princess ariana
JF-Expert Member
- Aug 19, 2016
- 7,553
- 14,381
Salute kwake
hivi fiesta Dar mkisema anakuja Rihanna na kusema watakuepo wakina Lina tu?MosiOfThunder kama ambavyo wenyewe wa Zambia wanapenda kuliita hili tamasha ni kati ya matamasha makubwa Zambia na linafanyika kila mwaka chini ya wizara ya Utamaduni na kampuni ya Bewaries yaani kama inavyokua Fiesta huku kwetu na wana utaratibu wa kualika wasanii toka nje ya Zambia na safari hii ilikua atumbuize Tekno ila akashindwa kwenda dakika za mwisho ndio kijana wetu Diamonda akapata nafasi ya kwenda kama mbadala wa Tekno.
Tuache uwasilishaji mbovu wa habari ni aibu kama Tekno alivyokuja Fiesta Dar alafu akatangaze aliujaza uwanja wa Leaders wakati kulikua na timu kubwa ya wasanii wetu ambao wamewavuta hao watu hii ni sawa Diamond yeye alienda kama mualikwa naamini hata angeenda Kingwendu watu wa Zambia wangejazana kwenye tamasha lao maalumu ila tunadanganyana kua kijana wetu amejazana uwanja ingawa mwenyewe Diamond aliweka wazi kua anaenda kuungana na wasanii lukuki toka Zambia kwenye hilo tamasha ni sawa uwepo wake ni chachu lakini hata asingeenda asingepunguza idadi ya watu,kwenye ukweli tuwe tunaambiana tu sio vibaya ila pia Diamond ametuwakilisha vyema kwa classic show.
watasema Davido hakwenda!Kama walikuwa wanauwezo wa kujaza uwanja bila diamond walimualika wa nini kupoteza zaidi ya milioni 100 za bure? are you serious?
Wanatanzia tunapenda mafanikio lakini tunachukia waliofanikiwa
Mkuu nyingine hii hapa itafanyika DRC CONGO akijaza tena uwanja huko mtasema Tekno hakwenda
View attachment 503598
Acha uongo!!hiyo ratiba ya Diamond kwenda kupiga show huko Zambia alikuwa nayo tangia mwezi wa kwanza!!Tatizo lako akili yako inawaza Diamond na Kiba kwa kua wamewafundisha kuvaa suruali za kubana au pengine umri wako pia hawa watoto ndio wamekufanya upende muziki sasa nakushauri kajifunze kuhusu hilo tamasha jaribu ku-google attendence ya mwaka jana wakati wamelikwa Casper na Roberto ilikuaje na mwaka huu ilikuaje utajua hilo tamasha sio la mtu au msaani mmoja ndio maana nimesema hata angeenda Kingwendu asingepunguza wala kuongeza idadi ya watu kwa kua wizara yenyewe wanasimamia kuvuta watu kwenye utamaduni wao duh watoto wa siku hizi hata nguo za ndani mtakua mnavaa kuwafuata hao wanaongoza timu zenu Diamond na Kiba maana mtu akitoa maoni tu fast mnawahi uyu atakua timu flani kwa kifupi hao kuku wenu wawili wamenikuta naupenda muziki hata kabla hawajaruhusiwa na mama zao kuimba.
Rudi kwenye comment yangu ya mwanzo nionyeshe nilipomtaja uyu kaka yenu Kiba maana ishu ya Diamond sijui Kiba ameingiaje,itakua ni KICHAA 1st class siku Baraka the Prince ajisifie alijaza uwanja wa Nangwanda Sijaona wa Mtwara kwenye tamasha la Fiesta wakati waliotumbuiza walikua wengi wapo walioenda kumuona Blue na wengineo,narudia tena Diamond kwenye tamasha la MosiOfThunder hakua kwenye ratiba amepata zali baada ya yule mtoto Tekno kuthibitisha hatokwenda na hata angeenda Tekno tungekataa kama angetuambia kajaza ule uwanja wa golf maana kwenda au kutokwenda kwa Tekno hakujabali idadi ya wahudhuriaji duh walimu wana kazi kweli uko mashuleni FYI hiyo show nimeiona yote.