aliambiwa amependeza kwa sababu ya kupenda misifa hakujuwa yule tailoring hakumpima nguo yoyote bali alimwacha atembee uchi.
 
Naona povu linawatoka tu leo, jana mlisema Diamond aimbe mziki wa asili asicopy Nigeria sasa leo kafanya hivyo mnaanza kutapatapa..hahahaha

music wa asili wenyewe ni tatu nane, inafrica band, che mundugwao, kharid tongolanga na saida kaloli. wacha kujitowa ufahamu.
 
I am a big big fan wa diamond, so kabla hamjaanza kunivamia ni make that clear.
Ukiangalia hii video ya mdogo mdogo kama ukitafakari utakuja gundua ni idea ya mwimbo wa AYE wa Davido.why?
Kwenye Aye davido kampenda mke wa mfalme huku diamond mtoto wa mfalme, zote zimetumia midundo ya asili, wameshoot in an african traditional environment.Japo diamond ka diversify kwa kuweka wazungu.Nadhani dangote baada ya kuona aye in mafanikio makubwa na ukiangalia ni miondoko ya kiafrica akaona isiwe tabu na yeye akaintroduce kigodoro

Sasa huoni kama Davido ndio alicope mziki wa mchiriku huku kwetu? Lakini ndio ukampa tuzo cha ajabu Diamond naye kufanya mziki wa nyumbani watu povu limewatoka.
 
music wa asili wenyewe ni tatu nane, inafrica band, che mundugwao, kharid tongolanga na saida kaloli. wacha kujitowa ufahamu.

kwahiyo huo wimbo wa Mdogomdogo Diamond kacope Nigeria au bondeni?
 
hii inanikumbusha hadithi ya mfalme aliyekuwa uchi lakini aliambiwa amependeza kwa sababu ya kupenda misifa hakujuwa yule tailoring hakumpima nguo yoyote bali alimwacha atembee uchi.

Ukiskia bangi za kuvutia chooni ndo hizi! Na bado.
 
Back
Top Bottom