Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,224
- 26,039
Amani iwe nanyi wadau!
Leo napenda nitoe Elimu kwa watanzania juu ya propaganda za wana CCM kuwa yeyote anayempinga Raisi Magufuli ni kibaraka wa Mabeberu. Wanasema haya wakitaka kujenga picha kwa watanzania ( wadanganyika) kuwa ubeberu ni kama dhambi au jambo fulani ambalo halifai. Najua kwa watanzania wenzangu wengi wetu Elimu kwetu imekuwa shida na kwa sababu hiyo wanasiasa wamekuwa wakitumia kutokujua kwetu katulisha mambo ambayo wao wanataka tuyaamini. Wanafanya haya kwa maslahi yao ya kisiasa
Asili ya Ubeberu ni nini hasa?
Kwanza kwa watanzania wasiofahamu, Dunia ya leo inaongozwa na pande mbili zinazopigana kila kukicha kutawala Dunia.
Pande ya kwanza inaongozwa na Marekani na washirika wake hasa nchi za Ulaya Magharibi na Scandnavia yaaani Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Uholanzi, Canada, Sweden , Norway, Hispania, Ureno, Ubelgiji na washirika wao wengine. Hizi nchi zote zinaamini katika dhana ya maendeleo ya ubepari Yaani uhuru katika kuamua, kuwekeza na kumiliki.
Dhana hii hairuhusu serikali kukamata njia kuu za uchumi na inawapa nafasi watu binafsi kukamata njia kuu za uchumi. Dhana hii ina hatua yake ya juu ambayo wengi wanaiita kuwa Ubeberu. Kutokana na dhana ya ubepari/ ubeberu kuamini kwenye Uhuru wa watu katika maendeleo na kumiliki vitu nchi nyingi zenuw hii dhana raia wao wana maisha mazuri sana na wanaishi maisha ya kistaarabu sana na kuheshimiana.
Katika nchi hizi mtu unaweza kuwa tajiri wakati wowote kwa sababu kuna mifumo imara ya kuruhusu watu kukua kiuchumi na kimaisha ili mradi ufanye tu kazi na uwe na kipaji halali . Taasisi za hizi nchi ni imara na ndo zinawasimamia viongozi wa serikali. Viongozi hawana uimara kuzizidi taasisi zao. Na wakati wowote viongozi wanaweza kuwajibishwa.
Pande ya pili inaongozwa na Urusi na washirika wake ambao ni Venezuela, Cuba, Korea ya Kusini na nchi chache za ulaya ya mashariki. Hawa wanaamini kwenye ujamaa yani Sera ya serikali kumiliki njia zote kuu za uchumi. Nchi hizi haziamini kwenye Uhuru wa watu wao kwenye biashara, siasa, dini au maisha na hata ukiziangalia nyingi zimepiga Marufuku dini mbalimbali Tanzania Chama cha Mapinduzi nacho kinaamini kwenye Sera za ujamaa ingawa wao wanaamini kwenye uhuru wa dini Ila zile zinazokuwa chini ya uangalizi/ mkono wa serikali Mf. Bakwata.
Katika hizi nchi , nyingi raia wake wana maisha magumu sana kwa sababu wote wanategemea serikali ili kuishi na kukua. Kwenye nchi hizi huwezi kuwa tajiri kama serikali haijaridhia na wakati wowote hata ukiwa tajiri serikali inaweza kukufanya kuwa masikini. Wananchi wanaaminishwa serikali ni kama Mungu na haikosei. Watu wanaaminishwa kuwa kiongozi mkuu wa serikali hawezi kukosea. Vyombo vyote na taasisi za nchi lazima ziwe na utii kwa serikali na kiongozi wa serikali. Kwenye hizi nchi viongozi wa kisiasa ndo wanakuwa matajiri kuliko watu wa kawaida kwa sababu wao ndo wanakuwa na access ya vitu vizuri
Katikati ya hizi nchi kuna nchi kama China. Wao kisiasa wanaamini kwenye dhana ya Ukomunist ambayo haitofautoani sana na upande wa pili niliouelezea hapo juu ila kiuchumi wana mfumo wa kibepari/ ubeberu. China anafanya hivi kwa sababu alipeleka watu wake wengi Urusi na Marekani/ Ulaya ambao walisoma hizi dhana zote mbili na wakarudi kwao kutengeneza dhana yao.
Washirika wa Mabeberu
Hapa duniani Mabeberu/ Mabepari wana washirika wao pia. Washirika wa mabeberu ni nchi kama Korea kusini, Malyasia, Kuwait, Dubai, Saudi Arabia, Israel, Morocco, South Africa, Botswana, Ivory Coast, Ghana, Algeria, Singapore, Japan na wengineo wengi. Nchi hizi zote hizi kiujumla zimepiga hatua kubwa sana kimaendeleo hasa maendeleo ya watu na vitu. Kuna miundombinu ya uhakika, uwekezaji wa uhakika, fursa nyingi za ajira na kiwango kizuri cha elimu na teknolojia.
Washirika wa Wajamaa
Hapa kuna nchi kama Tanzania, Cuba, Venezuela, Korea ya kusini, Burundi, Congo, Sudan ya Al bashir, Sudan Kusini, Korea kaskazini na wengineo. Nchi hizi zote zina umasikini wa kutupwa na kuminywa kukubwa kwa haki za binadamu. Kuna umungu kwa viongozi wa mataifa na kiwango kikubwa cha kuzuia kukua kwa wananchi hasa wenye mawazo huru na mipango huru. Matajiri kwenye hizi nchi ni wale wanaojitoa kula na viongozi wa serikali na mara nyingi hawako stable kwa sababu wote wanategemea serikali na Viongozi wake. Vyombo vya maamuzi havo a Uhuru.
Hapa Tanzania Vyama viwili vikuu CCM na Chadema vimegawanyika kwenye mgawanyo huu. CCM wanaamini kwenye dhana ya ujamaa na Chadema wanaamini kwenye dhana ya Ubepari
Ewe mtanzania embu pata hii Elimu na ujue wanaosema huyu ni Bepari/ Beberu wanamaanisha nini na anayesema huyu mjamaa anamaanisha nini.
Mwisho niseme hakuna shida yeyote mtu kufuata dhana ya ubepari/ ubeberu ila kuna walakini mkubwa mtu anapofuata dhana ya ujamaa
Usisahau Kushare!!
Sambaza Upendo.
No hate No Fear!
Lord Denning
Leo napenda nitoe Elimu kwa watanzania juu ya propaganda za wana CCM kuwa yeyote anayempinga Raisi Magufuli ni kibaraka wa Mabeberu. Wanasema haya wakitaka kujenga picha kwa watanzania ( wadanganyika) kuwa ubeberu ni kama dhambi au jambo fulani ambalo halifai. Najua kwa watanzania wenzangu wengi wetu Elimu kwetu imekuwa shida na kwa sababu hiyo wanasiasa wamekuwa wakitumia kutokujua kwetu katulisha mambo ambayo wao wanataka tuyaamini. Wanafanya haya kwa maslahi yao ya kisiasa
Asili ya Ubeberu ni nini hasa?
Kwanza kwa watanzania wasiofahamu, Dunia ya leo inaongozwa na pande mbili zinazopigana kila kukicha kutawala Dunia.
Pande ya kwanza inaongozwa na Marekani na washirika wake hasa nchi za Ulaya Magharibi na Scandnavia yaaani Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Uholanzi, Canada, Sweden , Norway, Hispania, Ureno, Ubelgiji na washirika wao wengine. Hizi nchi zote zinaamini katika dhana ya maendeleo ya ubepari Yaani uhuru katika kuamua, kuwekeza na kumiliki.
Dhana hii hairuhusu serikali kukamata njia kuu za uchumi na inawapa nafasi watu binafsi kukamata njia kuu za uchumi. Dhana hii ina hatua yake ya juu ambayo wengi wanaiita kuwa Ubeberu. Kutokana na dhana ya ubepari/ ubeberu kuamini kwenye Uhuru wa watu katika maendeleo na kumiliki vitu nchi nyingi zenuw hii dhana raia wao wana maisha mazuri sana na wanaishi maisha ya kistaarabu sana na kuheshimiana.
Katika nchi hizi mtu unaweza kuwa tajiri wakati wowote kwa sababu kuna mifumo imara ya kuruhusu watu kukua kiuchumi na kimaisha ili mradi ufanye tu kazi na uwe na kipaji halali . Taasisi za hizi nchi ni imara na ndo zinawasimamia viongozi wa serikali. Viongozi hawana uimara kuzizidi taasisi zao. Na wakati wowote viongozi wanaweza kuwajibishwa.
Pande ya pili inaongozwa na Urusi na washirika wake ambao ni Venezuela, Cuba, Korea ya Kusini na nchi chache za ulaya ya mashariki. Hawa wanaamini kwenye ujamaa yani Sera ya serikali kumiliki njia zote kuu za uchumi. Nchi hizi haziamini kwenye Uhuru wa watu wao kwenye biashara, siasa, dini au maisha na hata ukiziangalia nyingi zimepiga Marufuku dini mbalimbali Tanzania Chama cha Mapinduzi nacho kinaamini kwenye Sera za ujamaa ingawa wao wanaamini kwenye uhuru wa dini Ila zile zinazokuwa chini ya uangalizi/ mkono wa serikali Mf. Bakwata.
Katika hizi nchi , nyingi raia wake wana maisha magumu sana kwa sababu wote wanategemea serikali ili kuishi na kukua. Kwenye nchi hizi huwezi kuwa tajiri kama serikali haijaridhia na wakati wowote hata ukiwa tajiri serikali inaweza kukufanya kuwa masikini. Wananchi wanaaminishwa serikali ni kama Mungu na haikosei. Watu wanaaminishwa kuwa kiongozi mkuu wa serikali hawezi kukosea. Vyombo vyote na taasisi za nchi lazima ziwe na utii kwa serikali na kiongozi wa serikali. Kwenye hizi nchi viongozi wa kisiasa ndo wanakuwa matajiri kuliko watu wa kawaida kwa sababu wao ndo wanakuwa na access ya vitu vizuri
Katikati ya hizi nchi kuna nchi kama China. Wao kisiasa wanaamini kwenye dhana ya Ukomunist ambayo haitofautoani sana na upande wa pili niliouelezea hapo juu ila kiuchumi wana mfumo wa kibepari/ ubeberu. China anafanya hivi kwa sababu alipeleka watu wake wengi Urusi na Marekani/ Ulaya ambao walisoma hizi dhana zote mbili na wakarudi kwao kutengeneza dhana yao.
Washirika wa Mabeberu
Hapa duniani Mabeberu/ Mabepari wana washirika wao pia. Washirika wa mabeberu ni nchi kama Korea kusini, Malyasia, Kuwait, Dubai, Saudi Arabia, Israel, Morocco, South Africa, Botswana, Ivory Coast, Ghana, Algeria, Singapore, Japan na wengineo wengi. Nchi hizi zote hizi kiujumla zimepiga hatua kubwa sana kimaendeleo hasa maendeleo ya watu na vitu. Kuna miundombinu ya uhakika, uwekezaji wa uhakika, fursa nyingi za ajira na kiwango kizuri cha elimu na teknolojia.
Washirika wa Wajamaa
Hapa kuna nchi kama Tanzania, Cuba, Venezuela, Korea ya kusini, Burundi, Congo, Sudan ya Al bashir, Sudan Kusini, Korea kaskazini na wengineo. Nchi hizi zote zina umasikini wa kutupwa na kuminywa kukubwa kwa haki za binadamu. Kuna umungu kwa viongozi wa mataifa na kiwango kikubwa cha kuzuia kukua kwa wananchi hasa wenye mawazo huru na mipango huru. Matajiri kwenye hizi nchi ni wale wanaojitoa kula na viongozi wa serikali na mara nyingi hawako stable kwa sababu wote wanategemea serikali na Viongozi wake. Vyombo vya maamuzi havo a Uhuru.
Hapa Tanzania Vyama viwili vikuu CCM na Chadema vimegawanyika kwenye mgawanyo huu. CCM wanaamini kwenye dhana ya ujamaa na Chadema wanaamini kwenye dhana ya Ubepari
Ewe mtanzania embu pata hii Elimu na ujue wanaosema huyu ni Bepari/ Beberu wanamaanisha nini na anayesema huyu mjamaa anamaanisha nini.
Mwisho niseme hakuna shida yeyote mtu kufuata dhana ya ubepari/ ubeberu ila kuna walakini mkubwa mtu anapofuata dhana ya ujamaa
Usisahau Kushare!!
Sambaza Upendo.
No hate No Fear!
Lord Denning