Dhana ya "kumbemenda mtoto"

Dhana ya "kumbemenda mtoto"

kuna jamaa aliniambia kuwa kuna njia uzazi wa mpango inaitwa breastfeeding method ambayo mama anaweza kushiriki mapenzi ndani ya miezi 6 baada ya kujifungua na mumewe lakini sharti ni lazima mama awe anamnyonyesha vizuri mwanae angalau kwa siku si chini ya mara kumi na tano hiyo inapelekea homoni zinazosupport kunasa mimba ziwe bize katka utengenezaji wa maziw na kufanya mama asipate mimba katika kipindi icho
 
kuna jamaa aliniambia kuwa kuna njia uzazi wa mpango inaitwa breastfeeding method ambayo mama anaweza kushiriki mapenzi ndani ya miezi 6 baada ya kujifungua na mumewe lakini sharti ni lazima mama awe anamnyonyesha vizuri mwanae angalau kwa siku si chini ya mara kumi na tano hiyo inapelekea homoni zinazosupport kunasa mimba ziwe bize katka utengenezaji wa maziw na kufanya mama asipate mimba katika kipindi icho

Hii ntaifanyia utafiti pia
 
ukijua mume sio muaminifu,akirudi asimguse mtt kabla hajaoga
pia baada ya kukutana nae hakikisha unajiswafi thn endelea
na mtt,ila kwa mwanaume muelewa akijua katoka kwny uchafu wake
hatothubutu kumgusa mtt!!

Naungana na wewe inspector laddy, mwafrika akikaririshwa vitabu vya wazungu anadharau elimu ya mababu zake anaiita "imani potufu"

Brain wash nalo ni tatizo katika jamii yetu. Siyo kila elimu iliyokuwa inatolewa na wazee wetu ni "imani potofu" japo walikuwa hawaandiki kwenye vitabu lakini walifanya tafiti na kuona ni kweli. Kuna vitu vingine havielezeki kisayansi lakini vipo! Mfano Mungu, malaika, shetani, jini, mizimu nk! Huwezi kuingia maabara ukathibitisha na kuonyesha ulimwengu kuwa kuna roho hizo! Kuna kitu watu wanaita "machale", huwezi kuprove kisayansi mtu kuchezwa machale akaepuka hatari fulani!

Turudi kwenye mada, ukubwa dawa, sisi tunao ishi kwenye jamii huru, hali ya mtoto kubemedwa tunaifahamu na inatokea-hutaki acha! Kama mama ana mtoto mchanga aka anza kutembea na mwanamume asiye baba wa mtoto, kwa vyovyote vile lazima afya ya mtoto itateteleka labda aache kumnyonyesha kabisa huyo mtoto. Vinginevyo mtoto atadhoofika na hata kufa! Hii si imani potofu bali ni kitu kipo na huwezi kuprove kisayansi.
 
tunawaona sana wtt waliobemendwa mitaani
mtt anakua wa ajabu,ila hua namchukia sana
mwanamke anaefanya hvyo kwa mtt wake,una yako
muachishe mtt kunyonya na si kumharibu!!
 
Sawa, kwhy mama anaenyonyesha anaweza akaendelea kukutana na mumewe bila kipingamiz chochote! na mtoto asiathirike?

baba na mama hawabemendi mtoto isipokuwa wajihadhari wasitunge mimba kwa kuwa mzunguko wa mwili wa mama unakuwa haujakaa vizuri.mtoto hyathiriwa na wazazi kuwa na mahusiano ya nje.
 
someni mtakavyosoma digrii na vyeti ila mfahamu kuna vitu vya asili vipo na ni halisi.kubemenda kupo ,wazazi hawatakiwi kuwa na mahusiano ya nje pindi wanapokuwa na mtoto mchanga.
 
Wandugu, kwanza hili jambo lipo!? Yan lina ukwel? Na inakua vipi mpaka mtoto anabemendwa??? Kwa wanaoujua tafadhali

====================
====================

kubemenda-mtoto.jpg


KUBEMENDA MTOTO



Kumbemenda mtoto ni mtoto kutokua vizuri ikidhaniwa kutokea kutokana na mama anayenyonyesha mtoto kukutana kimapenzi na mwenzi wake hasa kipindi mtoto bado ni mchanga na ananyonyeshwa.

Hii ni dhana iliyopo katika jamii mbalimbali, na inadhaniwa hutokea kwa sababu mtoto kunyonya maziwa yenye mbegu za kiume zilizoingia kwenye maziwa baada ya kufanya mapenzi.

Je, kuna ukweli wowote?


Hapana. Kiukweli na kiutaalamu dhana hii si sahihi kabisa!
Kufanya mapenzi na mwenzi wako baada ya kujifungua hakuwezi kusababisha afya ya mtoto kuzorota. Mwanamke anapokutana na mwanaume kimapenzi, shahawa huingia kwenye tumbo la uzazi na kubaki huko. Haziingii kwenye damu wala haziwezi kufika kwenye maziwa. Dhana ya kuwa shahawa huingia kwenye maziwa na kumuathiri mtoto sio sahihi.

Ni baada ya muda gani mwanamke aliyejifungua anaweza kufanya mapenzi?


Unaweza kuanza kufanya mapenzi tena baada ya maji maji yenye damu ya uke (lochia) kuacha kutoka ambayo ni kama wiki 3 mpaka 4 baada ya kujifungua, na wewe kujisikia vizuri na kuwa tayari kushiriki katika mapenzi. Pia, mnaweza kusubiri mpaka wiki 6 zipite toka ulivyojifungua.


Je, kuna athari yoyote ya kufanya mapenzi baada ya kujifungua?


Kufanya mapenzi baada ya kujifungua hakuwezi kuleta madhara kwa mtoto endapo hamna maambukizi ya magonjwa kama Virusi Vya UKIMWI (VVU). Ikiwa mwanaume ana VVU anaweza kumuambukiza mama na kisha mtoto kuambukizwa kupitia maziwa ya mama.
Ikiwa mnafanya mapenzi kabla ya damu damu ya ukeni kukata, maambukizi ya bakteria yanaweza kutokea kwenye tumbo la uzazi (endometritis). Pia kuna uwezekano wa mama kupata ujauzito miezi 6 ya kwanza ya kunyonyesha.


Nini kinasababisha afya ya mtoto kuzorota?


Kama tulivyoona, kufanya mapenzi hakusababishi mtoto kubemendwa. Afya ya mtoto inaweza kuzorota kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo;



  • Kukosa maziwa ya mama ya kutosha
  • Mtoto kushindwa kunyonya vizuri
  • Kuanzishiwa vyakula vya ziada mapema, kabla mtoto hajafikisha miezi 6 au vyakula visivyo na viritubisho vya kutosha.
  • Homa, nimonia na maambukizi ya mfumo wa mkojo (UTI) za mara kwa mara.
  • Maambukizi ya magonjwa kama Virusi vya UKIMWI (VVU) au Kifua Kikuu.
  • Matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo (congenital heart diseases).

Kufanya mapenzi na mwenzi wako hakusababishi mtoto kubemendwa. Baada ya kujifungua mtoto hutegemea kupata lishe bora kutoka kwenye maziwa ya mama, hivyo nyonyesha mtoto wako vizuri. Ukiona ukuaji wake unazorota, onana na daktari.


Chanzo.
www.afyamd.co.tz

 
wandugu.....kwanza hili jambo lipo!???yan lina ukwel??? na inakua vipi mpaka mtoto anabemendwa??? kwa wanaoujua tafadhali
kubemenda-mtoto.jpg


KUBEMENDA MTOTO



Kumbemenda mtoto ni mtoto kutokua vizuri ikidhaniwa kutokea kutokana na mama anayenyonyesha mtoto kukutana kimapenzi na mwenzi wake hasa kipindi mtoto bado ni mchanga na ananyonyeshwa.

Hii ni dhana iliyopo katika jamii mbalimbali, na inadhaniwa hutokea kwa sababu mtoto kunyonya maziwa yenye mbegu za kiume zilizoingia kwenye maziwa baada ya kufanya mapenzi.

Je, kuna ukweli wowote?


Hapana. Kiukweli na kiutaalamu dhana hii si sahihi kabisa!
Kufanya mapenzi na mwenzi wako baada ya kujifungua hakuwezi kusababisha afya ya mtoto kuzorota. Mwanamke anapokutana na mwanaume kimapenzi, shahawa huingia kwenye tumbo la uzazi na kubaki huko. Haziingii kwenye damu wala haziwezi kufika kwenye maziwa. Dhana ya kuwa shahawa huingia kwenye maziwa na kumuathiri mtoto sio sahihi.

Ni baada ya muda gani mwanamke aliyejifungua anaweza kufanya mapenzi?


Unaweza kuanza kufanya mapenzi tena baada ya maji maji yenye damu ya uke (lochia) kuacha kutoka ambayo ni kama wiki 3 mpaka 4 baada ya kujifungua, na wewe kujisikia vizuri na kuwa tayari kushiriki katika mapenzi. Pia, mnaweza kusubiri mpaka wiki 6 zipite toka ulivyojifungua.


Je, kuna athari yoyote ya kufanya mapenzi baada ya kujifungua?


Kufanya mapenzi baada ya kujifungua hakuwezi kuleta madhara kwa mtoto endapo hamna maambukizi ya magonjwa kama Virusi Vya UKIMWI (VVU). Ikiwa mwanaume ana VVU anaweza kumuambukiza mama na kisha mtoto kuambukizwa kupitia maziwa ya mama.
Ikiwa mnafanya mapenzi kabla ya damu damu ya ukeni kukata, maambukizi ya bakteria yanaweza kutokea kwenye tumbo la uzazi (endometritis). Pia kuna uwezekano wa mama kupata ujauzito miezi 6 ya kwanza ya kunyonyesha.


Nini kinasababisha afya ya mtoto kuzorota?


Kama tulivyoona, kufanya mapenzi hakusababishi mtoto kubemendwa. Afya ya mtoto inaweza kuzorota kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo;



  • Kukosa maziwa ya mama ya kutosha
  • Mtoto kushindwa kunyonya vizuri
  • Kuanzishiwa vyakula vya ziada mapema, kabla mtoto hajafikisha miezi 6 au vyakula visivyo na viritubisho vya kutosha.
  • Homa, nimonia na maambukizi ya mfumo wa mkojo (UTI) za mara kwa mara.
  • Maambukizi ya magonjwa kama Virusi vya UKIMWI (VVU) au Kifua Kikuu.
  • Matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo (congenital heart diseases).

Kufanya mapenzi na mwenzi wako hakusababishi mtoto kubemendwa. Baada ya kujifungua mtoto hutegemea kupata lishe bora kutoka kwenye maziwa ya mama, hivyo nyonyesha mtoto wako vizuri. Ukiona ukuaji wake unazorota, onana na daktari. chanzo.
www.afyamd.co.tz
 
wandugu.....kwanza hili jambo lipo!???yan lina ukwel??? na inakua vipi mpaka mtoto anabemendwa??? kwa wanaoujua tafadhali
Hii hutokea ikiwa mama wa mtoto atashiriki tendo na mwanaume ambaye si baba wa mtoto huku mtoto akiwa bado ananyonya
 
Hii hutokea ikiwa mama wa mtoto atashiriki tendo na mwanaume ambaye si baba wa mtoto huku mtoto akiwa bado ananyonya

Sina hakika na usemacho, wanawake wengi wanaosingizia mimba kwa wanaume wengine au wanaochepuka hadi wanabeba mimba za nje watoto wao wangekuwa wamebemendeka, hili ni suala la mtoto kukosa matunzo ikiwemo lishe nzuri tu, na siamini vinginevyo.
 
Hii ishu ipo jamani tusidanganyane,labda mniambie kuwa haijathibishwa kidaktari lakini ipo.
Mwanamke yeyote akitoka kukutana na mtu kimapenzi halafu akaja kumshika mtoto mdogo kabla hajaoga mtoto anadhoofu ukuaji wake unaanza kusuasua hii ndio inaitwa kubemenda co lazma awe mama yake,lakini kama ulipomaliza mambo yako ulioga vizuri wala hakuna tatizo.Swala la kwashiakor na marasmus ni ishu tofauti kabisa na hii.Ndio maana mwanamke mwingne anaweza kukukataza usimshike mwanae kama hana uhakika na utokako.Mwanaume anaweza kumshika mtoto akiwa ktk hali hyo ila effect yake haitakuwa kubwa kama ya mwanamke.
 
Sina hakika na usemacho, wanawake wengi wanaosingizia mimba kwa wanaume wengine au wanaochepuka hadi wanabeba mimba za nje watoto wao wangekuwa wamebemendeka, hili ni suala la mtoto kukosa matunzo ikiwemo lishe nzuri tu, na siamini vinginevyo.

Itabidi uamini pindi itakapotokea kwako,ukiwa na mtoto baada ya kufanya mambo yenu usiku mkalala bila kuoga usiku huo hadi asubui na mtoto akanyonya usiku ndio utajua ishu ni lishe au kubemenda..watu waliogundua hili wanaakili sema tu wameshindwa kuliweka kisomi
 
Unapobeba mimba ya mtto mwngne ili hal mtoto wa kwanza bado hajaacha kunyonya.. Hali hiyo humdhoofisha yule aliekatishwa, kitendo kile cha kudhoofika ndio huitwa kubemendwa.
 
hiyo kitu hata haipogo biti tu la wazee ili watu wavitulize
 
Sayansi inakataa kuwepo kwa kesi hii..
Hakuna uhusiano wowote kati ua ukuaji wa mtoto na wazazi wake kushiriki tendo la ndoa....
Mtoto huitaji..
Kunyonya vizuri..
Kulala vizuri na matunzo mengine mazuri kwa wakati huo..
Dhana hii ilikuwepo zamani za mababu...ili kiwazuia wazazi wa mtoto wasifanye mapenzi kwa kipindi fulani na badala yake waelekeze nguvu, akili na muda wao kwa mtoto wao mpya..
Mambo mengi ya zamani hayakua na maana kama yanavyosikika bali uanavyokusudiwa.
 
Itabidi uamini pindi itakapotokea kwako,ukiwa na mtoto baada ya kufanya mambo yenu usiku mkalala bila kuoga usiku huo hadi asubui na mtoto akanyonya usiku ndio utajua ishu ni lishe au kubemenda..watu waliogundua hili wanaakili sema tu wameshindwa kuliweka kisomi

Aisee sijui unasema nini, mim ni mzazi na sijawahi kuona afya ya mwanangu ikiteteleka hata siku moja, nichokiongea nakijua vizuri.
 
Unapobeba mimba ya mtto mwngne ili hal mtoto wa kwanza bado hajaacha kunyonya.. Hali hiyo humdhoofisha yule aliekatishwa, kitendo kile cha kudhoofika ndio huitwa kubemendwa.

we unafikiri mtoto huyo anadhoofika kwa nini? sababu amekosa maziwa ya mama yenye virutubisho vyote..... sababu mama uacha kunyonyesha pindi anaposhika mimba nyingine, kumbe tunaweza kumfanya mtoto hasidhoofike kwa kumpa formula i mean formula... angalia nchi zilizoendelea mama baada ya miezi 3 ya kujifungua anabeba mimba nyingine lakini hakuna msamiati huo wa kubemenda, sisi tukifanya hivyo huo msamiati unaingia sababu tunawapa maziwa ya nido na cowbell watoto chini ya miaka miwili kwa nini ilo lisitokee
 
Hii habari imekuwa ikigonga sana vichwa vya wazazi wengi sana. Ila mwisho wa siku ukweli unakuwa haueleweki,mana kila mtu anasema lake..
 
Back
Top Bottom