Dhana na Miongozo ya "Katika Utawala Wangu..."

Samahani,najua mnaongelea mambo serious ila mimi nimekumbuka wale maclass monitors wanaoanzaga na mbwembwe za kuwachoma notorious noisemakers,dodgers na wanafunzi wabishiwabishi haha

Walimu wanawapendaga sana.Yani hawa unakuta wanalist kumi kwenye begi za noisemakers incase mwalimu akiuliziana wanaongezaga masifa hawaridhiki hawa, wanaanza vibylaws vyao mara oh hamna kwenda break mtakuwa mnasoma..lohutaskia'FROM NAU ONI NOWANI IS GO TO TOLEITI ASKIN ME FASTI'Hehee basi sie backbenchers eti tunacheka unashangaa 'YOU ENDI YOU NILIDAUNI!' Heeeeeee kimyaaaaa.
Hawa hawakosagi cha kuwapa sifa.Ni kama ulevi yani.Halafu kama alikuwa ndio besty unashangaa na ww unaanza kula adhabu ndio wengine wanaanza kuelewa kumbe its real.dah.Basi ikafika extent wale walimu madodger wakaanza kuchomwa kwa headmaster.Na frontbenchers waliojiona wasafi wakaanza kula doso kama sisi.haha.basi backbenchers ewaaaa tukajifariji we are not alone
Naweza nkasema monitor wetu alikomaa bhana.Japokuwa tulikaziwa pepa na walimu dodgers kumkomoa monitor wetu,bado hakuterereka

Tukashangaa kidogokidogo wale manotorious waclass wakabadilisha strategy,wakaanza kujipendekeza.Since monitor aliachwa na marafiki wengi basi akakubali urafiki.haha.kushnei.leo hatamwandika flani ni noisemaker hata kama yeye peke yake ndo alikuwa anarukaruka na kuimba darasani.Mtapotezea.Kesho yake haandikwi.mhh.keshokutwa lile lijamaa linoisemaker eti nayeye anapewa kazi ya kuandika noisemakers.
Hapa noo.haiwezekani.Asa ndo pale darasa zima linaungana kujadili kunanini? Yani hakitaeleweka..backbenchers na frontbenchers wote wamechoka mnyoosho chezea kubaki class breaktime.

Kwaiyo tunapata courage ya kumfata monitor wetu mtukufu asiyependelea aliyemchoma hadi besty yake damudamu aliyemsapoti mpaka kapata umonitor,tunajua hili ni jambo dogo sana kwake.ohoo kumbe monitor wetu alikuwa hapangiwagi haha.Dah.Kuna haka kasichana cha lasiitaA kalikuwa kanamsuta monitor wetu bas na sisi tukawa tunamsapoti tunampa habari za wongo na kweli alimradi tu amuumize monitor wetu..siunajua tena huku ukifungua domo unachezea adhabu.Kalikuwa kanasuta for free sema baadae ikaabidi tumpe boost za mihogo icecream nini siunajua tena

Ila kipindi cha uchaguzi kilikaribia bhana si akatulegezea zile bylaws zake zakijinga.Imagine tukaanza tena kwenda break af saiv ukimjibisha au kumcheka english yake unapiga magoti tu hamna kuita mvua kwahiyo tukafurahi kichizi..unafikiri,tukamchagua tena mbona.hahaa.usishangae ila ndo hivyo.

Sema juzi kwenye yale magroup ya primary jamaa akanifata inbox eti anasoma diploma chuo flani ila anagari haha halafu akatuma picha nyingiii akanikumbusha jinsi alivyotusaidia kusoma kwa bidii badala ya kwenda break ndo nikamkumbuka haha nlicheka sana baadae akanitongoza wakati zamani unapigwa makwenzi na unaambiwa ulale kwenye dawati lako na huyohuyo mwanaume haha Ila kwakweli kuna watu hawawezi kupumua bila credits za watu.Naona credits za classmates wake anaona ndio za maana saiv.

Aisee minlikuwa nmekumbuka tu enzi za utawala wa monitor wangu.haha mnaweza kuendelea kuchangia points za maana, nlikuwa napita

NB.Fiction based on true stories.
 
The Obama administration.
Bush Administration
Clinton Administration.
Sema jingine
Sawa hao wote uliowataja walikuja na vipaumbele vyao. Lakini hakuna hata mmoja kati ya hao aliyevunja misingi ya taifa la Marekani , akaanza kuongoza nchi kwa utashi wake , huku akipuuza utawala wa sheria.

Nchi siyo familia eti uitawale unavyotaka wewe. Juzi Trump alitaka kuleta upuuzi pale Marekani lakini Mahakama ulimzuia.

Viongozi lazima waheshimu utawala wa sheria.
 
Hujamsikia akisema Tanzania ya Magufuli?Kwa miaka hii mitano Tanzania tumeishaumia tukubali maumivu tu.Tukimaliza miaka ya jamaa yako tutaanza kutibu vidonda vya chuki,visasi na ubaguzi.Jiandae tu.Hayo mengine ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu
Shem Tetty no. Hiyo Tanzania ya Magufuli ni neno tuu, the actual fact ni Tanzania ni ya Watanzania. Usiwe na wasiwasi kuhusu hizi kauli za vitisho na maneno makali, ni mikwala tuu, but in reality sisi Wasukuma ni watu tuko peace sana, ndio tunaoongoza kwa upendo, huruma na kwa kupenda idadi kubwa.

Kule kuongea kama kwa ukali kusikutatize ni nature yake tuu, ndani ya ukali ule kuna upole wa ajabu, ndani ya chuki ile kuna upendo wa ajabu, na ndani ya papara hizi kuna subra ya ajabu.
Kanda ya Ziwa na kuongea kwa ukali: Ukali wa Rais Magufuli ni asili tuu ya wasukuma, sio udikteta!
Paskali
 
Nyerere mwaka 1967 alisema asiwepo mtu yeyote kusema kitu flani ni mali yake mfano eebwana unaona lile gari lile ni mali yangu ..Je na dereva je? na dereva pia ni dereva wangu.
Nyerere alikua akimaanisha jambo kubwa ambalo leo ndio lipo kwa viongozi wetu wa leo kuanzia mkuu wa wilaya/mkoa hadi raisi kutaka wao ndio wamiliki mpira na kujipatia umaarufu kisiasa
 
Guys... Who is legal advisor wa Rais Magufuli? Au advisor wa namna yeyote ile?

Hii ziara ya Pwani yametokea matamko ya Rais ya kusema "katika utawala wangu" but kwangu naona hakuna jitihada kuweka mfumo, kanuni Na Sheria Imara zinazoeleweka ili uwajibikaji uwe ni kitu Na tunu ya kawaida si mfumo w utegemezi wa kiongozi mkuu wa nchi au hamasa yake kuongoza Na "kunyoosha" Taifa!

JPM alipokujaa alishangaa kukuta madudu na machafu kupindukia, sababu yawezekana sana kuwa JK naye alisema "katika utawala wangu" akajifanyia mambo Na maamuzi mengi ambayo Magufuli anayashangaa. Labda naye Kikwete alikuta aliyoyarithi ambayo yalifanywa kwa mantiki ya "katika utawala wangu.." iwe ni Serikalini au hata katika Chama.

Leo Magufuli anaongoza nchi Na kufanya kila kitu kwa kigezo cha "katika utawala wangu" Keaho akiondoka Magufuli, atakayekuja naye atasema "katika utawala wangu" na kubadilisha Yale yaliyofanya "katika utawala wangu" wa Magufuli !

Now nikiangalia kwa nini kuna non-responsive kutoka taasisi, mashirika, Serikali, watendaji Na hata wananchi, jibu lake ni kila mtu anajua "katika utawala wangu" utapita Na kuna expiry date Na si mfumo unaoeleweka kisheria... Wanapuuzia wanajua wakisema "ametukuta, ataondoka, atatuacha"!

Nchi imekuwa ikiendeshwa au kuongozwa na maamuzi kufanywa kwa dhana na fikra za "katika utawala wangu.." kuanzia Rais mpaka Mkuu wa Wilaya au hata mwenyekiti wa kijiji kupuuzia kabisa mipaka ya kisheria, mamlaka,kanuni hata katiba.

Zaidi, dhana hii ya "Katika utawala wangu.." si kwamba imekwamisha maendeleo ya jamii na Taifa, lakini hata imepunguza uwajibikaji wa kweli, kujenga kiburi nauungwana wa kukiri makosa, kujikosoa au kujisahihisha kunakosekana.

Mfano inawezekana DC wa Hai juzi akivunjavunja shamba la Mbowe alitumia kigezo hicho cha "katika utawala wangu.." au leo Mkuu wa TRA Arusha anaposema ukikutwa huna risiti fainielfu thelathini, naye anatumia nguvu ya "katika utawala wangu".

Keshoanapokuja mtendaji au kiongozi mwingine naye akasema "katika utawala wangu" (mfano mzuri ni Nape na Mwakyembe wizara ya habari) naye akaamua kusema anabadilisha na kufuta kila kilichofanywa na aliyemtangulia kwa kuwa "katika utawala wangu" haoni manufaa.

Kuna tofauti ya kufanya mambo "katika utawala wangu" kama mambo hayo hayahusu kanuni, sheria, taratibu, katiba au maamuzi yenye impact kubwa kwa jamii na Serikali.

Ni haki kusema "katika utawala wangu" uvivu,uzembe, ubabaishaji, uchelewaji, umangimeza, uhujumu nu mwiko na kamwe hautavumiliwa. Lakini kuna haja ya kuweka na kurejea misingi iliyopo na kuhoji kwa nini utovu wa nidhamu upo na au unaongezeka!

Leo Rais Magufuli kawasema Brela mpaka kutoa tamko (presidential executive order) verbally kuwa wenye nia ya kuanzisha viwanda au biashara wasisubiri Brela, waanze mchakato maana Brela wanajivutavuta na kupunguza kasi ya maendeleo na azma ya viwanda ya awamu ya tano. Najiuliza je kwa nini Brela leo ni miezi 20 tangu awamu ya Tano iingie madarakani bado inajivutavuta na kuwa na umangimeza au ukiritimba ambao unakwamisha ufanisi? je hawana kanuni za uwajibikaji? au usimamizi wa kanuni za uwajibikaji na majukumu zina mapengo na mianya ya uzembe, uhujumu au hata kulea rushwa na kero?

Je yawezekana huko Brela hakuna hizi kanuni kwa kuwa kila mkubwa wa sehemu anafanya mambo ya "katika utawala wangu" na kujiamulia mambo na wafanyakazi wa chini kwa kukosa mfumo unaoeleweka na kushuhudia kwao wakubwa wakifanya mambo kwa itikadi ya "katika utawala wangu" basi wanajijengea kiburi cha "alitukuta, atapita, atatuacha hapahapa"?

May be tukiongelea mambo kwa mtazamo huu, ubishi na ushabiki unaopinga kujengwa kwa mfumo huru Imara kuanzia Katiba, Sheria na Kanuni hata uwajibikaji wake utaangalia mambo kiuhalisia Na si kushangilia current happenings ambazo "baada ya utawala wangu" tutarudi kule kule au atakuja mwingine na mtazamo wake na kusema "katika utawala wangu"?


Independence ianzie kwenye vyombo vya mfumo, polisi, jeshi, mahakama nk. Rais asiwe ndio mteule wa vyombo hivi maana ndivyo vinasimamia utekelezaji wa sheria, bali viwe china ya taasisi ambayo haina mahusiano kabisa na utawala pamoja na kuwa vitawajibika kwa utawala.

IGP, Jaji Mkuu wanapo teuliwa na Rais, ni vigumu sana kutomsikiliza mteule wao na ndio tunayo yashuhudia kila leo kwamba wakosaji ni wapinzani tu na CCM pamoja na wingi wa wabunge wao na watendaji wengine wao ni malaika, huku kila leo skendo zikiongezeka, ESCROW, EPA, MAKINIKIA you name them.
 
Ningekuwa rais Magufuli,ningejipunguzia mlundikano wa kazi nyingi kwa kuzitawanya kupitia uandishi wa katiba bora!
Napenda kuwa rais mkali ila mla bata,kwa kuwaachia wale wa mihimili mingine wafanye kazi zao!
Yanini kufanya kila kitu,mpaka kujichosha!
Uoga wa nini,wakati kwa ujinga wa watz wengi,hakuna kama kuna mtu wa kunipindua!?
Katiba ndiyo mwarobaini!
Huu utawala wa kujifanya "kiraka" wa kucover namba zote unakera,kuboa na unakufanya mwoga mpaka unapelekea kuwabana wapinzani ili wasikukosoa maana hujiamini!
 
Guys... Who is legal advisor wa Rais Magufuli? Au advisor wa namna yeyote ile?

Hii ziara ya Pwani yametokea matamko ya Rais ya kusema "katika utawala wangu" but kwangu naona hakuna jitihada kuweka mfumo, kanuni Na Sheria Imara zinazoeleweka ili uwajibikaji uwe ni kitu Na tunu ya kawaida si mfumo w utegemezi wa kiongozi mkuu wa nchi au hamasa yake kuongoza Na "kunyoosha" Taifa!

JPM alipokujaa alishangaa kukuta madudu na machafu kupindukia, sababu yawezekana sana kuwa JK naye alisema "katika utawala wangu" akajifanyia mambo Na maamuzi mengi ambayo Magufuli anayashangaa.
...
May be tukiongelea mambo kwa mtazamo huu, ubishi na ushabiki unaopinga kujengwa kwa mfumo huru Imara kuanzia Katiba, Sheria na Kanuni hata uwajibikaji wake utaangalia mambo kiuhalisia Na si kushangilia current happenings ambazo "baada ya utawala wangu" tutarudi kule kule au atakuja mwingine na mtazamo wake na kusema "katika utawala wangu"?
Mkuu unataka kusikia habari ya mifumo Tanzania? Utasubiri hadi mwisho wa dunia. Nchi hii watu wengi ama hawajui au hawana utashi wa kufahamu nini maana halisi ya itikadi, sera, mfumo, katiba, sheria, kanuni. Hawana uwezo wa kuelewa vigezo hivyo "vya mzungu" vinasaidia nini katika jamii. Wao wanataka kuongozwa na aina ya "mtu maalum" wa kumfuata, kumshabikia na hata kumuabudu, period!

Mtu ambaye neno lake ndio sheria, ndio agizo la kiserikali, na ndio uamuzi wa mwisho kwenye kila nyanja ya maisha ya taifa. Akiamka leo akapiga marufuku kusinzia mchana basi Polisi wanaingia kazini kusaka wakosaji hata wanaokonyeza - hakuna kuhoji. Akiamua kufuta sikukuu ya kitaifa basi ndivyo itakavyokuwa. Akitangaza mapumziko, hewala. Akimpa kibali mwekezaji kwa agizo la mdomo tu wanashangilia hadi kutambaa. Akimnyang'anya na kumtangaza mwizi wanaandamana kuunga mkono na kumvamia huyo "mwekezaji mwizi". That's TZ for you!
 
Ktk mambo ambayo mwakilishi wa benki ya dunia ameyaongelea kwenye magazeti ya leo ni umuhimu wa kuwa na 'muungano wa watu na taasisi za umma, asasi za kiraia na sekta binafsi' ktk kupambana na mambo yanayolikabili taifa ikiwemo la rushwa. Sasa ushirikiano huu hauwezi kuwepo bila kuwa na mfumo unaoeleweka uliowekwa kikatiba. Kinachoendelea ktk nchi yetu ni utashi wa mtu mmoja ambao sio endelevu kwa vile atakeyekuja hatakuwa na kikwazo chochote cha kubadilisha atakavyo.
 
Kwa hiyo mtoa post hizi taasisi huru zinajengwa huu ya mawe? Mbona marekani ambayo mnaichukulia kama reference wanastrugle kutafuta raisi makini au mzuri kwa process nyingi? Si wangechagua kichaa tu kwa sababu wana taasisi strong? Tu nataka rais strong ambaye anaconverge mawazo ya debates za watu na kutos msimamo Wa serikali.
Soma uongozi au management ndiyo utajua dhana hii. Soma kitu kinachoitwa bcg matrix katika uongozi kijana inaelekea umekalilishwa tu na akina lisu ambao hawajui management skulls.

Management ni science ndugu yangu na ni proffesion siyo kila mtu anaweza. Mnadannganywa na akina mtatilo vilaza wasioelewa lolote na nyie mdaka kama kasuku.
In a family of strong father the family will excell and viceversa is true. Ndiyo mana mdada anastrugle kutafuta Mme mwenye maamuzi mazuri vinginevyo angeolewa na yeyote au chizi.
You just lost my respect for failing kujenga hoja na kuanza personal attack...
 
Si nia yangu kugeuza huu mjadala kuhusu suala la wasichana wa shule kupata mimba na kuzaa kufukuzzwa shule, ila inanibidi kuliingiza kama mfano.

1. Serikali ya Tanzania ni mshiriki na imetia sahihi mkataba na agano la kimataifa la kulinda wasichana walio chini ya unmri wa miaka 18 na walioko mashuleni wenye kupata mimba.

2. Ilani ya Chama cha Mapinduzi inasema wazi kuwa Wasichana wa shule za msingi na sekondari wenye mimba na watoto watapatiwa huduma za elimu bila kufukuzwa.

3. SSera ya elimu inaruhusu waendelee na masomo.

Je "katika utawala wangu"ambao Rais Magufuli anasema ni marufuku kinyume na sera na mikataba tutalisemaje?
 
Back
Top Bottom